Uchaguzi 2020 Tundu punguza kunadi sera ya mishahara kwa wafanyakazi mbele ya watu masikini

Uchaguzi 2020 Tundu punguza kunadi sera ya mishahara kwa wafanyakazi mbele ya watu masikini

Sawa lakini ni wajibu wa mgombea kueleza atafanya nini ili hao wasio na kazi wasiendelee kuwa tegemezi,afu nimezungumzia mtizamo wa jamii kubwa kwa waajiriwa vs wasioajiriwa na serikali
Hivi elimu zenu ikoje nyie nyenyere? Yaani hujawahi kabisa kumsikia akisema namna atakavyopanua wigo wa ajira? Basi kichwani kwako kuna shida! Tafuta hotuba ya jana akiwa Musoma usikilize mwanzo mwisho utaelewa!
 
Hivi elimu zenu ikoje nyie nyenyere? Yaani hujawahi kabisa kumsikia akisema namna atakavyopanua wigo wa ajira? Basi kichwani kwako kuna shida! Tafuta hotuba ya jana akiwa Musoma usikilize mwanzo mwisho utaelewa!
Ni ushauri tu Ila mnadhani Yuko sawa aendelee kunadi hili kila mkutano mtapata majibu,mgombea hajui kundi gani kubwa la kujielekeza,huwajui watz wewe wanavyowachukulia wafanyakazi au laa hujawahi ona japo kazi la salary ya 170,000 inavyogombaniwa.Endelea kutukana mkuu
 
Huu ushauri una mantiki kiasi fulani. Ni muhimu kuangalia kura ziko wapi na katika hoja zipi.

Inawezekana kama baadhi walivyosema hapo juu, calculation zake ni kuwa akiwaongelea hao watumishi, watapambana kwa ndugu na jamaa zao kumtafutia kura zingine.

Ni vizuri pia kuwajua Watanzania na fikra na tabia zao. Kama mmoja alivyosema, wengi tuna tabia ya kufurahia habari mbaya za wengine, tena hata za jamaa zetu.

Kwa mfano, mimi binafsi namkubali sana Lissu ila suala la vyeti feki nina mtazamo tofauti. Kuna watu wengi walifoji kweli vyeti na kujipatia ajira. Mimi naona hao hawastahili huruma haijalishi ufanisi wake kazini au amedumu kwa muda gani. Hata hivyo kama kuna waliooonewa, hao inabidi waangaliwe upya.
 
Hongereni kwa kampeni.

Twende kwenye hoja moja kwa moja,binafsi Sina tatizo na watumishi kuongezwa mishahara hiyo ni haki yao lakini ni vyema hoja Kama hii ikachagua majukwaa ya kuizungumzia.

Wafanyakazi hususani wa serikali wa kada zozote ni moja ya kundi ambalo jamii kubwa inaliona kuwa na maisha mazuri au ya nafuu maana ukiacha huo mshahara Hawa Wana fursa za mikopo kwa dhamana ya kazi zao na vimapato vya hapa na pale,ambapo kwa upande wa Pili wa shilingi Kuna kundi kuubwa Sana la vijana hawana kazi,wakulima,wavuvi,machinga na makundi mengine ya jamii wasio na kipato maalumu.Ni rai yangu kwa kua kundi hili la pili ni kubwa Sana na ndio kundi muamzi wa uchaguzi ni vyema sera zako zingejielekeza zaidi kwa Hawa kuliko watumishi.

Sio sawa kuzungumzia mishahara kwa kamii ambayo inaona mtu kuajiriwa ni kulamba bingo regardless of how much one is paid.Jikite kwenye sera za kulainisha ugumu wa maisha na kurahisisha biashara za watu wa kawaida,binafsi hata kwa observation yangu watu wa kawaida Wana Hali mbaya za maisha kuliko kuzungumzia wafanyakazi ,watu wataona Bora huyu huyu aliopo,narudia kusema Chadema msaidieni mgombea wenu kunadi sera kwa lugha rahisi Kama wafanyavyo wagombea wengine wa Upinzani maana kwa sasa anapata muitikio mkubwa zaidi kadiri siku zinavyosogea, Ila sio Kama wanasisiemu huwa wanasoma risala.Nawatakia kampeni yenye mafanikio
Mkuu una uelewa mdogo sana. Nakupa mfano (wa kubuni tu lkn ili uelewe)
Watumishi ukiwapa mshahara kwa mwezi kima cha chini milioni mia moja (ndio sijakosea 100,000,000) unadhani nini kitatokea

Pesa hiyo itazunguka kwa kila mtu. Kila mtu mpaka mama muuza mihogo
Niko busy hapa nikikaa vizuri nitaendelea kukudadavulia....
 
