Tunga Sentensi ikianza na maneno "Tafuta Hela"

Mbali na semi nyingi zinazotrend kuhusu kutafuta hela kama vile..
1. Tafuta hela V8 sio gari ya serikali
2. Tafuta hela kitanda hakikai kwenye kona[emoji23]
3. Tafuta hela wanawake hawakai mbali na simu [emoji23]
Na nyingine kibao..

Hu usemi wa tafuta hela ndugu sio wachache nimeamini. Sina kiasi hicho ila namshukuru Mungu angalau kidogo naweza hata kula mara 3 kwa siku. Sasa ndugu zangu sijui wananionaje aisee. Unapigwa mizinga mpaka unatamani kuzima simu. Kwa siku lazima upokee simu 2 mpaka 4 sijui mie mtoto wa fulani, mie fulani, siku ya mwisho anataka hela imsaidie jambo fulani duh... ndugu zangu mie sina hela kihivyo maisha ni magumu kama lilivyo jina langu.
Tafuta hela uache kusumbua ndugu.
 
Sipingi umuhimu wakua na hela ila ulioandika ni ushabiki na majigambo
Sijigambi ndugu yangu. Hata hivyo hutakiwi kujivunia umasikini. Watanzania wengi wanapenda kuona kiongozi ni masikini, Kiongozi anapoomba kura akionekana ana umasikini basi huyo ndio anafaa. Mwendazake alikuwa anapenda kutumia neno wanyonge na watu walikuwa wanapenda kuitwa hivyo mimi hapana aisee sio mnyonge.
 
Ndugu, jana tu kukuomba pesa kidogo ushakuja kunitangaza JF, aiseee 😅
 
sio ushabiki mkuuu ndo uhalisia, japo ni mchungu
Hatupendi kuambina ukweli. Kuna ndugu yangu yeye alikuwa na tabia ya kukutafuta siku akiwa na shida tu. Kuna siku nikamwambia basi hata siku ukiwa na raha tutafutane sio siku ya shida tu. Alipotea mazima toka 2012 sijawahi wasiliana nae tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…