Pre GE2025 Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru

Pre GE2025 Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kuendelea kufanya uchaguzi ambao hauna maana yoyote ni ujing na kuootezeana muda, tunakubaliana bora Samia aendelee kutawala atakavyo kuliko kutumia hela za umma na tutuchosha bure wananchi kufanya uchaguzi usio na maana yoyote ile.

Lissu yupo sahihi, aungwe mkono na wote wenye akili timamu.
Chadema kama haitashiriki.ni shauri yao vyama vingine vyote vya upinzani vitashiriki
 
Huyu mbwatukaji wa hovyo sana, anafikiri baada ya hiyo miaka 2 rais atakuwa yeye? Samia yupooo!

Wewe unawaza urais tu kwa sababu ndiye mungu wako .

Biblia iko sahihi sana unaposema rushwa hupofusha macho .
Yaani ukiangalia kwenye mitandao utaona mpaka baadhi ya viongozi wa dini wamekua vipofu kwa sababu ya rushwa na hofu hata ya kutamka neno haki.

Leo viongozi wa baadhi ya dini wanaogopa kusema wazi kuwa bila haki amani ya nchi itayumba.

Watu hawaoni ubaya wa sheria kwa sababu wapo madarakani na familia zao zinanufaika.

Jifunzeni kitu kwa yule polisi anayefukuzwa kwenye nyumba za serikali wakati ametumikia kwa miaka zaidi ya 30 kwa kutii na uvumilivu hata pale alipodhulumiwa haki yake.
Yule polisi anatamani pangekuwa na watu wa kupigania haki yake mapema lakini hana watu.
Aliodhani ni wenzake hawana habari naye kwa sababu hao hao ndio waliokula pesa zilizopaswa kulipwa kwake .
Hana pa kukimbilia maana sheria za dhulma zinambana .Waliokula na kudhulumu malipo yake wapo salama zaidi kwa sababu wapo kwenye mfumo usiojali malalamiko ya watu . Pale amejitoa tu muhanga lakini maisha yake yako hatarini kwa sababu serikali iliyopo haitaki kuambiwa ukweli wala kulaumiwa zaidi ya kusifiwa kama Mungu.

Yule polisi atufungue macho tudai sheria za haki na katiba inayowajali watu wote ndani ya nchi hii.
Katiba iliyopo inapigania maslahi ya walioshiba na kuvimbiwa. Ndio maana wanaCCM wote wanaufyata wanapoona kakikundi kadogo kanakazimisha mtu asiye na maono yoyote kugombea urais bila kupingwa kwa sera na maono juu ya Taifa hili . Mtu asiye na maono hawazi namna ya kuwasimamia na kuwaelimisha watanzania namna ya kutumia rasilimali zao wenyewe. Anawaza tu kuuza kila kitu halafu watanzania wabaki kama manamba kwenye nchi yao.


Fuatilia uone kama ni sahihi Zoezi la kuhakiki wapiga kura liko sawa !!
Yaani nchi kwa sasa ina vijana zaidi ya mil. 30 halafu zoezi hilo linafanyika kwa siku zisizozidi kumi . Yote ni kwa sababu ya kutumia watumishi wa halmashauri .Yaani kusambaza tu vifaa vya kujiandikishia na kuhakiki ni zaidi ya wiki mbili lakini zoezi la kuandikishwa ni siku kama tisa au nane tu. Sasa hapo kitakachofanyika ni kutengeneza majina feki ili kuwafurahisha waliowatuma.
Ujinga huo waliufanya kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa .
Wanaandika majina feki na kutoa takwimu za uongo .

Hivi tangu 2015 mpaka leo wamekufa watu wangapi na wameongezeka wangapi ?
Watajuaje kuwa wengine ni marehemu wasiporudia na kuhakiki kwa watu wote na iwe ni zoezi la lazima na lifanyike bila kujali mtu atampigia wapi kura ili kwanza watolewe marehemu na kuandikisha wapya .

Kila kitu kinachofanywa na wanasiasa na wateule wa Rais kipo kimaslahi binafsi na sio taifa.

Hivi kama inawatumia wafanyakazi wa umma wanaolipwa na serikali kama walimu na polisi na watumishi wengine kwa nini wasifanye kazi hiyo kama Sehemu ya majukumu yao kwa mwajiri .
Walipwe wale tu wanaotoka nje ya ajira kama Migambo basi.

