kirengased
JF-Expert Member
- Jan 10, 2016
- 6,348
- 7,058
Tumejifunza Rwanda wamejaribu wameweza hao wengine hatuwafatishi na hatuogopi kukosea maana tutakuwa tumejifunza kumbuka kukosea sio kushindwa na hatukati wala hatukatishwi tamaa! we learn from the best...Ndege zinazeeka na hivyo zitahitaji vipuri ambavyo ni bei sana ( pengine hujui: vipuri vya ndege vina expire date.)
Mashirika makubwa yanafungwa kwa kushindwa hii biashara. Kujaribu si kubaya lakini kujaribu tu ili mradi uonekane umejaribu ni jambo la ajabu kabisa.
Mbona ameshasema atawafanyia Nini,Tena kaanza kusema juu ya wakulima na wafugaji.Umeiaikiliza vizuri hotuba yake?Kosa kingine kwa Tundu lissu
Lissu hatakiwi kumshambulia Magufuli
Lissu anatakiwa atuambie atafanya Nini,kukomaa na Magufuli ni sawa na kuzidi kujipunguzia kura tu
Hivi kujenga hospital kubwa 69 sio maajabu
Kukarabati shule za sekondari ambazo haziguswa toka mkoloni si maajabu
Chadema mjipange sana na lissu wenu mtajikuta mmeishiwa maneno baada ya wiki moja tu toka kuanza kampeni
Mkuu huo sio utani jamaa alichoandika ni kweli, nasisitiza si utani.Unataka kutuambia Marais wote walio pita hawakuwahi kununua ndege? Wakati kuna walio nunua tukala majani?
Kwamba shule hazikuwepo? Mimi nilisoma Uarabuni?
Kwamba hosipitali hazikuwepo tulitibiwa wapi? Hebu tuache utani kwenye mambobya msingi jamani.
Magufuli vs Lissu, who is the best??Yote uliyoorodhesha Nyerere aliyafanya vyema kuliko Magufuli.
Na bado Nyerere hakuthubutu kujenga Uwanja Wa Ndege Kule Butiama.
Nakubaliana na wewe hajajenga nidhamu makazini,Bali kajenga woga na hofu kwa wafanyakazi.Hakuna nidhamu wala nini, ni kuwa watumishi ni waoga! Nidhamu ya woga, wakiachiwa tu watalipiza kisasi!
Hahaha mkuu umenichekesha sanaKuna nidhamu gani kazin we kima. Watu wanaiba tena sana na undugunization ndo umeongozeka kwa sbb ya kutoajiri miaka mitano. Hivi jpm ni mtu au ni jitu
Kama hayo kweli ameongea lisu basi miongoni mwa wagombea ambao kichwani ni zero huyu anaongoza. Hiyo mbuga unaihamishaje kutoka sehemu moja kwenda nyengine? Mwambieni azungumzie issues zitakazowatoa wafuasi wake hapo walipo kiuchumi.Tundu Lissu akihutubia mamia ya wafuasi wa Chadema na wananchi wasio na itikadi ya chama chochote mkoani Dodoma ametoa hoja kali ambazo CCM hawana uwezo wa kuzijibu zaidi ya kupanic na kukimbilia kwenye vyombo vya habari viwahurumie wasirushe mikutano ya Tundu Lissu.
Mosi, amezungumza kuwa jipya na la ajabu kwenye utawala huu ni Rais kujenga uwanja mkubwa Chato wakati marais waliopita hawakufanya maajabu haya, amesisitiza Tundu Lissu.
Pili, ni kitendo cha Rais kupeleka mbuga Chato. Hili ni ajabu kuu ambalo halijawahi kufanyika amesisitiza Tundu Lissu.
Tatu, Lissu amesisitiza kuwa watu wamedhalilishwa, hasa viongozi wa serikali na akina Mama kwa kauli chafu zinazotolewa.
Lissu amesisitiza hii nchi sio kila mtu ni mjinga na unaweza kuwadanganya kirahisi. Kuna watu werevu na wanakwenda kuwaambia wananchi kwa miaka mitano madudu yaliyofanyika.
Je, haya maajabu ni kweli yamefanyika huko Chato?
Je,wakazi wa Lindi, Dodoma, Mbeya, Ruvuma, Arusha, Mtwara, Kilimanjaro mnafahamu maajabu haya ya huko Chato?
Kwa hoja hizi ambazo hata mimi sikuzijua kwa miaka mitano, sasa nimeamshwa usingizini.
Hoja haipigwi rungu, bali hujibiwa kwa hoja. Hii ni kauli ya Dkt Jakaya Kikwete
CCM oyeee oyeeee oyeeee, jibuni hoja hizo!
