Uchaguzi 2020 Tundu Lissu na CHADEMA hawana Ilani?

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu na CHADEMA hawana Ilani?

Nazgur

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2020
Posts
3,729
Reaction score
2,851
Habari wana jamvi,

Nimekuwa nikifuatilia mikutano yote ya CHADEMA, mara nyingi wanakuja na hadithi mpya na nyingi zinatungwa na washabiki wao hapa JF kisha mgombea anapanda nazo jukwaani.

Je, Chadema hawana Ilani yao? Nimejaribu kuingia Google lakini nimeona ya mwaka 2015. Je, mpya bado haijachapishwa au bado ipo kwenye vimakaratasi?

Kuna jambo lililetwa na mwana JF hapa kuwa kuna kifungu kwenye katiba yao kinasema kitatungiwa Sheria kwamba endapo mwanamke atalalamika police kuwa mwanaume amefanya mapenzi nae bila ridhaa yake basi atakuwa amebaka.

Tulitaka ufafanuzi wa jambo hilo kwa mgombea, atuambie je huyo mwanaume yeye atakuwa na haki gani ya kujitetea endapo atakuwa amesingiziwa au ananyanyaswa na huyo mwanamke?

Pia, kuna kifungu 84 cha madini ambacho kimeongelewa na ndugu pole pole kuhusu rasilimali madini kuwekwa rehani.

Je mgombea anasemaje juu ya hilo na tunataka kusikia akikisoma kutoka kwenye ilani yake na si majibu ya mtaani.

Pia, Chadema ilani yenu si mkataba kwa wananchi bali ni maneno ya kwenye mitandao ndio ilani yenu?

Tunataka majibu hayo, kwanini hamtembei na ilani yenu kama reference ya mnachoongea na mkitupa ufahamu kuwa hayo yanatokana na kifungu gani kutoka kwenye Ilani yenu ili tuwaamini?

Chadema na mgombea wenu acheni dharau kwa wananchi, toeni ilani ili tujue kilichomo.
 
Aibu kubwa sana kwa mgombea wa Chadema anasikiliza hoja za wafuasi wake wa JF! Mfano wanamuambia eti kujenga SGR si lolote si kitu hata mkoloni alijenga reli. Yeye anakurupuka na kuongea upuuzi kama huu majukwaani! Yaani hajui umuhimu wa mradi wa SGR ukikamilika!
 
Hivi naachaje kumchagua Lissu wakati ana Sera ya kumsomesha hata mwanangu ambaye nimemsomesha private?

Hivi naachaje kumchagua Lissu ambae anarudisha makato ya mikopo ya bodi ya mikopo kutoka asilimia 15 ya magufuli hadi asilimia 6?

Hivi naachaje kumchagua Lissu ambaye ametoa sera ya kunijali mimi mlipa kodi na mfanyabiashara kwa kuniwekea mswada wa kunilinda mimi mlipa kodi ili TRA wasininyanyase?

Hivi naachaje kumchagua Tundu Lissu ambaye hataniwekea mipaka kwenye masoko ya kuuza mazao yangu niliyoyalima kwa jasho kubwa?

Hivi naachaje kumchagua Tundu Lissu mwenye Sera ya kurudisha katiba mpya ya warioba itakayoweka misingi ya utawala bora na kuondoa matumizi mabaya ya madaraka?
 
Ilani Ipo mkuu Ilani Iliyopo Mgombea urais anainadi vizuri sana.

Tundu Lissu anasema "hii alani ni Agano au Covenant kati ya CHADEMA na watanzania" anaahidi kuisimamia na kuitekeleza ilani kisawa sawa.

Inasikitika kama hadi leo hujaisoma mkuu
Ama unashabikia vyama na si sera????
 
Ilani Ipo mkuu Ilani Iliyopo Mgombea urais anainadi vizuri sana.

Tundu Lissu anasema "hii alani ni Agano au Covenant kati ya CHADEMA na watanzania" anaahidi kuisimamia na kuitekeleza ilani kisawa sawa.