Tunpoteza pesa nyingi kulipa watumishi ambao ni kazi yao kwa mwajiri .
Basi ni bora tume itangaze nafasi za kuomamia uchaguzi kwa Wasio na ajira ili walipwe na wafanye kazi chini ya tume na sio mkurugenzi.


Zoezi la uhakiki wa Daftari la'mpiga kura liendelee mpaka mwezi wa nne miezi miwili ili watu wote wajiandikishe na marehemu waondolewe kwenye daftari la wapiga kura .

Nchi gani inapata viongozi waliochaguliwa na wafu .

CCM wanapenda madaraka sasa watanzania wengi wanataka rais na bunge lake waongezewe muda mpaka tume na katiba ifanyiwe marekebisho lakini pia daftari la mpiga kura lifanyiwe maboresho na majina yabandikwe mapema kila mtu aone orodha ya watu hai sio marehemu .

Nchi hii sio mali ya Samia wala CCM wala polisi bali ni ya watu wote mil.64. Sasa kama karibu nusu ya watanzania hawakubaliani na mfumo wa kupata wawakilishi basi ni bora ufanyiwe kazi kuepusha Shari . Watu karibu mil 40 hawataki mfumo wa uchaguzi hasa vijana .CCM mnataka mtumie majeshi kuwaua wote kwa sababu ya Kumfurahisha Mzanzibari mmoja na mkwe wake . ? Hapana hayo marekebisho hayana ubaya wowote kwa polisi wala jeshi zaidi ya hofu ya mafisadi wachache wanaoogopa kunyimwa kura.
 
Lisu mjanja fulani huvi anachowinda gapi ni ruzuku iendelee kwa miaka miwili cha
CHADEMA ipate pesa za ruzuku

Kifupi Chadema haijajiandaa kwa uchaguzi na yeyebhajajiandaa.Chama hakina pesa kaligundua hilo baada ya mwenyekiti

Kila akipiga hesabu za pesa za uchaguzi mkuu anaona hazienei na muda wa kupokea ruzuku imebaki miezi minne tu bunge livunjwe na ruzuku isimame
 
Hivi CCM hampendi Uchaguzi wa haki na wazi,wenye kusimamiwa na chombo huru pasipo kuua wale kuteka wananchi??...kumbukeni huwa mnaenda ibadani kila siku wengine Makka na Israel kuhiji

Wale wa Maka wanaamini kwamba unatakiwa ufanye madhambi makubwa alimradi upate pesa za kuhiji na kupeleka watu hija.
Ukifika Maka kwenye vivutio vya utalii wa mambo ya kule basi utasamehewa mdhambi yako yote na kuwa kama mtoto mdogo.

Ndio maana mtu mwenye historia ovu kama chengera naye alikwenda kuhiji Maka kwenye kaburi la Mtume aliyesimisha Hukumu ya Haki kwa umma wake , tena chenhera alikua na furaha kabisa baada ya kufanikisha uchafuzi ulioacha vilio huzuni na misiba kwenye nchi .
Hata CCM wakikataa kabisa upinzani usitawale lakini kwa maovu wanayofanya basi Mungu atamuinua mtu ndani yao na atawanyoosha kidikteta bila kufuata sheria na ndipo watakua na vilio na kusaga meno .



Hiyo pepo atakayokwenda huyo mtu kwa imani hiyo ukijikuta upo naye siku ya mwisho basi ujue uko jehanam . Kama utaweza kukimbia basi kimbia mbio za marathoni.
 
..hizo ndizo gharama ambazo CCM imetuingiza kwa kuchelewa kufanya mabadiliko ya maana ktk sheria zetu za uchaguzi.

..nadhani kukiwa na nia njema kuanzia sasa hivi tunaweza kutumia muda mfupi kufanya mabadiliko kuliko huo anaopendekeza Tundu Lissu.
Kwa mawazo yangu wazo la kusogeza mbele uchaguzi ni baya kwa sababu:
1. Linatoa loop hole ya kubadilisha term ya urais.
2. Hamna guarantee ya mabadiliko yeyote maana inategemea mno nia njema ya waliopo sasa madarakani.
3. Rais aliyepo hatakubali kuwa Rais wa kwanza wa CCM aliyedumu kwa muhula mmoja. Hilo CDM wasahau.