Jamani hivi mnafuatilia hotuba zake lakini? Jana hujamsikia akiongelea sekta binafsi?
Ni Mara mia kurudia hata Mara Saba Mara sabini kwenye specific rally mambo yanayogusa common wananchi kuliko mishahara ya watumishi unless huwa hamuwasikilizi wagombea wengine hata Kama hawana ufuasi mkubwa lakini Wana deal na ishu za common wananchi kwa lugha rahisi Sana,narudia habari za mishahara zitawapiteza
 
Amekuwa akiongelea ile annual increaments zaidi na siyo kupanda kwa madaraja ambayo ndiyo hupandisha mishahara vizuri! Na Hili la annual increaments imekuwa weak point kwa serikali ya JPM hence Ni capital kwa tundu.smart politics
 
Huu ushauri una mantiki kiasi fulani. Ni muhimu kuangalia kura ziko wapi na katika hoja zipi.

Inawezekana kama baadhi walivyosema hapo juu, calculation zake ni kuwa akiwaongelea hao watumishi, watapambana kwa ndugu na jamaa zao kumtafutia kura zingine.

Ni vizuri pia kuwajua Watanzania na fikra na tabia zao. Kama mmoja alivyosema, wengi tuna tabia ya kufurahia habari mbaya za wengine, tena hata za jamaa zetu.

Kwa mfano, mimi binafsi namkubali sana Lissu ila suala la vyeti feki nina mtazamo tofauti. Kuna watu wengi walifoji kweli vyeti na kujipatia ajira. Mimi naona hao hawastahili huruma haijalishi ufanisi wake kazini au amedumu kwa muda gani. Hata hivyo kama kuna waliooonewa, hao inabidi waangaliwe upya.
Binafsi sikubaliani na waliofoji vyeti kuendelea kuwepo kazini Ila angalau wangepewa hata robo ya pensheni zao wakajikimu huko.
Wanaopinga hoja yangu waendelee Ila narudia tena unless hawawajui watz wanavyowachukulia wafanyakazi.
 
Amekuwa akiongelea ile annual increaments zaidi na siyo kupanda kwa madaraja ambayo ndiyo hupandisha mishahara vizuri! Na Hili la annual increaments imekuwa weak point kwa serikali ya JPM hence Ni capital kwa tundu.smart politics
Sawa endeleeni na hizo smart politics labda Tzn inawafanyakazi wengi Sana na ndio kundi lenye turufu ya kura,mtapata majibu oktoba
 
Mkuu una uelewa mdogo sana. Nakupa mfano (wa kubuni tu lkn ili uelewe)
Watumishi ukiwapa mshahara kwa mwezi kima cha chini milioni mia moja (ndio sijakosea 100,000,000) unadhani nini kitatokea

Pesa hiyo itazunguka kwa kila mtu. Kila mtu mpaka mama muuza mihogo
Niko busy hapa nikikaa vizuri nitaendelea kukudadavulia....
Wewe ndio huna uelewa wa muktadha ya hoja yangu na jinsi navyowaelewa wa Tzn.Kwa taarifa yako Mimi ni msomi wa uchumi huna Cha kunifundisha kwenye njia za expansionary fiscal policy Ila nazungumzia wananchi wengi mtizamo wao dhidi ya watumishi na namna ya ku win kura zao,nasisitiza Wana mtizamo hasi kwa watumishi kwa hiyo kuzungumzia mishahara kwa wasio watumishi ni kujipotezea kura kwa yule anayeitwa mtetezi wa wanyonge Kama hamtaki endeleeni kuzungumzia mishahara kwa common wananchi mkidhani Wana uelewa Kama nyie.
 
Nijuavyo watanzania huwa wanafurahia wanaposikia fulani katumbuliwa kwenye kazi yake. Watanzania wengi wanapenda ile hali Mbaya waliyonayo na wengine wawe nayo pia.
Uzi wako nimeuelewa kuna watu wananuna kusikia wafanyakazi watalamba mishahara minono.
Kweli iongelewe hoja ya mishahara Lakini sio kwa kurudia Sana kila siku na kila Mahala.
Mbona niye mnaludia ludia kila mahala kuwambia watu masikini kuwa tuminunua mindege mikubwa,fraiova na nk.
 
Tundu Lisu karudia mambo ya mishahara ya watumishi tena akiwa Bunda huku wananchi wakimshangaa,hii itazidi kuonesha kwamba yeye anaguswa na mambo ya watumishi tu na sio machinga au wakulima nk nk,natoa tafadhari msije sema hamkuambiwa.

Kuna dhambi gani akiongelea maslahi ya wafanyakazi? Kwa akili yako unadhani watumishi wa umma nao hawastahili kuishi maisha mazuri au kulipwa mishahara mizuri?

