Tuseme ukweli kuhusiana na Bidhaa za Azam. Kuna mengi tunayanyamazia…

Kunywa juice za viwandani siyo ujanja ila ni umasikini. Tunakunywa kwa sababu.
1. Hatuna vifaa kama blender za kutengeneza juice nyumbani.
2. Hatuna pesa ya kununua matunda ya kutosha kutengeneza juice.
3. Hatuna muda wa kutengeneza juice, una liamsha saa 10 alfajiri unarudi nyumbani saa 4 usiku hoi.
 
Hata ingekuwa hamsini kama wakiharibu wataambiwa tu. Unauliza maswali ya kipumbavu ambayo hayana msingi.
Uzuri ni kuwa pamoja na kupayuka hovyo hovyo lakini bado utarazimika kutumia bidhaa za Azam maana hazikwepeki.
 
Wenzangu na mimi waroho kutoka rohoni....
Tukutaneeee kuja jambo letu.
 
Nishagombana na wife nimemwambie asiwape hayo madude watoto haelewi
 
Kwa hoja zako basi vinywaji vyote vinavyo tengenezwa viwandani havifai maana vyote vina tengenezwa na kuhifadhiwa na kemikali ambazo ni hatari kwa maisha ya mwanadamu.
Angeleta hoja wa kuwa vinywaji vyote vina tengenezwa viwandani havifai hapo hoja zake zingekuwa na mashiko na sio kuishambulia Azam.

Hivi nikikuuliza soda ya Coca-Cola,pepsi au grand Malta vinatengenezwa kwa tunda gani unaweza kunipa jibu?
 
[emoji3586]AZAM EMBE NI SALAMA KWA MATUMIZI YA BINADAMU[emoji3586]
[emoji3591]Kuna kipande Cha video kinasambaa mitandaoni kikionyesha kuwa juisi ya "AZAM EMBE" Ina madhara kwa binadamu, inasababisha ugonjwa wa kansa. Madai ya msambazaji wa video hiyo ni kuwa ndani ya juisi hiyo kuna mchanganyiko wa viungo vinavyotumika kuhifadhi juisi isiharibike haraka kama "Benzene" na "Ascorbic Acid", ambavyo mchanganyiko wake unasababisha ugonjwa wa kansa kwa watumiaji wa juisi hiyo.

[emoji3591]Kwanza nimrekebishe msambazaji wa video hii ya kuwa kwenye viambata/viungo vilivyotumika kwenye kuhifadhi juisi ya "AZAM EMBE", hamna kiambata Cha "Benzene", isipokuwa kuna kiambata Cha "Sodium Benzoate (E211)", hivyo "Benzene" inaweza kuja kuzalishwa kwenye juisi kama matokeo lakini sio lazima izalishwe. Hivyo kutoa hitimisho la moja kwa moja kuwa ndani ya juisi Kuna "Benzene" ni makosa.

[emoji3591]Sasa tuanze kuichambua "Benzene" kama msambazaji wa video anavyotaka kuogopesha umma kutokana na hatari yake kiafya. Wataalamu wa fani ya Kemia wanathibitisha kuwa karibu asilimia 99% ya "Benzene" inayoweza kuingia katika mwili wa binadamu inatokana na vyanzo vya asili kama kuchomwa kwa misitu, uvutaji wa sigara, harakati za milima yenye volcano, kuungua kwa mafuta kama ya kuendesha mitambo kama petroli, dizeli, n.k. Hivyo kama kweli muandaaji wa video ana lengo la kweli la kutaka kulinda afya za wanadamu, basi awekeze nguvu kwenye kupiga vita hizi asilimia 99%, kuliko kukazana na asilimia 1% ya "Benzene" inayompata mwanadamu kupitia vyakula. Mfano kwa siku inakisiwa mtu mmoja anayekaa jirani na mvutaji sigara anafyonza "Benzene" mwilini mwake kiasi cha microgramu 200-450 kwa siku.

[emoji3591]Je sumu ya "Benzene" inaweza kuzalishwa kwenye juisi?