Badala yake CDM iweke nguvu katika kuhakikisha vyama vya upinzani makini vinapata wabunge na madiwani wengi. Muda uliobaki utumike katika kupata wagombea wanaokubalika na kujenga ushirikiano na vyama vingine. Wakiweza kupata wabunge makini watakuwa katika nafasi ya kusukuma jambo hili nje na nfani ya Bunge.

CDM itumie vilevile kupata resources za kujiendesha na kuwahamasisha wananchi.

Aidha, mwaka 2030 patakuwa na mabadiliko ya uongozi CCM na hivyo kukifanya kuwa vulnerable kuliko sasa kwa sababu patakuwa na mnyukano wa wanaoyaka kugombea urais.

Aidha, Rais wa sasa atataka kuacha legacy ya kuacha nchi yenye Katiba bora inayowapa watanzania uhuru wa dhati wa kuchagua viongozi wanaowataka ambao watawajibika kwao. Tukumbuke kuwa Samia alihusika sana katika juhudi zilizopita za kupata Katiba Mpya. Naamini angependa kumalizia kazi aliyoanza.

Mwisho, miaka mitano utaipa CDM muda wa kutosha wa kutibu majeraha ya uchaguzi wa Mwenyekiti wake na hivyo kuunganisha wanachama na wafuasi wake. Watakuwa wanajidanganya kama wataamini hayapo.

Amandla...
 
Huyu mbwatukaji wa hovyo sana, anafikiri baada ya hiyo miaka 2 rais atakuwa yeye? Samia yupooo!
Sidhani kama upo sahihi je wewe unalizika na tume hii ya uchaguzi,, jinsi inavyo fanya kazi kama unalizika basi huitakii mema nchi yako.Hakuna mtu yoyote ambaye Anauhakika wakushinda kukiwa na Mabadiko ila, watu wataridhika na kufurahia uchaguzi huru na haki kwa sasa wewe hata kama ukubaliki hata huko CCM, Wakiamua upite unapita. Hiyo siyo haki. Asilimia kubwa sana ya Watanzania ni jamaa na marafiki wa watu walio CCM na wanaipenda CCM kwa kuwa na mifumo inayo eleweka shida inakuja kwenye kupeana madaraka.
 
Kwa mawazo yangu wazo la kusogeza mbele uchaguzi ni baya kwa sababu:
1. Linatoa loop hole ya kubadilisha term ya urais.
2. Hamna guarantee ya mabadiliko yeyote maana inategemea mno nia njema ya waliopo sasa madarakani.
3. Rais aliyepo hatakubali kuwa Rais wa kwanza wa CCM aliyedumu kwa muhula mmoja. Hilo CDM wasahau.

Badala yake CDM iweke nguvu katika kuhakikisha vyama vya upinzani makini vinapata wabunge na madiwani wengi. Muda uliobaki utumike katika kupata wagombea wanaokubalika na kujenga ushirikiano na vyama vingine. Wakiweza kupata wabunge makini watakuwa katika nafasi ya kusukuma jambo hili nje na nfani ya Bunge.

CDM itumie vilevile kupata resources za kujiendesha na kuwahamasisha wananchi.

Aidha, mwaka 2030 patakuwa na mabadiliko ya uongozi CCM na hivyo kukifanya kuwa vulnerable kuliko sasa kwa sababu patakuwa na mnyukano wa wanaoyaka kugombea urais.

Aidha, Rais wa sasa atataka kuacha legacy ya kuacha nchi yenye Katiba bora inayowapa watanzania uhuru wa dhati wa kuchagua viongozi wanaowataka ambao watawajibika kwao. Tukumbuke kuwa Samia alihusika sana katika juhudi zilizopita za kupata Katiba Mpya. Naamini angependa kumalizia kazi aliyoanza.

Mwisho, miaka mitano utaipa CDM muda wa kutosha wa kutibu majeraha ya uchaguzi wa Mwenyekiti wake na hivyo kuunganisha wanachama na wafuasi wake. Watakuwa wanajidanganya kama wataamini hayapo.