Una uhakika kwenye hizo kampeni zake hazungumzii masuala mengine yakiwemo ya hao wakulima na wamachinga? Ifikie wakati Watanzania wote wawe na haki ya kufaidi keki ya Taifa.

Unajisikije kuona Wafanyakazi wa nchi hii wanafanyishwa kazi kama punda na vitisho vingi vya kutosha tu kwa miaka yote hii mitano na huyu dikteta uchwara huku wakinyimwa haki zao za msingi kwa kigezo cha kununua ndege?

Lissu anakuja kutetea haki, eti unatoa angalizo! Kwa hiyo hao wamachinga na wakulima ndiyo wanaostahili zaidi kuongelewa na kupata haki kuliko makundi mengine? Au makundi yote kwenye jamii yanastahili kuongelewa na kupata haki sawa bila ya ubaguzi wowote?
 
Hata mfanyakazi akiongezwa mara mbili ya mshahara wake,hawezi kuwatosheleza hao wategemezi. Kila mtegemezi anahitaji mafanikio yake binafsi..
Wewe ambaye siyo tegemezi una mafanikio gani? Au unawasaidia vip hao tegemezi unao wapiga spana?
 
Unasahau kuwa mtumishi mmoja ana wategemezi wasiopungua 10 nyuma yake, ndio maana tatizo la vyeti feki limeleta mtikisiko mkubwa kwenye jamii hata kama waliobainika ni wachache compared to watumishi waliopo...

Unasahau wasio na kazi wengi tegemeo lao ni wale wenye ajira rasmi na zisizo rasmi. Hao graduate wengi ni tegemezi kwa wenye ajira, think twice, think big
Pia wafanyakazi ni wanunuzi nalipaji kwa wananchi. Ndio maana mama ntilie huenda kuuza karibu na sehemu ya kazi. Na kuku na mayai kule vijijinu huuzwa kwa wafanyakazi. Wafanyakazi hutoa vibarua... Husaidia, hutoa sadaka, hukopesha.

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Hata mfanyakazi akiongezwa mara mbili ya mshahara wake,hawezi kuwatosheleza hao wategemezi. Kila mtegemezi anahitaji mafanikio yake binafsi..
Sawa, lakini bado kutakuwa na unafuu kwa tegemezi kama tegemeo kipato kitaongezeka.
 
Wewe ndio huna uelewa wa muktadha ya hoja yangu na jinsi navyowaelewa wa Tzn.Kwa taarifa yako Mimi ni msomi wa uchumi huna Cha kunifundisha kwenye njia za expansionary fiscal policy Ila nazungumzia wananchi wengi mtizamo wao dhidi ya watumishi na namna ya ku win kura zao,nasisitiza Wana mtizamo hasi kwa watumishi kwa hiyo kuzungumzia mishahara kwa wasio watumishi ni kujipotezea kura kwa yule anayeitwa mtetezi wa wanyonge Kama hamtaki endeleeni kuzungumzia mishahara kwa common wananchi mkidhani Wana uelewa Kama nyie.
Dah 🤭 yaani zama hizi akitokea kima akiniambia yeye ni msomi ndio namuona bogus kweli aisee. Samahani lkn kama nitakuboa nimeona niwe muwazi katika hili.
Yaani ulivyosema tu wewe ni msomi umeni turn off, frankly speaking. Napata picha yaani nabishana na Mwigulu Nchemba, nabishana na profesor Lipumba nabishana na profesor yule majalalaaa. All these plus kima wote wajiitao wasomi useless kabisa kwa taifa letu hili linalo race to the bottom like nobody's business.
Kwa taarifa yako wasomi wako wengi siku hizi na wanatuharibia tu na kwa sauti ya chini Mimi mwenye naweza kuwa kwenye hilo group lakini naonesha humility tu.
Khaaaaaa yaani umentoa kwenye mada mpaka njaa inaniuma sasa.
 
Anachofanya TL ni kutetea haki za watu wote. Maumivu yakikuzidi kunywa simu
[/QU
Jamaa kweli atakunywa SIMU kwa hasira aliyo nayo. Anaitwanga twanga halafu anachanganya na maji hatimaye anakunywa ili awe na software ya Android mwilini mwake.
 
hv mgombea anapoenda mkutanoni huwa anapewa sifa na kazi wanazofanya wale waliohudhulia kwenye huo mkutano? Anapohutubia eneo fulani anakuwa amedhamilia ujumbe kwa jamii husika 2 au nchi nzima kupitia vyombo mbalimbali vya habari?,mbona magufuli anahubili kila siku masuala ya ndege kwa wananchi maskini?,.Hata ningekuwa mimi ningebeba hii kama agenda muhimu cz madhira waliyopata wafanyakazi miaka mitano ni makubwa sana ,naona spana za lissu zinapenya sana
 
Back
Top Bottom