Tupia vimbwanga vya siku ya mtihani wa darasa la saba

Tupia vimbwanga vya siku ya mtihani wa darasa la saba

Nakumbuka siku ya mtihani kwa vile tunashinda shuleni kutwa nzima, hivyo tunaenda na chakula, jamaa mmoja jina nimemsahau alikuja na machapati magumu hayo af yanaunga..... hakuwa na soda wala maji anayatafuna ivo ivo....... dah....... mademu wakamuonea huruma walimrundikia mamisosi, mzee baba alikula kinoma... kufika class tumbo likaanza kuzingua..... dadek..... kila akienda toi, akirud kabla hajakaa..... kainuka..... ilikuwa balaa. ikabidi atoke na mwalimu mmoja wakae karibu na toi hadi amalize pepa.
Hamjupikiwa pilau mzee, mm nakumbuka mwaka ule tulikula shuleni
 
Darasa la saba tulinunua majibu kwa shilingi 15,000/-, mimi nikakubaliana na jamaa niliyekaa naye dawati moja snipe 5,000/- nimpe majibu yote.

Tulifanya paper zote na nilimpa majibu yote ila hakunipa hata 100, akamwambia mzee wake, mzee wake akamwambia baba, baba akaja kunibana nikamwambia ilibidi nifanye hivyo kwa sababu zile karatasi za majibu zilikuwa zikiletwa wanaziona na alitishia kunisema.

Matokeo yalivyotoka jamaa hakufaulu, tuliofaulu ni wale tuliotoa hela peke yake, akaanza kulalamika kwamba nilimpa majibu ya uongo, nikamuuliza ulitoa sh ngapi?

Kitu ambacho sielewi mpaka leo ni kwa nini tuliowapa majibu hawakufaulu wakati tumejaza sawa sawa.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] du! Mm hadi Leo sielewi ilikuwaje nikafaulu vizuri std 7 wakati hakukuwa na wizi wala kuoneshwa majibu
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] du! Mm hadi Leo sielewi ilikuwaje nikafaulu vizuri std 7 wakati hakukuwa na wizi wala kuoneshwa majibu

Mimi nilikuwa best class, na ile mitihani ya kata nilikuwa ni lazima niwe wa kwanza.

Ila kabla ya paper mwalimu mkuu alimfata mdingi akamwambia, hata kama mwanao ana akili, hawezi kumshinda mwalimu wake.

Kwa hiyo akaambiwa ni lazima atoe hiyo 15,000/- hata kama sitayatumia majibu.

Na hata majibu yalivyokuwa yanaletwa muda mwingi nakuwa nimeshamaliza, nabaki nalinganisha, na kuna makosa walikuwa wanayaweka ili tusifanane.
 
Kwa kuanza tuwaombee dua wanetu, wajukuu zetu, wadogo zetu wanaofanya mitihani yao leo na kesho...

Turudi kwenye mada,

Nakumbuka siku moja kabla ya mtihani wangu wa darasa la saba tulikwenda shule kuosha madawati, tulikuwa na viwembe kukwangua michoro na maandishi yote kwenye madawati. aisee tulisugua na kukwangua mpaka madawati yakawa kama yamepigwa randa.

hebu na wewe tupia tukio ulilofanya wakati wa mtihani wa darasa la saba.

CL
Sasa hiki ni kimbwanga au usafi tu kawaida?
 
Back
Top Bottom