Tupeane mawazo wapendwa

Tupeane mawazo wapendwa

Nyumba ndogo inahusika kushape nyumba kubwa kwa taarifa yako.[/QUOTE


jamani jamani jamani....hivi wewe Fidel180 upo over 18 kweli???,
hili jibu laweza kuwa jibu tata la kwanza kwangu kwa mwaka huu,
KIVIPI????,
Ila bado nina mashaka sana na age yako,
nahisi bado upo kwenye ile age ileeeeeeeeee.....
wakubwa wezangu nahisi mtanielewa....lol

Mi mbona nahusika sana kusaidia ndoa zenye migogoro
 
Ulokole peke yake hautoshi kusimamisha ndoa...
Ndoa ina nguzo zake, kama kuheshimiana, kusikilizana, Upendo, Hekima etc etc...
.. maana mnaweza mkaishia kushusha mapazia nje ya ratiba, ha ha haaa!.

Nadhani wengi wetu tunahitaji more, hatuzingatii ipasavyo au hatujui nini heshima, masikilizano na upendo unaotakiwa kwenye ndoa. Labda imefika wakati wa kufafaua haya na kutaweka sawa ili kila mmoja wetu ayaelewe kabla hajaingia kwenye ndoa.
 
Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Wanandoa wengi hasa wa miaka ya sasa, wakikorofishana korofishana baada ya muda wanachoamua ni tuachane bwana kila mtu ataanza nataka niishi kwa amani, nahitaji furaha mimi maisha yenyewe mafupi haya. Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.

Dear maty yaani leo umegusa mtima muhimu sana katika maisha yetu ya sasa. Kusema ukweli hal hii inatisha na kwa bahati mbaya sana ndio kwaaanza inakamata chati kwa kasi. Sometimes nasema bila kumtanguliza MUNGU katika ndoa na maisha yetu, mambo kama haya ni inevitable kabisa. Na kama ulivyosema ndoa za wenye viwango flani vya elimu mamb ndo huwa magumu zaidi kuliko ndoa ambazo wanaume ndo wenye elimu au mali kuliko wanawake. Kwenye ndoa ambayo wenzi wote wana viwango sawa vya elimu au kipato mara nyingi kuna mambo ambayo katu hayatavumilika na pande yoyote kati yao. Mf. Katika ndoa kama hii kwa wale wanaume wenye tabia ya kunyanyasa wanawake kwa kisingizio kuwa ni mkewe na hapaswi kuuliza, hoji au kufuatilia mambo anayoyafanya yeye kama mume ni wazi akileta ubabe kwa vitu ambavyo ni obvious mke atapata kichwa kuwa asimbabaishe.
hali kadhalika mke anawezakuwa ndo chanzo cha matatizo especially kama naye akikinga mkono kiganja kinajaa....... anawezajikuta analeta hadithi za usawa mpaka kwenye kugawa dozi............jana nilikupa leo nami napumzika (utadhani akitoa anayefurahia ni mpewaji tu). Sasa kwa mwanaume mwenye mke wa hivi ni lazima hatakubali na ataona ni bora atafute amani huko inakopatikana.

Ni tofauti na nyumba ambayo mke ni msomi, mume msomi but kila mtu anajua na kutimiza wajibu wake kama mume/mke na kama Baba/mama. Hawa wataishi kwa amani pamoja na kuwepo kwa migongano ya kawaida, heshima inatawala zaidi na kila mtu anatambua thamani ya mwenzie. Kinyume cha hapo ni kutengana.
wa maisha halisi ya w



Hapo kuna watoto mmezaa, lakini kila mtu utamsikia napenda kuishi kwa amani, ni vipi kuhusu watoto? Je hao hawatakiwi kuishi kwa furaha na amani wakiwa na baba na mama? Hivi hamuwezi kukaa mkazungumza na kuelewana ili mlee watoto pamoja badala yake mnafikiria kuachana?

Darling maty...........when worse comes to worse sometimes ni bora mkatengana kuliko kuwakuza watoto katikati ya uwanja wa vita. Madhara yake ni makubwa kuliko yale wanayoyapata kwenye utengano kwani huko unawezakupanga mpangilio maalumu. Kulea watoto ndani ya ndoa yenye migongano kila kukisha (sisemi ile ya kawaida) but sometimes watu wanakuwa na irreconciliable issues ambazo nyingine wanashindwa kabisa kuzicontant na kutozionyesha kwa watoto. Mfano kupigana, kutukanana, kunyanyasana n.k. madhara ni makubwa sana kisaikologia kwa watoto wanaokulia ndani ya familia za aina hizo na usijeshangaa mtoto akakua na yeye kuwa violent au na tabia za ajabu kwa familia yake........ni effect aliyoipata wakati anakua na ameichukulia ndivyo ndoa zilivyo au zinavyotakiwa ziwe. Mtoto anayekuwa kwenye familia ambayo mama yake haeshimiwi, ananyanyaswa na mama huyo kukaa kimya naye atachukulia kuwa ndivyo mke mwema anavyopaswa kuwa...so mkewe akiwa tofauti tu ni tatizo. The same kwa watoto wa kike, kama baba ananyanyaswa, anatukanwa au anapigwa watategemea kupata wenzi wenye nidhamu kama baba yao.