Ni kweli sumu ya "Benzene" inaweza kuzalishwa kwenye juisi pindi "Sodium Benzoate" itakapokutana na "Ascorbic Acid"(Vitamin C), lakini sumu hiyo, itazalishwa pindi kutakapokuwa na joto la kati ya Sentigrade 40-60, kuwe na mwanga wa kutosha (UV-Light), lakini pia kuwe na Metali nzito kama madini ya chuma (Fe) na Copper (Cu), tena kuwe na hali ya ya utindikali wa kuanzia PH 3-5.

[emoji3591]Je utazuiaje uzalishwaji wa sumu ya Benzene kwenye juisi na vinywaji vinginevyo?
[emoji1484][emoji1484]
(I)Tunza kinywaji chako kwenye ubaridi chenye viambata vya Sodium Benzoate na Ascorbic Acid kwenye joto chini ya Sentigrade 40. Ndio maana ukichukua kopo la AZAM EMBE wameandika "Best served Cold" (Bora ukitumia ikiwa baridi).Hiyo "Best served Cold" inakusaidia kwenye ladha lakini pia kwenye kuzuia kuzalishwa kwa sumu ya Benzene.

(II)Zuia mwanga wa jua kwenye kinywaji chako
Ndio utakuta kwenye kopo la juisi ya "AZAM EMBE", wameandika kwa maandishi ya herufi kubwa "WEKA MBALI NA MWANGA WA JUA"

(III)Kuongeza kwa sukari
Kinywaji chochote kama kitakuwa na sukari, sukari itazuia utengenezwaji wa "Benzene". Sasa ukisoma lebo ya AZAM EMBE utakuta kiwango Cha sukari kilichopo ni 12g.

[emoji3591]Je Bidhaa za vinywaji zenye "Sodium Benzoate" na "Ascorbic Acids" ni salama kwa matumizi?
Bidhaa hizo ni salama kutumia kwa sababu kiwango cha Sodium Benzoate na Ascorbic Acids zinazowekwa kwenye bidhaa hizo Huwa kinapitishwa na kamati ya wataalamu bobezi inayoitwa (JECFA) "Joint Expert Committee on Food Additives of the WHO/FAO". Kamati ambayo imekubaliana kiwango cha Benzene kama kitakuwa kwenye bidhaa basi kisizidi 5 ppb (parts per bilion). Yaani kwa hesabu nyepesi, chukua 5 ugawe kwa Bilioni 1,( 5/1,000,000,000), jawabu lake ndio kiwango kinachotakiwa kisizidi kwenye bidhaa. Nadhani unaona ni kwa namna gani kiwango ni kidogo sana[emoji1787][emoji1787][emoji1787].

[emoji3591]Kwa kuhitimisha, usiogopeshwe sana na maneno ya kimombo kama "Benzene", ukajua unatakiwa uiepuke kwa asilimia 100, katu huwezi kwa sababu vyakula vya asili kama nyanya,karafuu,tufaha(Apple), na vinginevyo vina "Benzoic Acid" ya kutosha ambayo inaweza kuwa chanzo Cha "Benzene" hata kama utakwepa juisi ya AZAM EMBE. Lakini hiyo "Ascorbic Acids" anayoitaja kwa mbwembwe ndio vitamin C tunayoitafuta kila siku kwa kula matunda kama machungwa, embe, n.k...

Imetayarishwa na;
Badi M.Bao: Human Nutritionist & Food Technologist
Email: badi.bao11@gmail.com
Phone: 0625920847/0684900249
 
Jambo la uhakika ni kwamba lazima mabadiliko yafanyike katika uandaaji wa hiyo juice bila hata kufika huko mahakamani

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Utetezi wa kipumbavu sana.
 
Wewe jamaa unaishi nchi gani ? Ina maana hujapata habari za ongezeko la kansa nchini hasa kanda ya ziwa !!

Unataka ushahidi gani zaidi ya huo kwamba Azam wenyewe wameandika ingredients, haupo rational kabisa, comment yako inaonesha unaongozwa na hisiq katikq kufikiri
 
Unahamisha magoli.... Naomba nijibu kwanza maswali yangu mawili..
1)Barua ya TBS ni uongo unaikataa
2)Lete picha ya juisi ya Azam ikiwanna ingredients zake...ili kama hazipo zilizoelezwa na TBS .
 
