Tungekuwa na Baraza la Mawaziri sharp na smart tungekuwa tunaipeleka SGR Uganda kwa focus ya kuifikisha Sudan Kusini na Afrika ya Kati

Tungekuwa na Baraza la Mawaziri sharp na smart tungekuwa tunaipeleka SGR Uganda kwa focus ya kuifikisha Sudan Kusini na Afrika ya Kati

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Dunia hailali. Kila siku watu wanaumiza vichwa vyao wafanyaje kukamata fursa ili kuwa na maendeleo makubwa kiuchumi.

Kenya anapambana akamate soko la mizigo la Uganda, Sudani Kusini , Ethiopia na baade Afrika ya Kati kupitia Sudani Kusini. (Kupitia mpango wao wa The Northen Corridor)

Wiki hii Waziri wa Miundombinu wa Uganda ametangaza wanaanza ujenzi wa reli (SGR) kutoka Malabo hadi Kampala. Huku Kenya anapambana kufikisha SGR yake Malabo kutoka Mombasa.

Sisi tunapeleka SGR hadi Burundi na kisha Congo (alafu tunalizika tu). Hivi tunashindwaje kuipeleka hadi kagera iingie Uganda alafu tupambane ifike hadi Sudani Kusini kabla ya Kenya?

Kama tungekuwa na Baraza la Mawaziri lenye akili zinazochaji kweli sasaivi nilitegemea tuwe na taarifa ya SGR kufika kagera mpaka wa Tanzania na Uganda alafu watu wanapambana iunganishwe hadi kufika Sudani Kusini.

Viongozi wetu wanalala sana. Ujinga wa Watanzania unawafanya wasiumize kichwa kufikiri kwa ajili ya kesho ya Tanzania zaidi ya Matumbo yao tu.

OMBI KWA RAIS SAMIA
Anzisha ujenzi wa Reli ya SGR kuelekea Kagera ifike hadi mpaka wa Tanzania na Uganda haraka iwekekanavyo kabla ya Kenya hajaanza kutekeleza ujenzi wa SGR Mombasa- Kisumu- Malabo.

Lord denning
Sinza, Dar es Salaam!
 
Wewe ndiye utajenga hiyo reli ndani ya nchi ya watu?, kwani ziwa Victoria haliwezi kutumika kusafirisha mizigo ya Sudan kusini?
Kwani SGR ya sasa inajengwaje Burundi?

Umeishia darasa la ngapi?

Hujui sisi tukiwahi kuifikisha SGR mpakani mwa Uganda na Tanzania kabla ya Kenya itasababisha Uganda na South Sudan wabadili mipango yao na kuja Tanzania hivyo Tanzania kufaidika zaidi?
 
Baraza mawaziri wote wana lorties na buses....unategemea nini ? Malori Abdul yatafsnya nini ? Ya Mwigulu ? Wapiga deal tuuuu
 
Kipaumbele Kwa Sasa ni zanzibar.hujasikia mama amesema wizara ya miundombinu waharakishe ujenzi wa daraja kuunganishwa Zanzibar?
 
Baraza mawaziri wote wana lorties na buses....unategemea nini ? Malori Abdul yatafsnya nini ? Ya Mwigulu ? Wapiga deal tuuuu
Hii battle ya uchumi ya Afrika Mashariki ingeikuta nchini yetu ina watu smart na sharp nchi yetu ingekuwa mbali sana ndani ya muda mfupi sana

Unaweka reli ya umeme hadi kyaka pale alafu unamsikilizia Museveni. Nyingine unafikisha Rusumo pale kuingia kwa Kagame.

Unaweka nyingine hadi mpaka wa Burundi na nyingine unamaliza mipaka ya Zambia na Malawi.

Kama hatujawa Transport Hub East and Central Afrika basi kuna uchawi. Maana nchi zote lazima zitapambana zijiunganishe na hiyo reli kwa urahisi wa usafirishaji wa mizigo yao
 
Kipaumbele Kwa Sasa ni zanzibar.hujasikia mama amesema wizara ya miundombinu waharakishe ujenzi wa daraja kuunganishwa Zanzibar?
Tunaweza kuwa na vipaumbele vyote na tukafanikiwa
 
Kama jiwe angekuwepo jamaa allikua na mapubgufu yake ila jamaa angeweza kulifanyia kazi hilo ila kwa mama tuache kwanza amalizie kazi nzito ya miradi mikubwa alio achiwa na mzee.Wakija wengine 2025 Walifanyie kazi hilo maana litaongeza mizigo bandarini na watz tunaweza kupata fulsa huko.
 
Kama jiwe angekuwepo jamaa allikua na mapubgufu yake ila jamaa angeweza kulifanyia kazi hilo ila kwa mama tuache kwanza amalizie kazi nzito ya miradi mikubwa alio achiwa na mzee.Wakija wengine 2025 Walifanyie kazi hilo maana litaongeza mizigo bandarini na watz tunaweza kupata fulsa huko.
Bandari zetu zote zinaweza kuwa busy 24/7 tukilifanya hili.

Hii nchi imekaa kwenye eneo zuri sana kijiographia shida Katiba yetu inasababisha tuwe na viongozi wa hovyo sana kiasi ambacho tunaenda mwendo wa kinyonga
 
smart is relative, binafsi naona vingine, reli ilipaswa isambazwe ndani ya tanzagiza yetu kwanza kabla ya kufikiria kuhudumia foreigners, meaning reli ya dar/tanga- moshi-arusha iende mpaka kanda ya ziwa; tazara ifufuliwe kuunganisha mikoa ya kusini maeneo ya ifakara-iringa mpka mbeya na ruvuma yaunganishwe na bandari; mikoa ya kanda ya ziwa nyasa iunganishwe na outside world kupitia mtwara corridor project iliyokuwa advanced sana na raisi B.Mkapa kuunganisha mikoa ya ziwa nyasa na bandari ya mtwara, kwangu mimi hiyo ndiyo inapaswa kuwa priority, hizo nchi jirani iwe by the way tu kwamba itawafikia tukishafikisha reli kwa watu wetu kwanza …
 
smart is relative, binafsi naona vingine, reli ilipaswa isambazwe ndani ya tanzagiza yetu kwanza kabla ya kufikiria kuhudumia foreigners, meaning reli ya dar/tanga- moshi-arusha iende mpaka kanda ya ziwa; tazara ifufuliwe kuunganisha mikoa ya kusini maeneo ya ifakara-iringa mpka mbeya na ruvuma yaunganishwe na bandari; mikoa ya kanda ya ziwa nyasa iunganishwe na outside world kupitiq mtwara corridor project iliyokuwa advanced sana na raisi B.Mkapa kuunganisha mikoa ya ziwa nyasa na bandari ya mtwara, kwangu mimi hiyo ndiyo inapswa kiwa priority, hizo ncho jirani iwe by the way tu kwamba itawafikia tukishafikisha reli kwa watu wetu kwanza …
Una wazo zuri ila reli kwa faida kubwa ni vizuri isafirishe both mizigo inayotoka ndani na nje ya nchi. Focus iwe mizigo ya nchi na nchi.


Sie ndio lango la kwenda Asia, Australia na Ulaya kwa ukanda huu. Tukiweza kulitumia hili vizuri tutafaidika sana!
 
Back
Top Bottom