Kuna haja kubwa kuweka kigezo kinachomtaka mgombea urais awe ametembelea wilaya zote za nchi , hiyo itawasaidia kujua magnitude ya KAZI wanayoiomba. Waingereza wanasema TO SEE IS TO BELIEVE.haoni reli? haoni madini? haioni dodoma? haoni ndege? haoni vituo vya afya? haoni meli? haoni elimu bite, haioni ubungo? haoni majizi kushughulikiwa? haoni makusanyo yakodi kuongezeka? haoni ccm safi? Nk. Nk. Haoni??
akatafute shughuli nyingine ya kufanya, akaombe hko ulaya ama ajiajiri mahali
Siyo ubinafsi,hiyo ni rushwa na matumizi mabaya ya Mali ya umma.Unajiuliza huo uwanja wa chato unajengwa ili uhudumie kina nani hasa?Je,ni kipaumbele cha nchi au Jiwe na chato yake?Kosa kubwa la Magufuli ameenda Chato ndani kujenga uwanja mkubwa wa ndege huku akijua kuwa hauna faida yoyote zaidi ya hasara. Yani ni kama kwa mfano Tundu Lissu awe Rais kisha akajenge uwanja mkubwa wa ndege Ikungi.
Ukiwa unaenda Chato unaupita mji mkubwa wa Geita kisha unaenda mji mdogo wa Katoro then Chato. Yani sijui alitumia findings zipi kujenga huko Chato! Sijui!
Yani ni kama marehemu Mkapa airuke Mtwara mjini, airuke Masasi mjini kisha aende Lupaso akajenge uwanja mkubwa wa ndege. Huu ni ujinga wa aina yake.
Maendeleo gani hayo mbona sisi hatuyaoni mnatumia darubini gani kuyazoom hayo maendeleo?Fatilia viongozi wa mageuzi kina Mohammad rajah Al mahtoom, Putin, J. zemin nk. Hakunaga maendeleo bila kuumia, Kama mwanaume ulitahiriwa Kama mwanamke Alizaa basi hujua hilo!! Chamuhimu malengo ya JPM ni Tanzania yamaendeleo tena yakasi
Haya na atawale baada ya Magufuli kumaliza muda wakeKwa hoja Lissu is the Best.
Kiutendaji Magufuli amejaa ubinafsi na kupenda kuabudiwa kiasi amekaa kimya alipofananishwa na Masihi Wa Bwana.. Ameshindwa kuleta Umoja Wa Kitaifa kwa kupendelea Kanda yake zaidi.
Lissu utendaji wake kwenye sheria sote tumeona jinsi anavyotetea wanyonge dhidi ya sheria kandamizi za Serikali ya Magufuli.
Bora Lissu.
Bunge lilipitisha?Mmeanza kumezeshwa maujinga kichwani na tundu? Chato hainahaki kujengwa uwanja wa ndege? Mbona KIA Ipo vijijini? Endeleeni kumskiliza huyo mropokaji asiyeweza kuona mazuri ya wengine.
Kwani hakukuwa na reli? Tazara, reli yaa kati?haoni reli? haoni madini? haioni dodoma? haoni ndege? haoni vituo vya afya? haoni meli? haoni elimu bite, haioni ubungo? haoni majizi kushughulikiwa? haoni makusanyo yakodi kuongezeka? haoni ccm safi? Nk. Nk. Haoni??
akatafute shughuli nyingine ya kufanya, akaombe hko ulaya ama ajiajiri mahali
Kwa hiyo na Lisu nae ni Mchaga?Chadema wanataka maendeleo yaende kaskazini peke yake. Mfundisheni Lissu Siasa bado mchanga sana. Siasa siyo sheria.
Mukato!!Ati huyu.. anataka kuongoza nchi hii!!!.. mipasho mipasho ipo kwa damu yake. Yeye anataka kuongoza.. ili akae Ikulu.. kupiga mipasho kwa Mh. Magufuli.. anaonyesha ana wivu sana na mafanikio ya Magufuli.. wivu mubaya sana.. nyie munao mushangilia humu.. ni basi tu hamuwezi badili gia angani.. humu ila rohoni kura kwa Magufuli.. tumewazoea.. 2010.. 2015.. πππ si mukubali kwamba anawatia aibu.. nyie wafuasi wapenda maisha ya mukato.. aliyoziba Rais wenu mpendwa JPM.. yaani hana hata sera.. akiwongea ni upupwu tu anashusha.. BTW akimaliza mazoezi tarehe 27 Okitoba 2020.. atakwenda shangilia kumaliza ndoto ya kupiga michapo.. tumbo tu mbele.. tamaa ya kupenda kutawaliwa na mabeberu.
Magufuli 2020π―
..MusikilizaSijayasikia nilipomusikiliza haya madai yako.. tafuta lingine..
Hivi mnaamini nchi itajengwa na rais Tundu na makamu wake Salumu? Mawaziri ndokina Lema, sugu, esta, haule, nabii shilla. .. Hahahahaaaa haya pambaneniMaendeleo gani hayo mbona sisi hatuyaoni mnatumia darubini gani kuyazoom hayo maendeleo?
Magu atupishe tuijenje nchi kwa umoja na amani
Masikini huelewi lolote,unahitaji kufahamishwa taratibu.Kwani chato ipo Kenya?