Amandla...
Hivi kiongozi umewahi kusimamia uchaguzi?, kwa sheria hizi za uchaguzi zilizopo ziweze kuwapa wapinzani wabunge wengi?, Kwa taarifa yako Samia hana tofauti na Magufuli kwenye uchaguzi.Nimesimamia serikali za mitaa nimeona wakurugenzi ambao ndoo wasimamizi wa uchaguzi jimboni wanavyokuja na mikakati iliyopangwa kutoka huko juu.Anakwsmbia kwenye kituo chako unatakiwa kufanya lolote ili mgombea wao apate asilimia zaidi ya 90.Kila dk katibu kata ,tarafa,viongozi wa chama wanakutembelea kukukumbusha suala hilo.Mgambo na polisi wote wameishaelekezwa cha kufanya mnashirikiana vyema kuhakikisha mambo yanaenda vyema.Sasa ndoo nakuuliza hao wabunge wengi unaowasema wanapatikanaje kwa staili hiyo?
 
Hivi kiongozi umewahi kusimamia uchaguzi?, kwa sheria hizi za uchaguzi zilizopo ziweze kuwapa wapinzani wabunge wengi?, Kwa taarifa yako Samia hana tofauti na Magufuli kwenye uchaguzi.Nimesimamia serikali za mitaa nimeona wakurugenzi ambao ndoo wasimamizi wa uchaguzi jimboni wanavyokuja na mikakati iliyopangwa kutoka huko juu.Anakwsmbia kwenye kituo chako unatakiwa kufanya lolote ili mgombea wao apate asilimia zaidi ya 90.Kila dk katibu kata ,tarafa,viongozi wa chama wanakutembelea kukukumbusha suala hilo.Mgambo na polisi wote wameishaelekezwa cha kufanya mnashirikiana vyema kuhakikisha mambo yanaenda vyema.Sasa ndoo nakuuliza hao wabunge wengi unaowasema wanapatikanaje kwa staili hiyo?
Nimesimamia serikali za mitaa nimeona wakurugenzi ambao ndoo wasimamizi wa uchaguzi jimboni wanavyokuja na mikakati iliyopangwa kutoka huko juu.Anakwsmbia kwenye kituo chako unatakiwa kufanya lolote ili mgombea wao apate asilimia zaidi ya 90.Kila dk katibu kata ,tarafa,viongozi wa chama wanakutembelea kukukumbusha suala hilo.Mgambo na polisi wote wameishaelekezwa cha kufanya
 
Nadhani bado hamjaelewa dhana na mantiki ya No reform no election. Pia hamjaelewa mbinu na mikakati ya CHADEMA kwenye hili.

Iko hivi, kwa hali ilivyo sasa ni vigumu kwa CHADEMA kupata viti vya ubunge na udiwani kwenye uchaguzi. CCM itaendesha uchaguzi fake halafu itaamua kuwagawia CHADEMA na vyama vingine viti kadhaa. Inaweza kugawa viti vi 5 kwa chadema, 3 kwa ACT na 1 kwa vyama vingine ili ijidai kuwa uchaguzi umefanyika. Sasa kuna haja gani kushiriki kwenye uchaguzi wa namna hii?

1. Mbinu ya kwanza ni kushinikiza mabadiliko. Hoja ya CCM hapa ni kwamba muda hautoshi kufanya mabadiliko. Ingawa siyo kweli lakini hoja hii ina mantiki fulani. So ndo maana Lisu anasema bora kusogeza mbele uchaguzi ili mabadiliko yafanyike. Hapa anajaribu kutoa proposal kujibu hoja ya CCM ya muda hautoshi ili kukaribisha mazungumzo ya kujadili muda kiasi gani uongezwe. Kama CCM wataingia kwenye mazungumzo basi watakubaliana na wadau wote wa siasa muda wa kuongeza.

2. CCM wanaweza kukataa hili la kuongeza muda wakaamua kwenda kwenye uchaguzi. CHADEMA wanaweza kutumia mbinu mbalimbali kuzuia lakini ni kweli hawatafanikiwa. Fujo zitakuwa nyingi, watu watakufa, watu watakamatwa na kufungwa n.k. hapa ndo jumuiya ya kimataifa itaingia na watu wanaweza kupelekwa ICC baada ya huo Uchaguzi fake. Serikali itakayo kuwa madarakani itakuwa haina uhalali wa kisiasa na italazimika kufanya mabadiliko makubwa kwa ajili ya uchaguzi wa 2030.