Inasikitika kama hadi leo hujaisoma mkuu
Ama unashabikia vyama na si sera?
Atusomee kifungu cha 84 alichokisema polepole, pia sijawahi kuona hata siku moja akisoma kutoka humo kwenye ilani.
Hata kuionyesha tu.
 
Wewe
Hivi naachaje kumchagua Lissu wakati ana Sera ya kumsomesha hata mwanangu ambaye nimemsomesha private?

Hivi naachaje kumchagua Lissu ambae anarudisha makato ya mikopo ya bodi ya mikopo kutoka asilimia 15 ya magufuli hadi asilimia 6?...
KAtiba mpya unanufaikaje nayo bwashee kama sio maana siasa?
 
Tunataka kuona Yale anayo yasema yanatoka kwenye kifungu gani katika ilani yao na sio hadithi tu
Maana kwenye mtandao haipo sasa wengine tutaisoma wapi?
Hata wabunge wa chadema hawana labda wanapewa vipeperushi tu.
Chadema acheni usanii
Ziwekeni hadhalani tuzijadili.
 
Ilani Ipo mkuu Ilani Iliyopo Mgombea urais anainadi vizuri sana.

Tundu Lissu anasema "hii alani ni Agano au Covenant kati ya CHADEMA na watanzania" anaahidi kuisimamia na kuitekeleza ilani kisawa sawa.

Inasikitika kama hadi leo hujaisoma mkuu
Ama unashabikia vyama na si sera????
Kama ipo twambie kifungu hicho alichokisema polepole je ni kweli mnaweka Mari zetu rehani? Na kwa mda gani?
Tuwekee hapa kama wewe unayo hiyo ilani.
 
Na bado...mtapigwa spana mpaka mtakunya mwaka huu. Si mlikuwa mnasema chadema imekufa lleo unahaha kutafta ilani ya chadema ili muanze kuicopy.
 
Na bado...mtapigwa spana mpaka mtakunya mwaka huu. Si mlikuwa mnasema chadema imekufa lleo unahaha kutafta ilani ya chadema ili muanze kuicopy.

😁😅😆😀😜 Lumumba wana haha hasa ,Moto kila mahali na wamekosa pa kushika.
 
Tunataka kuona Yale anayo yasema yanatoka kwenye kifungu gani katika ilani yao na sio hadithi tu
Maana kwenye mtandao haipo sasa wengine tutaisoma wapi?
Hata wabunge wa chadema hawana labda wanapewa vipeperushi tu.
Chadema acheni usanii
Ziwekeni hadhalani tuzijadili.
Ili muifanyie copy and paste
 
Ilani Ipo mkuu Ilani Iliyopo Mgombea urais anainadi vizuri sana.

Tundu Lissu anasema "hii alani ni Agano au Covenant kati ya CHADEMA na watanzania" anaahidi kuisimamia na kuitekeleza ilani kisawa sawa.

Inasikitika kama hadi leo hujaisoma mkuu
Ama unashabikia vyama na si sera????
Wanashindwa kusimamia michango ya wanachama na wabunge mpaka wanalalamika sembuse wataweza kusimamia fedha na maisha ya watanzania kweli msitanie watu.
 
Habari wana jamvi,

Nimekuwa nikifuatilia mikutano yote ya CHADEMA, mara nyingi wanakuja na hadithi mpya na nyingi zinatungwa na washabiki wao hapa JF kisha mgombea anapanda nazo jukwaani...
Yaaanii wanatia huruma, utasikia Leo wanaponda ujenzi wa miundombinu ya maendeleo, kesho wakiamuka kivingine, utasikia wanasema eti nao watajenga na kufufua viwanda. Yaaanii hatujui wanamalengo gani na taifa hili.
 
Tunataka kuona Yale anayo yasema yanatoka kwenye kifungu gani katika ilani yao na sio hadithi tu, Maana kwenye mtandao haipo sasa wengine tutaisoma wapi?....
Wewe hayakuhusu kwani tayari uko upande ule wa fiesta
 
Back
Top Bottom