Tundu Lissu, uhai wako ni muhimu kuliko chochote, usije Tanzania kwa sasa, ngoja kwanza

Chief spy unaemtaja anahusikaje na jaribio la kifo cha Lissu ilhali uteuzi wake ulianza 2019 na ameondoka 2023
Ilhali Lissu alikutana na dhahma ya risasi 2017

Ukiwa muongo muongo jitahidi uwe na kumbukumbu
Soma vizuri bandiko langu acha kukurupuka.
 
Mungu asipoilinda nyumba, wailindao wafanya KAZI Bure,

Rais haezi mlinda Lissu,

Mungu ndo amlinda Lissu na alimuokoa na MAUTI,

Kuna wakati Huwa nawaza risasi zile zimeleta athari Fulani ktk UBONGO wa Lissu.
Hayo ya Mungu unasema wewe, yeye Lissu anataka kulindwa au kuhakikishiwa usalama wake na Rais.
 
Sasa huyo Magufuli yupo?
 
Kuna mengi yameshajadiliwa, kukubaliana na kufanyika nyuma ya pazia.. Hivyo nadhani hakuna shida sana
 
Sasa huyo magufuli bafobyupo
 
ASANTE FOR YOUR DEEP THINKING AND ANALYSISI OF ISSUES!
 
Kuna watu wamekuuliza hapo, huyo lisu 2020 aliporudi kugombea urais akazunguka nchi nzima nani alimgusa.

Magu anaemsingizia kwamba ndio alikuwa mtesiwake Sasa hayupo for 2years.

Mambo mengine nikutafuta kiki za kijinga tu.
Magufuli hakuwa mjinga, alijua kuwa dunia nzima inamtazama yeye wkati wa kampeni na uchaguzi. Alisubiri attention ya dunia iondoke baada ya uchaguzi, then aendelee na hujuma dhidi yake.

Usiwe mtu asiyeweza analyse issues, simple issues. Baada ya uchaguzi kwanini walitaka kumkamata akaokolewa na European na USA embasies? Alikuwa na kosa gani? what was the motive behind the intended arrest?

To crown it all, kwanini walimpiga risasi? wakaondoa CCTV, walinzi etc etc. Huna akili kiasi hicho kuweza kuona kuwa huyu mtu yuko hatarini...
 
Tundu Lissu hana hakika ni nani adui yake, Lissu hana hakika nani alimpiga risasi wala kundi gani liliandaa lile tukio!
But with the trend of what happened before and after his shooting, one can irresistibly point to the involvement of the government of Magufuli!
 
Kaka umeongea kitu kizito sana! πŸ€”πŸ€”πŸ€”

Mwenye kuelewa ataelewa.....
Nani kakwambia wapo?! Ni nani kakwambia ukishindwa mission ile utabaki hai?!😊 Hizi habari mnapata wapi?!
 
Yupo Mungu atamlinda na kumwepusha na mabaya yote. Aliyemwokoa ktk gharika lile ndiye huyu atamlinda hata sasa adui zake atawachanganya.
Maandiko yanasema usimjaribu Bwana Mungu wako. Ndiyo maana ukishasali usiku huwa unafunga mlango na sio kuacha wazi eti Umeshamkabidhi Mungu jukumu la kukulinda kupitia sala.
 
Mashetani kwa sasa wanahaha pa kujificha baada ya baba yao kujifia, Je unawasikia? Yule mzee wa Kipeperushi cha Tanzanite unamsikia tena?

Ukiwa mtu makini, haya maisha ya Duniani ni ya kuheshimu sana.
 

Alipuuzwa wakati aliondoka kwa kukimbia. Au unadhani hatukuona kilichokuwa kinaendelea?
 
Shetani nyonya damu keshalala ndani ya futi 12 aje tu kuna amani sasa.
 
Tundu Lissu hana hakika ni nani adui yake, Lissu hana hakika nani alimpiga risasi wala kundi gani liliandaa lile tukio!

Aaa wapi, Lisu alikuwa anamtaja Magufuli waziwazi kuhusu shambulio lake, na mazingira ya shambulio lake aliyeweka wazi. Hivi mnatuona ni watoto hatujui ukweli ni upi? Tena isitoshe wakati ule CDM walipendekeza kuletwe shirika binafsi la nje kufanya uchunguzi wa tukio lile, maana Taasisi za ndani zilishachagua upande kwenye shambulio lake, kwa kutaka ama kwa kulazimishwa.
 
Mimi nachokiona hapa ni uspesho kwa Lissu kwamba Lissu ni mtu hatari sana kuliko wanasiasa wenzie wote ndio maana yeye bado anawindwa hadi leo na anahitaji kupewa ulinzi na Rais kuhakikushiwa hato sumbuliwa wala kudhuriwa kwa aina yeyote.

Huo ndio ukweli hata kama unataka kuongea kwa njia ya kubeza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…