Tupia vimbwanga vya siku ya mtihani wa darasa la saba

CharmingLady

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2012
Posts
18,296
Reaction score
12,972
Kwa kuanza tuwaombee dua wanetu, wajukuu zetu, wadogo zetu wanaofanya mitihani yao leo na kesho...

Turudi kwenye mada,

Nakumbuka siku moja kabla ya mtihani wangu wa darasa la saba tulikwenda shule kuosha madawati, tulikuwa na viwembe kukwangua michoro na maandishi yote kwenye madawati. aisee tulisugua na kukwangua mpaka madawati yakawa kama yamepigwa randa.

hebu na wewe tupia tukio ulilofanya wakati wa mtihani wa darasa la saba.

CL
 
Nilikuwa Bingwa wa Kucheza na Akili za wasimamizi CABED nakumbuka bado hiyo Code wakati naingia kufanya mtihani.
 
nakumbuka nlkuwa najaza majibu kwenye mtihani then kabla ya dkk 10 mtihani kuisha ndo nahamishia kwenye answer booklet
Themi Primary School Arusha.
 
Nilimuona jirani yangu anahangaika nikawa namwachia adese ila jamaa akawa haelewi halafu msimamizi alikua mdada yuko poa tu.
 
Nakumbuka matukio mawili.
1. Kuna jamaa tulimfaulisha akaingia deko kiulaini kabisa, tulikua tunamjazia majibu au tunampa karatasi akopi ila chujio la form two lilimpenda zaidi akabaki.

2. Kuna kama alikua anatuongozea toka darasa la 3 had Ia saba, nlijua had I seko atakua anaongoza yeye ila pepper la from two hakuweza chomoka
 
hivi huko madarasa ya chini kuna vituko kama vyuoni? 😂😂😂😂 maana vyuo ni shinda sana mtu kumeza karatasi ya kibomu bila maji ni kiti rahisi sana...

elimu yangu ya msingi nilikuwa katoto sana hatukuwa na vituko kabisa
 
Rubber band zilitumika sana kutransfer chabo (unaweka kikaratasi kwenye rubber band kisha unamlenga mhusika), msimamiz alikuwa zake bize anasoma gazeti la michezo[emoji4] [emoji1]
 
Nilikuwa na kalamu za biki 3 na kompasi utazani nilikuwa na mchoro wa hesabu wa kuchora. Ila nilifaulu vizuri sana Math 47, Lugha 44, Maarifa (Siyo yamii) hapa naamanisha Geo, Sayansi, Historia, S/Kimu, S/Kilimo nk 49 nikapelekwa shule nzuri sana enzi hizo tunaita za vipaji
 
Umenikumbushà mbalii
 
Nakumbuka siku ya mtihani kwa vile tunashinda shuleni kutwa nzima, hivyo tunaenda na chakula, jamaa mmoja jina nimemsahau alikuja na machapati magumu hayo af yanaunga..... hakuwa na soda wala maji anayatafuna ivo ivo....... dah....... mademu wakamuonea huruma walimrundikia mamisosi, mzee baba alikula kinoma... kufika class tumbo likaanza kuzingua..... dadek..... kila akienda toi, akirud kabla hajakaa..... kainuka..... ilikuwa balaa. ikabidi atoke na mwalimu mmoja wakae karibu na toi hadi amalize pepa.
 

Matokeo ya Primary hayabandikwi, ulijuaje?
 
Kama sio Gilman Rutihinda hyo shule!basi private!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…