Tundu Lissu: Ninahofu kuhusu uchaguzi mkuu wa CHADEMA lakini dawa ni moja tu

Tundu Lissu: Ninahofu kuhusu uchaguzi mkuu wa CHADEMA lakini dawa ni moja tu

Muongo huyo, hapo anazuga tu kwa kuwa kuna uchaguzi unakuja.
Mtu ameshatangaza wazi kuwa chadema siyo mama yake au baba yake, atabaki chamani namna gani?
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Unampangia cha kusema?.
Kati ya Mbowe na Lissu nani mroho wa madaraka?.
Tumia hata akili zako kwa 1% basi.
 
HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.
Mtu mwongo sana hyu wala msimuamini hata kidogo.........wenye akili hawawezi kumwamini

Sikiliza unaweza kumwamini mtu kama huyu? This is a rubbish person!
 

Attachments

  • SINA MPANGO WA KUGOMBEA UENYEKITI LISU.mp4
    7.1 MB
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu A.M. Lissu amesema kuwa ana hofu kubwa juu ya mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika juma lijalo.

Lissu ameyasema hayo katika kipindi cha runinga cha Crown Media kijulikanacho kama Kasri la Kikeke kilichoongozwa na Salim Kikeke. Lissu amesema kuwa kulingana na yanayoendelea kuelekea uchaguzini, mtu yeyote timamu lazima awe na hofu.

Lissu ameongeza kusema kuwa kwasasa CHADEMA imegawanyika katika pande mbili-ya Mbowe na Lissu...mgawanyo unaotishia mustakabali wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.

Kuhusu dawa ya kuzuia suitafahamu inayoweza kujitokeza baada ya uchaguzi, Lissu amesema kuwa dawa pekee ni kuwa na uchaguzi mkuu wa CHADEMA huru, wa haki na wa wazi.

Yetu macho na masikio!
Mbona Lissu ameishakubaliana na Mch. Msigwa kwamba akishindwa anaenda CCM? Hizi taarifa mbona sio ngeni Lumumba?
 
Huyo Lisu kawaida yake kulia lia, kabla ya kugombea urais TLS alipiga kelele sana, akashinda hakuna lililofanyika, yeye ni Makamu mwenyekiti hata haelewi nafasi yake anapaswa kufanya nini, maana hata ukimuuliza yeye kafanya nini tangu ashike hiyo nafasi haelewi, waulize wafuasi wake sasa, utaambulia matusi asubuhi mpaka jioni lakini nao hawana jibu.

Halafu wanakwambia Lisu ni kichwa anapaswa awe mwenyekiti, afanye nini, alichoshindwa kukifanya sasa?

Leo anagombea uwenyekiti chadema anajiona ni malaika aliyeshuka, lakini yeye ndiye huwa anahujumiwa tu kila siku, kila mahala, na keshaanza kulilia anatilia mashaka matokeo hata uchaguzi haujafanyika.

Labda atashinda, sasa ukiwauliza wafuasi wake atafanya nini, eti atakomesha Rushwa za Mbowe, Wakati hata sasa hawana ushahidi wowote wa Mbowe kupokea rushwa, wanasema Abdul na Mama yake, ushahidi hawana.

Lisu anawaburuza lakini watajuata ikitokea bahati mbaya akashinda.

Mini nashauri afukuzwe akishindwa, ili abebe wafuasi wake waende waendako, na wakiweza waanzishe chama chao.
Unafikiri Kwa kutumia kichwa kipi?
 
Muongo huyo,
Amekuwa akiwapaka kila mtu asiyemuunga mkono yeye, atabaki chamani namna gani akishindwa?
Lisu yuko chadema ili kuridhisha tamaa yake ya uroho wa madaraka tu, asipoyapata atatimuka mara moja!
Uko sahihi
Kwa siasa za Tanzania kwa sasa hakuna mtu muongo kama Lisu

Akishindwa tu uchaguzi anahama Chadema huyo
 
Hakuna cha kunywa maji wala soda, huo ni ukweli mtupu tunasubiri utimilifu wake tu. Aliposema chadema siyo mama yake wewe unadhani alimaanisha nini, kama siyo kuwa mguu mmoja ndani na mguu mwingine nje?
Kwahiyo alivyosema hivyo wewe ukateseka?

