Tundu Lissu: Ni mzee Mwinyi pekee ambaye hakuwanyanyasa Wapinzani/ Wananchi kwa kutumia Mapolisi katika Utawala wake

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lisu amesema Chanzo Cha Marais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kutumia Mapolisi kuwanyanyasa Wapinzani wao alikuwa ni Mwalimu Nyerere.

Lisu anasema ni Rais Mwinyi pekee ambaye hakuwanyanyasa Wapinzani au Wananchi kwa kutumia Mapolisi

Source: Star tv

My take; Nakubaliana na Lisu kuhusu Mzee Mwinyi

Mlale Unono πŸ˜€πŸ˜€
 
ni kwasabb wakati huo wapinzani hawakua na kiburi na ukaidi wa kutiii sheria bila shuruti kama yeye na wapinzani wenzie πŸ’
 
Mwinyi alikuwa raisi kwenye kipindi ambapo siasa za upinzani hazikueleweka kwa kuwa wengi wakiamini upinzani ni vita na ukoloni ungerudi kitu ambacho ccm hawakuona tishio la kupokwa madaraka kidemokrasia. Kwasasa bila hawa mapolisi hakuna mgombea wa ccm atakayepata kura
 
ni kweli, ila ndio aliongoza kwa kunyanyaswa na wapinzani, akina mbatia wakati wako daruso walimchora zile katuni waliita mzee punch,

ni mwinyi alinaswa kibao msikitini akiswali na hao wapinzani. alitukanwa na kukejeliwa wakimwita gabacholi tx mgeni kutoka unguja, je tuendelee kuvumilia hizi kejeli? wahenga walisema akifanya mazoea na mbwa atakufuata msikitini, sasa hatutaki mazoea na mbwa akaja tunasa vibao msikitini,
 
Tundu kama anapagawa vile hivi kulikuwa na chaguzi za vyama vingi enzi za mwinyi?
 
Huyu ameshavuta gawio inaonekana, ni suala la muda tu
 
Kwa hiyo tutarajie huko zanzibar 2025 yale ya 2020 hayatatokea?
 
Mzee alijua Dunia tunapita Kila mtu Aishi atakavyo na tule kilichopo wotee..hakutaka kashikashii za damu za watuu
Na ndio maana ameishi Maisha marefu sana kuliko Wengi hapa Tz.
 

..unataka kusema Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu alinaswa kibao na wapinzani wakati akiswali Msikitini?! Kweli?!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…