Tundu Lissu, vita na Wasafi hutoiweza, utagalagazwa wewe na chama chako

Diamond alibariki utesaji na dhuluma mpaka aliimba wimbo kubariki eti baba lao.
Uzalendo kwa afrika tulifundishwa na baba wa taifa .afrika ni moja
 
Watanzania wangekuwa wanawaelewa hao Roma na Nay basi sasa hivi ndio wangekuwa wanapigiwa kura ila hali ipo tofauti.
Kwani kuna kura zinapigwa nchi hii,zaidi ya maigizo?.
 
Kwani kuna kura zinapigwa nchi hii,zaidi ya maigizo?.
Nimekusudia kwamba Huyo Roma ndio angekuwa anagombea hizo Tuzo badala ya Diamond, kuhusu hayo maigizo ya kura ni kwamba watu wanayapenda na ndio maana kila mwaka wa uchaguzi huwa mnaenda kushiriki hayo maigizo.
 
Diamond alibariki utesaji na dhuluma mpaka aliimba wimbo kubariki eti baba lao.
Uzalendo kwa afrika tulifundishwa na baba wa taifa .afrika ni moja
Ungekuwa unaheshimu mawazo ya wengine hata usingesumbuka na hilo, msitake kulazimisha hisia mlizonazo ndio awe nazo kila mtu. Wasanii wao wameenda pale kwa ajiri ya burudani hayo mengine ya kwenu acheni ushamba.
 
Yaani Wasafi ndio wamgalagaze Lissu?

Hivi umesahau Mwendazake na serikali yake nzima,CCM,Jeshi la Polisi, pamoja na wasiojulikana walitumia nguvu zao zote Kuhakikisha Lissu anapotea?

Matokeo yake, Jiwe ndio Limepotea limemuacha Lissu anaishi huku wasiojulikana wakipoteana,Leo hao Wasafi wana nguvu ipi wakati ni haohao walikuwa washirika wa Jiwe.

Halafu naona watu wanalaumu kwamba wanampangia Diamond awe chama gani,hapa suala ni kwamba hata kama Diamond yupo CCM alipaswa awe na msimamo wa kutetea Yale aliyoyaona ya uonevu na sio kukaa kimya halafu ukiwa na jambo lako utake watu wote wakutetee hata wale uliowapa mgongo,haiwezekani
 
Vitu vyengine ni vya kitoto, huyu Mama samia mnaemshabikia yeye alifanya nini kipindi ni Makamu wa rais katika kukemea uovu? Et mnataka kila msanii awe na mawazo na hisia sawa kama Roma au Nay huo ni ushamba heshimuni maamuzi ya watu, kama Lissu katiwa ulemavu na Magufuli asijaribu kutaka iwe kwamba hasira zake ndio awe nazo kila mtu dhidi ya mbaya wake. Dunia ilivyo inawezekana Dr. Ulimboka akawa anamchukia JK na kumuona ni shetani kuliko anavyomchukulia JPM, sasa tusilazimishane tuwe sawa.
 
Ushamba ni kumshabikia muuaji na mtesaji kwa maslahi yako ya muda mfupi!
Kuna masilahi ya muda mrefu hapa duniani? ushamba ni huo kutaka mitazamo yako na hisia zako wawenazo na wengine hali ya kuwa watu tunatofautiana. Wewe hata kama unaona mtu fulani ni katili au aliwahi kukukatili hiyo sio sababu ya kutaka na wengine woooote wamuone huyo mtu kama umuonavyo wewe dunia haiendi hivyo hata siku moja.
 
Yani mtu anashindana na CCM wenye serikali awaogope WASAFI wenye hawana kitu[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]???
 
Wasafi ni jeshi kubwa ! unataka kumtisha nani ? Jeshi kubwa limeshindwa kummaliza Harmonize !

Ni hivi , Kila mtu ashinde mechi zake , Utaratibu ni ule ule Kale ulikopeleka Mboga .
Harmonize nae si CCM na amejichora kabisa tattoo ya Magufuli mkononi
 
Wapumbavu kama wewe ni hasara kubwa sana kwa Tanzania. Kajisemea CAG Assad you’re suffering from Acquired Stupidity disease.
 
Hauwezi kumuelewa LISSU, kwakuwa akili yako imemjaa DIAMOND na wasafi

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
 
kwani wapi ume/mmelazimishwa?
 
Reactions: BAK
Sadala hamuungi mkono Lissu na Lissu naye hamuungi mkono Sadala sasa shida iko wapi? Kwa nini hamtaki Lissu kuelezea hisia zake?
 
Sasa hizi hasira zako kwanini usielekeze kutafuta hela ili kuokoa ukoo wako unaoliwa na umasikini kuliko kutukana hovyo hapa?

Sasa diamond kuwa ccm ni kosa?

Mbona duniani huko wasanii wanawapigia kampeni watu wanaowataka je uliwahi kuona mtu aina ya Lisu wanasimama na kuinesha chuki zao kwao?

Lisu ni mbumbumbu wa siasa!
 
Mtoa mada akili yako mbovu sana.... Lissu kusema hamuungi mkono msanii ndio inakuwa kutangaza vita? Uhuru wa maoni uko wapi? Ingekuwa na hifadhi ya Serengeti ndio inatafutiwa tuzo ningeelewa, lakini msanii hawezi kugeuka a national concern.
Ningekubaliana na Lissu kama sababu za kutomuunga mkono Diamond zingekuwa ni performance ya kimuziki.Lakini kusema mtu yeyote ambaye yuko tofauti na CHADEMA sio mpenda haki huko ni kupotoka.
 
umesahau kunitaja!
kwa mazingira ya wakati ule hiyo inawezekana ikawa sawa lakini hawa watu hasa sio wa kuwaamini kila kitu kuna muda wanarudi wanajipendekeza ili yao yaende.
wapo watu wanafanikiwa lakini wengi ni kujipendekeza ndio kutokea kwao hao uliowataja hapo juu walibeba kwa uaminifu maslahi ya umma kwa maneno mengine walikubali kupoteza nafsi zao kwa ajili ya wengi lakini kwa sasa thubutuu! na si kwa sasa watu wanaangalia matumbo yao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…