So I dont think kuwa mara zote kutengana ni kuwadeprive watoto amani. ila tu kuwe na zingatio kubwa katika kujaribu kuwaelewesha why hali imekuwa kama ilivyo (epuka kuonyesha ubaya wa mwenzi wako kwa watoto)


Hivi kuachana ni suluhisho la matatizo yako? Na je ukiachana na mwenzio ndio kusema hutaki kuoa/kuolewa tena? Na je ukioa/olewa halafu huyo mwingine akawa na matatizo pia pengine kuliko uliyoyakimbia mwanzo utaachana nae pia? Au utavumilia?

Tushirikiane kupeana mawazo wandugu

Maty unauliza maswali mengii............. kuhusu kama ni suluhisho ninawezasema ndio na hapana. Itategemea unapoamua kuachana na mwenzi wako umejipangaje kukabili maisha yako ili usijikute kwenye wakati mgumu utakaokufanya ujutie maamuzi yako. Lakini vile vile kabla hujaamua "mimi sasa basi" ni vema ukachukua muda mzuri wa kukaa na kutafakari ili kujidhihirishia kuwa unachukua uamuzi sahihi na changamoto zake unazijua vema na una mikakati ya kukabiliana nazo. Epuka kuamua kwa hasira. Itakuumiza mwenyewe.

Kuhusu kuoa/olewa tena...............uhmmmmm inategemea na kama uliamua kuufungua tena moyo wako kwa mwingine na kama maamuzi yako ya kuolewa/oa yalishirikisha experiences ulizozipata kwenye ndoa yako ya mwanzo. Usikurupuke kwa kuwa tu kuna jamaa kakutamkia anakupenda na wewe ukataka kumdhihirishie mtalaika wako kuwa "yeye alipokuwa akisema wa nini, kuna walokuwa wanajiuliza watakupata lini" utaumbuka.

Usinisahau kadi ya mwaliko mamito
 
unatakiwa kubalance baina ya uvumilivu na mateso, hivi kama nina uhakika mai waifu anamgaia uroda jirani yetu ndio nivumilie tu kwa ajili ya watoto? khaaaa! si nitakufa bila symptoms?,
on the other hand uko right kama makosa yenyewe ni kunuka kikwapa, sijui asubuhi anachelewa kupiga msuwaki, sjui akinuna havai nguo za ndani, n.k , hapa tunapaswa kufikiria watoto


yaani jamani v2ko vyako mie vinaniacha hoi,hahaha nimecheka kwa nguvu zote sio mzima kabisa wewe haki ya nani vile.
 
Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Wanandoa wengi hasa wa miaka ya sasa, wakikorofishana korofishana baada ya muda wanachoamua ni tuachane bwana kila mtu ataanza nataka niishi kwa amani, nahitaji furaha mimi maisha yenyewe mafupi haya. Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.

Hapo kuna watoto mmezaa, lakini kila mtu utamsikia napenda kuishi kwa amani, ni vipi kuhusu watoto? Je hao hawatakiwi kuishi kwa furaha na amani wakiwa na baba na mama? Hivi hamuwezi kukaa mkazungumza na kuelewana ili mlee watoto pamoja badala yake mnafikiria kuachana?

Hivi kuachana ni suluhisho la matatizo yako? Na je ukiachana na mwenzio ndio kusema hutaki kuoa/kuolewa tena? Na je ukioa/olewa halafu huyo mwingine akawa na matatizo pia pengine kuliko uliyoyakimbia mwanzo utaachana nae pia? Au utavumilia?

Tushirikiane kupeana mawazo wandugu

hivi kile kitufe cha thanks nani kakiona?

ntarudi baadae aisee..
 
kaka/dada mcdhani kuna mtu anapenda kutengana na mwenzi wake na mkumbuke kuna mengine hayazungumziki/hayana suluhisho/yameshindikana...ikiwa hivyo inabidi tu.

Hapa ndo unapo ona ile point yangu ya zamani hit and run inavyo kuwa nzuri.
 
Jamani samahani sikujua kuwa njimeandika makitu marefu hivi duh..........wapi wanatoa mafunzo ya hatimkato?
 
Tena nakwambia Nyamayao ukikuta mtu ana imani zake utakoma kumbadili ni ngumu sana sikuzote ana amini ayafanyayo ni sahihi mpaka unabaki kujiuliza anayetakiwa kumsemea hayo ni nani ,waeza amini unafanya yaliyo sahihi kwa mwenzako kumbe ni kero tupu.




mie nina frnd wangu aliolewa na hawa wachungaji wa makanisa ya kiroho, haikupita miezi 6 ile ndoa ilivunjika, matatizo yaliyoporopmoshwa hapo na frnd wetu ni ya kuchosha nafc, usuluhisho ulikuwa historia kwenye hii ndoa, sasa kila mtu anaishi maisha yake, mchungaji cjui yupo kinshansa huko mdada kashaolewa upya...yaani jamani hizi vurugu cjui zinatupeleka wapi jamani.
 