Unahamisha magoli.... Naomba nijibu kwanza maswali yangu mawili..
1)Barua ya TBS ni uongo unaikataa
2)Lete picha ya juisi ya Azam ikiwanna ingredients zake...ili kama hazipo zilizoelezwa na TBS .
Na ukiangalia ni Juisi zake pekee ndo zina benzene, za wengine hazitoi benzene.

Swala hapa ni TBS ichunguze na kumuagiza aziondoe madukani
 
Umeambiwa kansa utaiona kwa muda mfupi hivyo, uchukua miaka na visababishi ni vingi sana sio hiyo benzene peke yake. Afya yako ni uamuzi wako mkuu.
 
Umeambiwa kansa utaiona kwa muda mfupi hivyo, uchukua miaka na visababishi ni vingi sana sio hiyo benzene peke yake. Afya yako ni uamuzi wako mkuu.
Nalielewa hilo, pia naielewa saratani vizuri tu.. pia nafanya kila njia (inayowezekana) kuiepuka. Visababishi ni vingi ikiwemo infection za baadhi ya virus, sumu zitokanazo na pombe, mionzi kadha wa kadha, sumu za baadhi ya vyakula n.k
Kitu cha muhimu kwangu ni kuwa na kinga imara ikiwemo kutumia bidhaa bora. Kwa kufupisha maelezo ni kuwa, bidhaa za Azam ni moja ya bidhaa za vyakula bora kabisa kwetu Tz na nchi jirani.. vifingashio vyake vinajieleza! TBS, Kenya Bureau of Halal Certification zinathibitisha hilo!!!
Cha ajabu huyo aliyeanzisha hicho kioja cha Sodium benzoate vs vitamin C, hata kuandika tu hajui (sarufi hajui, r na l ni shida kwake afu anajiita dokta). Tufike mahali tuwe na akili.. vipi kama Azam wangelijua hilo kosa na wangeliamua kutoandika kiambata kimoja wapo kwa lengo la kuficha hilo kosa! Je, wangekuwa certified na TBS na KBHC?
Kwangu mimi- kama bidhaa za Azam ni sumu, basi hakuna tena bidhaa za kiwandani za Tz zinazofaa kiafya..chunguza vifungashio vya bidhaa za vyakula za makampuni kadhaa ya Tz.. most of them kuna makosa kadha wa kadha yapo nje nje...🚶
 
Maelezo bora kabisa yanayojitosheleza.. bahati mbaya kwa wengi humu ni kama 'kipini cha dhahabu kwenye pua ya nguruwe'
 
Mimi juice local ama za kampuni local sinywi hata kwa bunduki.

Azam anasema ni maembe pure, ulishawahi kuona makontena ama malori ya maembe ama ukwaju kwenda Azam?

Mimi juice za kopo nitakunywa imported tu otherwise nitakunywa maji.
 
Kiwanda Cha Azam kilichopo Mwandege nimeenda kufanya project mara mbili na mara moja kuomba kazı!
Ukweli ni kwamba Maembe anayotumia ni halisi, yanatoka kwa wakulima na chama chao kinaitwa CHAMAVITA kama nipo sahihi....hata ukipita pale Mwandege utaona magari ya Maembe yamepaki nje yakisubiri kupakuliwa!
Na nlipata kupita stage karibuni zote za uchakataji WA matunda
Ila kuhusu hizo chemical zenu sijui lolote lile!
Narudia kuhusu matunda....ni matunda halısı anatumia kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio Azam tu hata Mo ni shida tupu tena Mo ni shida zaidi maana ye hupenda ku-copy sana bidhaa za wenzie
 
Mkuu Azam ungeachana naye maana hutaeleweka... halafu hunA utakachopata. Mtu ana utAjiri wa trillions huko wakati wewe hata milioni mbili cash huna... Unakuja kuleta porojo.....kumhusu.. umekula lakini..
Unaharibu afya wewe unazungumzia utumbo afya za watoto na wananchi wengine zinaharibiwa wewe unaongea nini
Shida ulikimbia chemistry
Ukadhani chemistry Iko kwenye vitabu tu
Kumbe Iko katika maisha yetu ya Kila siku
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…