Tuseme tu ukweli, ujenzi unahitaji kujinyima sana

Tuseme tu ukweli, ujenzi unahitaji kujinyima sana

Gharama kubwa au ndogo? Mkoani na nyumba ya vyumba 3,one master ,jiko ,stop,sebule,public toilet na vivaranda 2.
Sijajua kwa mkoani, ila kwa Dar hiyo burget ni ndogo....japo nasikia kuna baadhi ya maeneo kama Chanika wanajenga kwa gharama hiyo...ila maeneo kama Mbezi, Goba ni ndogo.
 
Sijajua kwa mkoani, ila kwa Dar hiyo burget ni ndogo....japo nasikia kuna baadhi ya maeneo kama Chanika wanajenga kwa gharama hiyo...ila maeneo kama Mbezi, Goba ni ndogo.
Hadhi ya eneo na eneo na pia kila mtu ana requirements na standards za nyumba anayoitaka,kwa hiyo ni sahihi hiyo bajeti kuwa ndogo .
 
Wizi wa vifaa na mafundi.Fundi aliyenishangaza Sana ni WA vioo na rangi huyu nilimwamini sana kwa kuwa nilisikia kuwa ni Mchungaji wa Kanisa x lkn ajabu alinifanyia uhuni,nikabaki mdomo wazi.
Wabaya sana hao
 
Ukitaka kujenga kwa haraka na pesa huna hapo ni kweli unahitaji kujinyima.

Ukitaka kujenga kwa haraka na pesa unazo hauhitaji kujinyima kwa sababu pesa ya bata utakuwa nayo na pesa ya kujenga itakuepo.

Na ukitaka kujenga haraka na pesa hauna hapa ndio tatizo utaona kila kitu ni kufuja kwa sababu unataka haraka.

Jenga taratibu huku unakula maisha,ukifa hiyo nyumba mwanao atauza na pesa atatumia kwa mambo mengine,au ataimalizia na kukaa yeye na vile itakavyouzwa unaweza kusema kwamba aliyeijenga hakujinyima,yani inauzwa kana kwamba aliyejenga hakupata tabu,inauzwa kana kwamba aliyejenga hakuwa na shida nayo yaaaaani,inauzwa kana kwamba ni mzigo wa fitina utawagombanisha ndugu yaani,hiyo ni nyumba yakoo mkuu.

Nashangaa mtu anatumia 80% ya kipato chake kujengea,wakati wadau werevu hutumia 30% ya kipato kujengea.


Hakuna haja ya haraka,fanya haraka kutafuta KIWANJA.
Nyumba yangu mpaka inakamilika idara zote ilinichukua 10 yrs kwa sababu nikipata milioni moja napeleka only laki tano ili maisha mengine yaelendelee na kwa kweli sikupata maumivu yoyote...
 
Kujenga nyumba ya "kuishi" ni kupoteza rasilimali.. Jenga nyumba ya kuuza au kupangisha.. full stop..

Wanaojinyima wanajenga nyumba za kuishi na hapo ndipo fikra zao zinapoishia..
Kuna tofauti gani kwenye gharama za kupangisha kwa miaka 30 na kuishi kwenye nyumba yako uliyojenga ndani ya hiyo miaka 30?
 
Nilijua utanijengea kumbe mafundi unawabana pia.Aise
Kuwabana ni kwamba upo sitte full time...hawa ukiondoka utakuta mlango wa garage unafungikia kuelekea ndani. Vibarua ndio kabisaaaa ata kama ni baba yako akili zao zakijinga sana.
 
Kuwabana ni kwamba upo sitte full time...hawa ukiondoka utakuta mlango wa garage unafungikia kuelekea ndani. Vibarua ndio kabisaaaa ata kama ni baba yako akili zao zakijinga sana.
Yeah sure
 
Kuna tofauti gani kwenye gharama za kupangisha kwa miaka 30 na kuishi kwenye nyumba yako uliyojenga ndani ya hiyo miaka 30?

Kujenga nyumba ya kupangisha ili ufaidike nayo ni lazima iwe eneo prime na nyumba yenye hadhi. Hizi za uswahilini ni hasara tupu.
 
Tatizo unalazimisha kujenga wakati wewe uwezo wako ni wa kujilisha tu
Utaingia nyumba mpya na vidonda vya tumbo ushangae watoto wote wanalia vidonda vya tumbo kumbe ni kujibana kula Ili ujenge
 
Nimesoma comments zote za wadau nimeishia na msimamo kuwa maisha mafupi bear tamu
 
Hahah [emoji23]

Kula bia tu mjuba
Msinitanie baba yangu ana nyumba tatu mbili kapangisha alafu watoto tupo watatu tu Tena wawili wakike alafu eti nianze kuwa na wasiwas sijui kujenga badala ya kununua mapira makali Kama vile allteza au harrier.ngoja Kwanza tutambe kwanza road
 
Msinitanie baba yangu ana nyumba tatu mbili kapangisha alafu watoto tupo watatu tu Tena wawili wakike alafu eti nianze kuwa na wasiwas sijui kujenga badala ya kununua mapira makali Kama vile allteza au harrier.ngoja Kwanza tutambe kwanza road
Nakubali mkali [emoji23][emoji1696]

Tafuta mpira mkali wa kuvimba nao.
 
Kuna fundi kaniambia wanajenga kwa 200 tofali moja

So unahesabu tofali unazidisha mara 200 unamlipa mnaachana
Una namba zake huyo fundi, tofali moja nilijengewa kwa Tsh 300, mwaka Jana 2021
 
Back
Top Bottom