Tupime Pombe na Madawa ya Kulevya kwa Wafanyakazi Taasisi za Serikali na Bunge

Tupime Pombe na Madawa ya Kulevya kwa Wafanyakazi Taasisi za Serikali na Bunge

Chaliifrancisco

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2015
Posts
26,021
Reaction score
79,710
Mimi kama Mtanzania mwenye nia nzuri na malengo na hii nchi japo nimetamani kuikimbia na nimepata nafasi kadhaa ila nikaamua kubaki naomba kupendekeza ofisi za serikali na bunge zianze kupima pombe na madawa ya kulevya.

Hii itasaidia kuondoa wafanyakazi na wabunge ambao wanafanya maamuzi ya kipuuzi ambayo mwisho wa siku yana madhara ya kudumu kwa walipa kodi wa nchi hii.

Akikutwa mtumishi na BAC (Blood Alcohol Concentration) ya zaidi ya 0.02 wakati anaingia kazini au akiwa kazini basi ni termination bila warning yoyote.

Na ikitokea mfanyakazi iwe waziri au balozi wa nyumba kumi amefanya maamuzi yasiyo sahihi au yakuleta maswali apimwe pombe na pia mkojo kugundua kama anatumia madawa ya kulevya.

Kuna kampuni za kigeni zinazingatia haya kwa kujali usalama mahali pa kazi. Je sisi kama watanzania tunashindwa nini? Kwani breathalysers ni bei gani? Je ni bora kununua hizo breathalysers au kuendelea kuliteketeza taifa?

Mtumishi wa umma ama mbunge anaingia kazini/bungeni akitokea bar saa 12 asubuhi je huyu atafanya maamuzi sahihi kwa taifa letu?

Naomba serikali ije na mpango huu kambambe ili tupunguze wasiokuwa na akili serikalini na taasisi zake pamoja na bunge.

Tuwapime pombe na madawa ya kulevya. La sivyo tutaendelea kupiga hatua kurudi nyuma.

Nawakilisha.
Mwananchi aliechoshwa.
 
Du ha ha ha! Simply not practible huku duniani ili sergion awe na ujasiri kumpasua mgonjwa kwanza anapata glass ya hard drink na operation inaenda vema je utamfukuza kazi?
 
Du ha ha ha! Simply not practibe huku duniani ili sergion awe na ujasiori kumpasua mgonjwa kwanza anpata glass ya hard drink na operationi inaenda vime je utamfukuza kazi?
Huu ni upuuzi mliokaririshwa kijinga. Hakuna surgeon anaelewa kama ana thamini uhai wa mgonjwa wake. Kama unabisha ma surgeon hapa jukwaani watanipinga.
 
Hii concentration ya 0.02 ni % au ppm? au ppb? ppt? au molar concentation? Tuanzie hapo kwanza. Ukute unataka kuleta unit standards ambayo hata kifaa cha kupima hatuna hapa nchini.
Haelewi alichoandika msamehe tu huoni kakimbia
 
Waitara na Kitwanga walitumbuliwa uwaziri kwasababu ya ulevi
 
Hii concentration ya 0.02 ni % au ppm? au ppb? ppt? au molar concentation? Tuanzie hapo kwanza. Ukute unataka kuleta unit standards ambayo hata kifaa cha kupima hatuna hapa nchini.
0.10 g of alcohol for every 100 ml of blood. How do you calculate that? Ni ppt au ppm?
 
[emoji3][emoji3][emoji3] wabongo tumekuzwa kwa uongo uongo tu , daktari wa upasuaji lazima anywe kidogo ndo anapiga kazi vizuri , oooh mwalimu wa hesabu !
 
[emoji3][emoji3][emoji3] wabongo tumekuzwa kwa uongo uongo tu , daktari wa upasuaji lazima anywe kidogo ndo anapiga kazi vizuri , oooh mwalimu wa hesabu !
Upuuzi mtupu mkuu. Wenzetu ndio wapo hivyo? Akina Einstein au Tesla au Marie Curie walikuwa wanakunywa kwanza ndio wafanye waliyofanya?
 
0.10 g of alcohol for every 100 ml of blood. How do you calculate that? Ni ppt au ppm?au
Hiyo ni 0.1% w/v (weight to volume) alcohol. Yaani kila 100 ml kuna 0.1% ya alcohol, Kwa hiyo kama una total volume ya 5000ml ya damu utakuwa na total alcohol ya 5% siku hiyo, mlevi sana.......utakuwa huna tofauti na Kitwanga au Pierre Liquod
 
Hiyo ni 0.1% w/v (weight to volume) alcohol. Yaani kila 100 ml kuna 0.1% ya alcohol, Kwa hiyo kama una total volume ya 5000ml ya damu utakuwa na total alcohol ya 5% siku hiyo, mlevi sana.......utakuwa huna tofauti na Kitwanga au Pierre Liquod
Ndio hali halisi hiyo. Tuwe na waleta maamuzi ambao wako sane maana pombe ina currupt medulla za watu wanafanya maamuzi ya kiduanzi.
 
Back
Top Bottom