Joseph lebai
JF-Expert Member
- Jul 19, 2017
- 8,452
- 8,670
Jana alilala nyumbani kwa mwalimu!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimekuuliza swali wewe kutokana na mchango wako wa kishamba sana, nawe unanitwanga swali! Jibu kwanza nijue kiwango chako cha umburura ndo turudi kumzungumzia TLKama anaamini hivyo anajipendekeza kwa sababu zipi?
Leo nimekumbuka hii ishu. Laana zakujitafutia mwenyewe.Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost
plus RIP John MagufuliRiP Mwalimu Nyerere
RiP Ben Mkapa
Chadema Lissu anapomkosoa hayati Mwalimu Nyerere wanadai ana haki ya kukosolewa kwa sababu ni mwanadamu. Which is true.Hivi kwanini viongozi wa Chadema Mbowe na Lissu wakikosolewa na ukajaribu kuelezea wanakosea wapi.Utatukanwa na kuitwa msaliti au kibaraka.
Hivi Mbowe na Lissu sio wanadamu wanaokosea?
Rudia kusoma nilichoandika.Sijasema Mbowe na Lissu hawataki kukoselewa.Nimeandika wakikosolewa basi wanachama na wapenzi wa Chadema watatukana ili kuonyesha kwamba viongozi hao hawakosei...sijawahi kumsikia Mbowe au Lissu amekataa kukosolewa.
..pia ni jambo la uhakika kwamba Mbowe, Lissu, na viongozi wengine wa upinzani, zaidi ya kukosolewa, wamekuwa wakitukanwa matusi makubwa, na kudhalilishwa, na viongozi na wafuasi wa Ccm.
Rudia kusoma nilichoandika.Sijasema Mbowe na Lissu hawataki kukoselewa.Nimeandika wakikosolewa basi wanachama na wapenzi wa Chadema watatukana ili kuonyesha kwamba viongozi hao hawakosei.
Utaitwa kila jina ukijaribu kukosowa .
Kwa namna hii wanufaika wa muunganobatili kwann lisu wasimchape risasi 16?Katika mwendelezo wa kupinga mawazo na mfumo wa utawala wa Mwl. Nyerere. Tundu Lissu amepasua jipu ambalo wengi huwa wanaogopa kulipasua pale aliposema kuwa Mwl. Nyerere alikuwa ni "msanii wa kisiasa" kwa sababu aliyokuwa anayasema siyo yale aliyokuwa anayatenda kuhusiana na suala la Muungano. Haya ameyabainisha wakati akitoa hoja kwenye Bunge Maalum
Mh. Tundu Lissu ameenda mbali na kusema, Mwl. Nyerere alizoea vya haramu na vya halali hakuviweza. Katika kuthibitisha maneno yake, Mh. Tundu Lissu alisema, mwaka 1968, Mwl. Nyerere aliudanganya ulimwengu pale aliposema kupitia gazeti la Observer la UK, ?Iwapo umma wa Zanzibar bila ya ushawishi kutoka nje, na kwa sababu zao wenyewe, wataona kuwa Muungano una hasara kwa uhai wao, sitawapiga mabomu kuwalazimisha......Muungano utakuwa hauna tena sababu ya kuendelea iwapo washiriki wake wataamua kutathmini na kuthibitisha jambo hasa tukio la kihistoria kama Muungano'
Mwaka 1984, Wazinzibari walipohoji Muungano, Alhaji Aboud Jumbe akafukuzwa kazi kwa amri ya Mwl. Nyerere na amewekwa kizuizini Mjimwema mpaka leo. Wolfgang Dourado akawekwa kizuizini, Bashiri Swanzy akapakiwa kwenye ndege ya kwanza akapelekwa Ghana
Mh. Tundu Lissu aliendelea kusema, kwa vile Mwl. Nyerere alizoea vya kunyonga, kwenye Kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania, Mwl Nyerere alisema, 'huko nyuma baadhi ya viongozi wapinzani wa Muungano wameishawahi kusema tufanye referendum kwa Zanzibar kuhusu Muungano, tukakataa kwa sababu safi kabisa'.
Tundu Lissu anadai, Mwl. Nyerere hakukataa hoja ya Muungano kwa sababu safi kabisa, bali aliwaweka kizuizini wale waliohoji Muungano. Mwl. Nyerere alizoea kuishi kwa uwongo na hakuweza kusema kweli.
Kitu muhimu kabisa cha kujiuliza na kufikiria. Kama kweli Mwl. Nyerere alikuwa anaishi kwa uwongo na udanganyifu, ina maana hata hati ya Muungano haipo na kama haipo, ina maana amewaingizwa 'mkenge' wananchi na hasa wanaCCM kwa kusimamia hoja ambayo kiuhalisia haipo. (Muungano wa serikali mbili).
Tukikubaliana na hoja ya Tundu Lissu, inabidi tujiulize, Kwa nini Baba wa Taifa alikuwa anaishi maisha ya uwongo na udanganyifu?. Alikuwa anafanya hivyo kwa manufaa ya nani?.
Kama hoja ya Tundu Lissu ni kweli basi hatuna budi kusema, kweli uwongo hupanda lifti wakati ukweli hutumia ngazi kuwafikia walengwa!.
Hoja hii inanipeleka kwenye angalizo la sababu ya baadhi ya wajumbe wakiongozwa na Leticia Nyerere kushauri bunge kwa nguvu zote liweke mipaka kwenye kanuni za bunge zikiwataka wabunge kutowadhalilisha waasisi wa Muungano. Kumbe nyuma ya hoja zao walikuwa wanaogopa ukweli usijulikane!.
Mpaka katiba mpya ipatikane, tutaona na kusikia mengi!.
Kauli mbiu ni serikali moja au kila nchi ichukue fito zake kwa sababu watu tuliowatuma kwenda kumalizia mchakato wa katiba kwa sasa wanahoji uhalali wa Muungano huku wakitaka mpaka makaratasi yenye sahihi za waasisi wa Muungano. Hawa wabunge wameshindwa kufanya kazi ya kumalizia mchakato wa Katiba badala yake wanaanza kuuliza kama Muungano ni halali au batili. Yaani baada ya Miaka karibia 50 ndiyo tunaanza kuuliza Muungano kama ni halali huku waasisi wa Muungano tukiwasema ni waongo na wadanganyifu.
Ninadhani kuna kitu hakiko sawa kwenye baadhi ya hoja za Wabunge!.
[video=youtube_share;bB7BxxMepR8]
[video=youtube_share;jE7oTPXtpas]