Tupumzike sasa sio kwa joto hili la Dar es Salaam

66% Dunia ingeganda, viumbe wengi wangekufa
 
Sasa mkuu unataka kubishana na wataalamu au ..
Alafu hayo ni mabadiliko ya hali ya hewa unapozungumzia kufa kwa watu kule makka na hii habari yangu huoni unachanganya mambo.
Wewe labda ndio unabishana na wataalam na uhalisia pia....
Mimi nakuambia joto linaongezeka pande za Kaskazini mwa dunia nikakutolea na mifano halisi
 
Wewe labda ndio unabishana na wataalam na uhalisia pia....
Mimi nakuambia joto linaongezeka pande za Kaskazini mwa dunia nikakutolea na mifano halisi
Daaah tatizo lako ww ujajua hii concept ipo vipi...?
Kwahiyo walitupa hiyo habari wanajichanganya au..
Mana hapa ubishani na mimi ila unabishana na mamlaka ya hali ya hewa mkuu
 
Mkuu ahsante kwa kunitag. Ni jambo zuri kuwa na nia ya kujifunza zaidi kuhusu matukio ya anga na afya bora.

Hata hivyo, ni muhimu kuthibitisha taarifa kabla ya kuzishiriki. Baadhi ya madai uliyotoa kuhusu Aphelion na athari zake kwa afya si sahihi kisayansi.

Tofauti ya umbali kati ya Aphelion na Perihelion (hatua karibu zaidi na Jua) ni takriban kilomita milioni 5, siyo milioni 62 kama ulivyoelezea. Hii ni tofauti ndogo sana (3.1%) na haisababishi mabadiliko makubwa ya joto.

Mabadiliko ya umbali kutoka kwenye Jua hayana athari kubwa kwenye hali ya hewa ya Dunia kwa sababu ya Dunia kujizungusha kwenye mhimili wake. Mhimili huu ndiyo sababu kuu ya misimu yetu, sio umbali kutoka katika Jua.

Aphelion haisababishi moja kwa moja kuongezeka kwa magonjwa kama vile homa na kikohozi. Hali ya hewa ni moja tu ya sababu zinazoathiri magonjwa haya.

Nawasilisha mkuu
 
Mkuu wewe upo kitengo cha haya mambo au ni vile ume deep down sana geography mkuu
 
Joto joto...
Ndani hapakaliki
Ofisini hapakaliki
Mtaani ndo kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…