Ndoa nyingi za wasomi ndio huwa zina matatizo. Na matatizo mengi kwa kiasi kikubwa huwa yanasababishwa na akina mama, tena kama mama ana elimu kubwa au ana uwezo mkubwa wa kipesa kuliko baba hapo tena ndo balaa. Ule ubaba unakuwa hauna maana kabisa. Mama ndo atataka kutawala nyumba, ukisema hiki jibu lake usinibabaishe na visa kedekede. Jaribu kufanya kautafiti kadogo tu, hata viongozi na wasomi wengi wanawake aidha huwa hawana waume au ndoa zao huwa zina migogoro mikubwa sana.

Ninayo mifano mingi sana ambayo nimeishuhudia mimi mwenyewe ya wanandoa ambao mama aidha ana uwezo na elimu kubwa kuliko baba au wako sawa. Wengine huwa wanafikia hata hatua ya kulala vitanda tofauti, asubuhi kila mtu anaondoka na gari yake japo wanafanya kazi ofisi moja. Basi ilimradi vurumai.
Akina mama/dada jirekebisheni (siwatuhumu). Fedha na elimu haviwezi kununua mapenzi.
Katika hili naomba tuwe wakweli na wawazi kabisa, mwanamke analaumiwa kwa vile ni mwanamke lakini si ndoa zote zenye matatizo wanawake ndio tatizo, no no no no and big no!!!!!!!!! Nina mfano mzuri kabisa wa mwanaume mwenye gubu lisiloelezeka! Angalia kwanza
Mwanaume form iv
Mwanamke Masters
Mwanaume baba wa nyumbani
Mwanamke anafanya kazi yenye akili
Mwanamke ndo anaendesha familia including yeye mwanaume hadi gari mwanaume kamnunulia na mambo mengine meeeeengi
Lakini cha ajabu na kushangaza mwanaume hajatulia na ana gubu acha tu hadi watu wanamuonea huruma mwanamke. Sasa hapo utasema wanawake wana matatizo jamani? Mwanaume na mwanamke woooooote wanapaswa kuheshimiana kama mke na mume si jukumu la mwanamke pekee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Inategemea unawaza nini maishani mwako. Kama unadhani kila kitu ni mteremko maishani basi ndoa siyo mchezo. Ukisikia mtu anakwambia nina miaka kumi ndani ya ndoa, jua kuna mishale mingi, mvua nyingi zimemnyeshea lakini amevumilia. Dunia ya sasa watu tunakosa uvumilivu, hata mumeo ama mkeo awe mbaya vipi, kuna moment mnashare ambazo kila mmoja anakuwa na furaha. Kugombana ndani ya ndoa ni kitu cha kawaida sana. Kinachahitajika ni kumuelewa mwenzio na yeye pia akuelewe. Kila mtu alizaliwa na kulelewa na wazazi tofauti, pia malezi nayo yanatofautiana. Kwa hiyo mlipokutana kila mtu alikuwa na tabia yake. Ku-i-shape hiyo tabia ya kila mmoja siyo tendo la siku moja. Uvumilivu unahitajika sana. Suluhisho siyo kukimbilia kuachana bali kuwaza ni wapi tunapokosea mpaka tushindwe kuishi. Jambo lingine linalotuharibu, tunaiga sana tamaduni za wenzetu. Wao kuoa na kuolewa ni fashion, believe me.. huwa wanaumia sana pia inapofika wanapoachana. Cha kujiuliza ni kwa nini wanakimbilia sana kuachana na mwisho wa siku wanalia divorce inapokuwa finalized??? All the best kwa wenye ndoa kama mimi..
 
Jamani samahani sikujua kuwa njimeandika makitu marefu hivi duh..........wapi wanatoa mafunzo ya hatimkato?

Ujifunze kuandika vifupi vifupi maana wengine tunashindwa kusoma mpaka mwisho tunasoma mwanzo katikati ya mistari na mwisho
 
Tena nakwambia Nyamayao ukikuta mtu ana imani zake utakoma kumbadili ni ngumu sana sikuzote ana amini ayafanyayo ni sahihi mpaka unabaki kujiuliza anayetakiwa kumsemea hayo ni nani ,waeza amini unafanya yaliyo sahihi kwa mwenzako kumbe ni kero tupu.

mie naamini kumbadili m2 mzima ni ngumu sana, huwa nawapa pole sana wale wanaoingia kwenye game kwa imani kwamba Asprin ni mlevi/mhuni wa kutupwa lakini mbeleni nitambadilisha, nabakiaga nashangaa, ni bora uingie ukikubaliana na alivyo huku ukiendelea kumbadili ukifanikiwa sawa, ikila kwako ujue uliamua mwenyewe tokea mwanzo...kumbadili kiumbe ni kitu kigumu sana.
 
Back
Top Bottom