Hivyo basi. Mkae mkijua lengo kubwa la No reforms no election si matokeo ya haraka haraka. Ni kwa ajili ya 2030.

3. Samia anajua kwenye uchaguzi huru hatoboi. Na hayuko tayari kuachia kiti. Bado anautamani urais. Na CHADEMA wanalijua hili. So ana machaguo mawili. La kwanza anatafute njia ya kubaki madarakani kwa kufuata ushauri wa kuongeza muda ili afanye marekebisho na kuamua kwamba baada ya muda huo hatagombea tena. Hapa atakuwa amejiongezea kipindi cha mteremko cha angalau miaka 2 akiwa Rais. Chaguo la 2 kuingia kwenye uchaguzi fake kwa nguvu na kuwa tayari kuongoza kipindi cha 2025 - 2030 kwa nguvu ya dola, na kuwa tayari kukabiliwa na jumuiya ya kimataifa ikiwa ni pamoja na kupelekwa ICC na kushurutishwa kufanya mabadiliko. Chaguo ni lake.
 
Nadhani bado hamjaelewa dhana na mantiki ya No reform no election. Pia hamjaelewa mbinu na mikakati ya CHADEMA kwenye hili.

Iko hivi, kwa hali ilivyo sasa ni vigumu kwa CHADEMA kupata viti vya ubunge na udiwani kwenye uchaguzi. CCM itaendesha uchaguzi fake halafu itaamua kuwagawia CHADEMA na vyama vingine viti kadhaa. Inaweza kugawa viti vi 5 kwa chadema, 3 kwa ACT na 1 kwa vyama vingine ili ijidai kuwa uchaguzi umefanyika. Sasa kuna haja gani kushiriki kwenye uchaguzi wa namna hii?

1. Mbinu ya kwanza ni kushinikiza mabadiliko. Hoja ya CCM hapa ni kwamba muda hautoshi kufanya mabadiliko. Ingawa siyo kweli lakini hoja hii ina mantiki fulani. So ndo maana Lisu anasema bora kusogeza mbele uchaguzi ili mabadiliko yafanyike. Hapa anajaribu kutoa proposal kujibu hoja ya CCM ya muda hautoshi ili kukaribisha mazungumzo ya kujadili muda kiasi gani uongezwe. Kama CCM wataingia kwenye mazungumzo basi watakubaliana na wadau wote wa siasa muda wa kuongeza.

2. CCM wanaweza kukataa hili la kuongeza muda wakaamua kwenda kwenye uchaguzi. CHADEMA wanaweza kutumia mbinu mbalimbali kuzuia lakini ni kweli hawatafanikiwa. Fujo zitakuwa nyingi, watu watakufa, watu watakamatwa na kufungwa n.k. hapa ndo jumuiya ya kimataifa itaingia na watu wanaweza kupelekwa ICC baada ya huo Uchaguzi fake. Serikali itakayo kuwa madarakani itakuwa haina uhalali wa kisiasa na italazimika kufanya mabadiliko makubwa kwa ajili ya uchaguzi wa 2030.

Hivyo basi. Mkae mkijua lengo kubwa la No reforms no election si matokeo ya haraka haraka. Ni kwa ajili ya 2030.

3. Samia anajua kwenye uchaguzi huru hatoboi. Na hayuko tayari kuachia kiti. Bado anautamani urais. Na CHADEMA wanalijua hili. So ana machaguo mawili. La kwanza anatafute njia ya kubaki madarakani kwa kufuata ushauri wa kuongeza muda ili afanye marekebisho na kuamua kwamba baada ya muda huo hatagombea tena. Hapa atakuwa amejiongezea kipindi cha mteremko cha angalau miaka 2 akiwa Rais. Chaguo la 2 kuingia kwenye uchaguzi fake kwa nguvu na kuwa tayari kuongoza kipindi cha 2025 - 2030 kwa nguvu ya dola, na kuwa tayari kukabiliwa na jumuiya ya kimataifa ikiwa ni pamoja na kupelekwa ICC na kushurutishwa kufanya mabadiliko. Chaguo ni lake.
Jumuiya ya kimataifa? Haya, ngoja tuone.
 