Pole sana, hakuna cha ajabu kwenye siasa. Najua una mambo mengi ya kusubiri badala ya huo utimilifu wa jambo ambalo siasani hata si la ajabu kabisa.
 
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu A.M. Lissu amesema kuwa ana hofu kubwa juu ya mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika juma lijalo.

Lissu ameyasema hayo katika kipindi cha runinga cha Crown Media kijulikanacho kama Kasri la Kikeke kilichoongozwa na Salim Kikeke. Lissu amesema kuwa kulingana na yanayoendelea kuelekea uchaguzini, mtu yeyote timamu lazima awe na hofu.

Lissu ameongeza kusema kuwa kwasasa CHADEMA imegawanyika katika pande mbili-ya Mbowe na Lissu...mgawanyo unaotishia mustakabali wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.

Kuhusu dawa ya kuzuia suitafahamu inayoweza kujitokeza baada ya uchaguzi, Lissu amesema kuwa dawa pekee ni kuwa na uchaguzi mkuu wa CHADEMA huru, wa haki na wa wazi.

Yetu macho na masikio!
Katika majaribu makubwa ambayo CDM imewahi kuyapitia, hili la uchaguzi wa M/Taifa ni mojawapo. Kwa kuwa limeshikilia mustakabali mpana wa chama hiki kwa siku zijazo.

Nafikiri Mwenyekiti anayemalizia muda anapaswa kujitathimini mwenyewe juu ya nia yake ya kuendelea kukishikilia cheo hicho. Ndiyo! Ameweka alama nyingi za kukumbukwa katika chama, lakini msanii bora hutambua vyema wakati sahihi wa kupanda na kushuka jukwaani.

CDM kweli imegawanyika, lakini inahitaji uongozi mpya ili kuleta hamasa mpya kwa wananchi. Maridhiano aliyoyafanya Mbowe yanaonekana hayaungwi mkono hata kidogo na wanachama wengi, na tena kuna hisia ya yeye kuhusishwa na pesa chafu kuingizwa katika mchakato wa uchaguzi unaoendelea hivi sasa.

Ili kulinda heshima yake kubwa aliyojijengea ndani na nje ya CDM kwa muda wa miaka zaidi ya 30, nafikiri ni muda sahihi kwa M/Kiti Mbowe kushuka jukwaani ili kumpisha mtu mwingine katika nafasi hiyo.

Atakuwa ameamua kutoka jukwaani kwa wakati uliostahili kama vile ambavyo alivyoingia kwa wakati stahili. Kutenda ni kuamua, na majuto ni mjukuu.

Beware!👆
 
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu A.M. Lissu amesema kuwa ana hofu kubwa juu ya mustakabali wa CHADEMA baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika juma lijalo.

Lissu ameyasema hayo katika kipindi cha runinga cha Crown Media kijulikanacho kama Kasri la Kikeke kilichoongozwa na Salim Kikeke. Lissu amesema kuwa kulingana na yanayoendelea kuelekea uchaguzini, mtu yeyote timamu lazima awe na hofu.

Lissu ameongeza kusema kuwa kwasasa CHADEMA imegawanyika katika pande mbili-ya Mbowe na Lissu...mgawanyo unaotishia mustakabali wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Alipoulizwa iwapo atashindwa uchaguzini atafanya nini na kama atahama au la, Lissu amesema akishindwa atakuwa hajawahi kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA na HATAHAMA chama hicho na atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa CHADEMA.

Kuhusu dawa ya kuzuia suitafahamu inayoweza kujitokeza baada ya uchaguzi, Lissu amesema kuwa dawa pekee ni kuwa na uchaguzi mkuu wa CHADEMA huru, wa haki na wa wazi.

Yetu macho na masikio!
Nilikuwa Kariakoo na sasa Arusha kila mtu anamtaka Lissu Mbowe ajitafakari.
 
Back
Top Bottom