Elections 2010 Tundu Lissu naye mwendo mdundo...!

Elections 2010 Tundu Lissu naye mwendo mdundo...!

Slaa alisema lissu ndio mrithi wa mikoba yake bungeni - ngoma inogile mjengoni ididomya!
 
Tundu Lissu, mwanasheria machachari ambaye amekuwa anaichachafya CCM kuhusu mikataba mibovu ya madini, ameshinda katika jimbo lake ila NEC inashindwa kumtangaza kwa sababu mpinzani wake anataka masanduku yafunguliwe kura zihesabiwe tena. Lissu anagoma kwani anasema sheria ya uchaguzi inamlinda -- huwezi kuhesabu kura wakati masanduku yalilala usiku kusikojulikana. Anasisitiza matokeo ya vituoni yaliyokuwa yamehakikiwa na wakala wa vyama na kusainiwa ndiyo yatangazwe.

Lissu amebana humo humo katika chumba cha kuhesabia kura na kitabu chake cha sheria ya uchaguzi ambacho tayari kakifungua ukurasa husika na kuweka juu ya meza.

Inasemekana CCM inamuoigopa sana Lissu, haimtaki akaingia Bungeni. CCM inaona ni bora hata akina 'Slaa" watano warudi Bungeni kuliko Lissu mmoja.

Safi sana hiyo CCM wezi na mwaka huu lazima watakiona cha mtema kuni kilichomtoa kanga manyoya.
 
welaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa. nimatokeo pekee niliyokuwa nikiyasubiri mno siku ya leo.ccm kazi ipo
 
Jamani wapendwa mwenye link ya Radio naomba anipatie niweze kujua kinachondelea maana nipo ofisin hakuna radio zaidi ya computer. Nisaidieni wapendwa
 
Kabila na Njowepo, hamnnishindi mimi...!! Nina hamu ya kupata confirmation kuwa kashinda, nimeshapata tetesi za ushindi wa mpiganaji huyu...!!
 
ndizo nazosubiri kwa hamu kubwa aisee
 
Mtanzania la leo linasema TUNDULISU ameshinda.
 
msiwe na hofu ameshinda. LISU Ni KISU kwa CCM. Mpiganaji wa dhati:nono::smile-big:
 
Waungwana wenye hamu ya kujua matokeo ya Mh. Antipasi TUNDU LISU, Ukweli ni kwamba sikukosea kumuita Mh. kwa maana it has been vehemently confirmed that TUNDU LISU has won the consistuency. Hivyo shak ondoa, mpiganaji wetu atakuwa mjengoni soon. thanks
 
Matokeo ya mwaka huu yanaonyesha dhahiri watu wanaanza kubadilika.
 
Kabila na Njowepo, hamnnishindi mimi...!! Nina hamu ya kupata confirmation kuwa kashinda, nimeshapata tetesi za ushindi wa mpiganaji huyu...!!
Na mimi nina hamu ya kujua huyu mpiganaji kafikia wapi
 
Back
Top Bottom