Mtanzania wa kweli? Familia yake ni raia wa USA, yeye anaishi Ubeleji, utamwitaje Mtanzania wa kweli? Wewe na mimi wenye familia na ndugu zetu hapa tutaitwaje sasa?
Una hata kovu la risasi?
 
Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru.
View attachment 3237446
Waati akihutubia Maelfu ya Watu huko Mkoani Singida hii leo, amesema Uchaguzi uahirishwe.

Amesema kuliko kufanya Uchaguzi katika mazingira haya ya sasa, Bora tarehe ya Uchaguzi isogezwe mbele kwani tarehe zimepangwa na binadamu.

Amedai kwamba CCM wanadai muda hautoshi wa kupitia katiba na sheria, kanuni za tume huru ya Uchaguzi. Kakubaliana na hali hiyo, ila akapendekeza kwasababu hiyo, bora tarehe isigogezwe mbele lakini sheria ifanyiwe marekebisho.

Tundu Lissu kadai bila mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi hakutakuwa na Uchaguzi
Pia Kohoji kwanini Mawakala wanaosimamia Uchaguzi wanaapa kwa Mkurugenzi kuficha siri, ni siri gani hiyo wanaoyoficha? Ya wizi wa kura?

Kasema hataki tena mambo ya kuapa kwa Mkurugenzi, Mambo ya Polisi kuingia vituo vya kupigia kura kwanini ndo wanaingiza kura feki
View attachment 3237163View attachment 3237164View attachment 3237165

Naona bado kuna tatizo kubwa sana kuhusiana na suala hili la Chaguzi za Kisiasa hapa nchini Tanzania na muktadha mzima wa Sheria za nchi kuhusu suala hili.
Nimekuwa nikitoa Maoni yangu na Ushauri wangu mwingi sana humu mtandaoni kuhusiana na suala hili, lakini kwa bahati mbaya sana Watu wengine wamekuwa wakipuuzia. Ukweli mchungu Sana ni kwamba Wanasiasa wengi sana bado hawajafahamu ni nini hasa wao wanachokipigania kwenye hizo harakati za Siasa wanazofanya.
 
Itakuwa na faida gani kama wao hawatakuwa sehemu ya watunga sheria?
Mimi sidhani wala sitarajii kwacserikali hii na viongozi hawa wanaweza kutuletea katiba boravkatika mazingira haya ambayocwako tayari hata kuuwa watu ili wabaki madarakani. Tusitajie kwa shinikizo bila shinikizo kuwa eti CCM itakuwa tayari kuruhusu apatika ne Raisi mwingine nje ya CCM hiyo haiwezi kutokea abadani katika mazingira ya kawaida, Tundulisu na kelele zake atapita kama walivyo pita wengine. CCM haisikii wala haielewi. Mpaka atokee mwehu mmoja.
 
Tundu Lissu: Tubadilishe tarehe ya Uchaguzi Mkuu kwa Miaka miwili ili tuwe na tume Huru.
View attachment 3237446
Waati akihutubia Maelfu ya Watu huko Mkoani Singida hii leo, amesema Uchaguzi uahirishwe.

Amesema kuliko kufanya Uchaguzi katika mazingira haya ya sasa, Bora tarehe ya Uchaguzi isogezwe mbele kwani tarehe zimepangwa na binadamu.

Amedai kwamba CCM wanadai muda hautoshi wa kupitia katiba na sheria, kanuni za tume huru ya Uchaguzi. Kakubaliana na hali hiyo, ila akapendekeza kwasababu hiyo, bora tarehe isigogezwe mbele lakini sheria ifanyiwe marekebisho.

Tundu Lissu kadai bila mabadiliko ya Sheria ya Uchaguzi hakutakuwa na Uchaguzi
Pia Kohoji kwanini Mawakala wanaosimamia Uchaguzi wanaapa kwa Mkurugenzi kuficha siri, ni siri gani hiyo wanaoyoficha? Ya wizi wa kura?

Kasema hataki tena mambo ya kuapa kwa Mkurugenzi, Mambo ya Polisi kuingia vituo vya kupigia kura kwanini ndo wanaingiza kura feki
View attachment 3237163View attachment 3237164View attachment 3237165
Chuma kinatema cheche. Yuko sahihi.
 
Back
Top Bottom