Tundu Lissu: Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uongo na udanganyifu


Tanzania haipo kihalali kwa kuwa zanziba hawakuridhia
 

kwa hiyo kumkosoa mzee wetu ni kumtukana ?
 
Tanzania haipo kihalali kwa kuwa zanziba hawakuridhia
Ile sahihi ya Mzee Abeid Amani Karume kwenye hati rasmi ya Makubaliano ni ya nini? Au kilikuwa cheti cha ubatizo kile!

Tanzania ilipataje kiti kule UN, OAU, NAM, CHOGM,....,?
 
kwani ukiambiwa we si mungu inamaanisha we ni shetani?yaliyopita si mbele ccm wajinga sana
Hili mbona liko wazi tu. Au kama wewe sio Simba basi ni Yanga kwa lugha rahisi. Hakuna cha Azam hapa ebo.
 
Maamuzi yeyote ya katiba yatategemea kura za BARA na za ZANZIBAR kivyake. Wanaoegemea hoja ya "umungu" wa Nyerere, wakafanye analysis na Zanzibar. Aliyotendewa Abdu Jumbe, Deurado na wengine na Nyerere yatawapa ugumu sana CCM Zanzibar. ..

Na UKAWA wameanzia Zanzibar! A deliberate move?? or a coincidence?!
 
Na UKAWA wameanzia Zanzibar! A deliberate move?? or a coincidence?!
Maeneo kama KibandaMaiti, MchambaWima ndio mahala pa kuanzia watu wa aina hii ambao shujaa wao ni Tundu Lisu.
 
Sidhani kweli kwa uchambuzi wa viongozi hapa duniani utamwita Nyerere mbinafsi na msaka umaarufu.
 
Kishimbe, ebu sikiliza hotuba ya Mwalimu alivyoongelea Azimio la Zanzibar. Hapakuwa na ridhaa pale maana hasingesema ilifanyika kwa siri, lakini kwa wenye akili tulijua tu Azimio la Arusha limezikwa.
 
Lissu ni mkristo wa kundi gani?
Wakatoliki ndio wanao muenzi zaidi Mwalimu.
Waislam wengi hawamuoni Nyerere kama mwema kwao..
Ccm wao wanatumia kina lake kujipandisha kwa wakatoliki.
Baba wa taifa ni title tu haifanyi kutomkosoa ni dhambi kama wanavo itikadi wakatoliki.
 
Ni kweli usiofichika kuwa Julius alishindwa kwa kila alilotabiri kwa asilimia 80 na sio sio 70 ni ukweli watu wasiotaka kuuona na jambo la kwanza unalotakiwa kulijua ni siri ya mwenge, serekali mbili mambo ya ajabu ajabu ila alikuwa dicteta hakuna ubishi juu ya hilo umemtaja Marehemu Babu ambaye alimwambia waziwazi " Yakhe wewe wapenda siasa za ewala Bwana"
 
wapo wasomi mbumbumbu wanaoshabikikia ujinga,kila nikiangalia bunge huwa naona kichefuchefu msomi mzima anaunga hoja upumbavu,eti serikali mbili,kisa yupo ccm,jamani niaibu kwa kwel,
 

Wasiotaka kukosoa ukweli ni wale wanaofaidika na uwongo.Kuna watu waliumizwa sana na utawala wake leo wakijitokeza sijui kama CCM watawafanya nini?Ni wengi mno.Unakumbuka wakati wauhujumu uchumi,je ni wangapi waliowekwa ndani walikuwa na hatia na wangapi walikuwa hawana?Je,waliruhusiwa kutetea au kufunguliwa kesi wajibu mahakamani?Ni kwa nini hawakupelekwa mahakamani,sababu hawakuwa binadamu?AU kwa sababu ya sheri alizokuwa anatunga yeye mwenyewe hazikuwa na impact kwa viongozi aliokuwa nao karibu bali watu wakawaida ndiyo alioumia,kuwekwa magerezani nk.

Kungekuwa na haki hata leo wanasheria wangeanza kuwatetea hawa waliodhulumiwa enzi za uongozi wa Mwalimu ili wapate haki zao hasa familia zao ambapo watoto walioswekwa ndani ndiyo walioumia kwa kukosa ada za shule,malazi,na hata chakula wazazi wao wakiwa jela.

Simlaumu Lissu hata kidogo ni bora ukweli utoke sasa kuliko baadaye.
 
mkuu jk ni dhaifu kuliko maelezo, na atatuacha vibaya sana, hebu chukulia hili la lukuvi lingetamkwa na mpinzani jumuia zote za kiislam mpaka mwisilam mmoja mmoja wangehamasishwa kulaani na kutoa matamko dhidi ya mtamkaji! Sasa hivi naona kimyaaaa au kuna jumuiya yoyote ya kiislamu iliyo laani tamko la Lukuvi?
 
Kimsingi suala la katiba mpya limekufa!Hii katiba inakosa Legitimacy km itaendelea bila ya kuwa na wawakilishi waliotoka kwani nao wanawakilisha watanzania wengi tu!Rais km ana hekima na wanaomshauri wanaona mbali angelivunja hili bunge tuendelee na katiba yetu ya 1977 ambayo ni manifesto ya CCM!!!!
 
Sijaona wala kusikia mtu ambaye ameweza (hata kujaribu) kuja na hotuba mbadala ya kupinga hoja za Tundu Lisu. Tena akitumia taarifa za kitafiti....Hadi hapo tutakapompata mtu wa namna hiyo, ila kwa sasa Lisua ataendelea kuwatesa wanafiki!
 
TISS ifanye mpango wamshugulikie lisu mapema!sijui kwa nini Kikwete anamchekea au ndio kawatuwa wazidi kumchafua mwalim?
 
Hakuna kitu kama kanuni ya imani kwa nyerere kuaminiwa, ubinadamu wake upo palepale, kinachowaudhi wengi juu ya hoja za kutapatapa za lissu ni jinsi anayotoa hoja zake as if what nyerere did 4 this country is useless wakati yeye ni product ya siasa makini na safi za huyo mzee wa watu...ukweli utabaki palepale..Nyerere sio na wala hatawahi kuwa malaika......lakini atabaki kuwa miongoni mwa viongozi na wanafalsafa bora kuwahi kutokea katika bara la Africa kwa kipindi chote alichoishi mpaka sasa
 
Sidhani kweli kwa uchambuzi wa viongozi hapa duniani utamwita Nyerere mbinafsi na msaka umaarufu.

Ubinafsi upo wa aina nyingi sio lazima kuwa wa mali tu bali hata kulazimisha mawazo yako kuwa ndio sheria.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…