Tundu Lissu na fimbo yake kama Musa kwa Farao

Tundu Lissu na fimbo yake kama Musa kwa Farao

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Katika siasa huwa kuna symbolism au utambulisho wa kisiasa na kimamlaka.

Ukisoma maandiko utakutana na nabii mkubwa kabisa wa wana wa Israel Musa akiwa na fimbo yake ambayo kama tunavyofahamu ilitumika kupitishia miujiza mikubwa kabisa ya Mwenyezi Mungu.

Hapa kwetu Tundu Lissu na yeye amejikuta akishikilia fimbo kila afanyapo mkutano. Naamini hiyo fimbo inamsaidia Lissu kumpa sapoti kutokana na kujeruhiwa sana kwa risasi kwenye miguu yake, lakini sisi wadadisi wa mambo tumegundua kuwa hiyo Fimbo pia inasaidia sana kumpa haiba Tundu Lissu.

Hii Fimbo inanikumbusha fimbo ya Musa kwa Farao, na inasymbolize ukombozi kwa Watanzania kutoka katika mikono ya udhalimu na utawala uliojaa jeuri na kiburi wa CCM.

Kwa jamii za Wafugaji, Fimbo hutumika kwa kujilinda dhidi ya wanyama wakali, kujilinda dhidi ya adui na kuihami familia. Fimbo ni alama ya heshima kwa mwanaume.

Nawapongeza sana waliomchagulia Lissu mavazi, Ile Lubega anayovaa kwenye mikutano yake na Fimbo anayoshika ni Ishara ya utamaduni wa mwafrika na inaonyesha kuwa yuko tayari kubeba majukumu ya Ukuu wa Kaya.

Lakini hii Fimbo ya Lissu , kama ilivyokuwa fimbo ya Musa inaashiria mwisho wa utawala mbaya kabisa wa JPM

Lissu hiyo fimbo usiiache popote utakapokuwa kwenye shughuli hizi za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu!

 
Tanzania Politics on transformation. Kwa miaka mingi Tanzania imekua ikisubiri aina hii ya siasa na wanasiasa wa aina hii.
Sipati picha siku Lissu, Mbowe, Msigwa, Lema na wale akina mama watakapoanza kusimama pamoja kwenye majukwaa ya kampeni.
 
Tanzania Politics on transformation. Kwa miaka mingi Tanzania imekua ikisubiri aina hii ya siasa na wanasiasa wa aina hii.
Sipati picha siku Lissu, Mbowe, Msigwa, Lema na wale akina mama watakapoanza kusimama pamoja kwenye majukwaa ya kampeni.

Hizi siasa ndizo zinazotakiwa!

1. Ondolea credibility Jiwe kutokana na namna alivyoendesha nchi hii kwa miaka mitano
2. Nadi sera mbadala hasa za kiuchumi

Combination ya hivyo vitu viwili vitaclick sana kwa wananchi!
 
Tanzania Politics on transformation. Kwa miaka mingi Tanzania imekua ikisubiri aina hii ya siasa na wanasiasa wa aina hii.
Sipati picha siku Lissu, Mbowe, Msigwa, Lema na wale akina mama watakapoanza kusimama pamoja kwenye majukwaa ya kampeni.
Kwani wote hao hawakuwepo miaka yote? Au wewe Ni mgeni wa siasa?
 
maji ya bahari kuchemshia nyama ili unywe supu kisa yana chumvi ni ulofa na ujinga uliopitiliza,
 
Back
Top Bottom