Tusidanganyike, Kiongozi aliyepatikana kwa hila, Utiifu wake ni kwa waliompachika

Tusidanganyike, Kiongozi aliyepatikana kwa hila, Utiifu wake ni kwa waliompachika

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Tumeshuhudia uchaguzi uliojaa uchafu wa kila aina, kuanzia kanuni za hovyo kabisa za kusimamia uchaguzi, uandikishaji wa wapiga kura bandia, uenguaji wa wagombea, mpaka utengenezaji wa kura bandia, kamatakamata ya wanaozuia kura za wizi, mpaka mauaji ya wanaoonekana ni kikwazo dhidi ya uovu wa kupokonya maamuzi ya wananchi.

Lengo la haya yote, ni kuwanyima haki wananchi ya kuwachagua viongozi wanaowataka. Watawala wameamua wawape wananchi watu wa kuwatawala.

Hawa viongozi walioletwa na watawala ili wawatawale wananchi, utiifu wao ni kwa aliyewapa hizo nafasi, kamwe hawawezi kuwa na wananchi, kamwe hawawezi kuwatetea wananchi. Wananchi watambue kuwa wameletewa vibaraka wa watawala ambao jukumu lao kubwa ni kutekeleza matakwa ya waliowateua.

Huu ni ukoloni mpya wa watu weusi dhidi ya weusi wenzao. Akina Chabruma, Mkwawa, Isike, Mirambo, japo hawakuwa na elimu, lakini walipambana kwa mioyo yao yote kuukataa ukoloni. Leo pamoja na elimu zetu za kwenye makaratasi, tumeshindwa kupambana na ukoloni mbaya zaidi kuliko hata ule wa mzungu.

Hata katika unyonge mbaya kabisa, tunastahili kuupinga ukoloni huu mpya.

Yeyote anayezuia wananchi kuwachagua viongozi wanaowataka, ni adui yetu, ni adui wa Taifa, kupambana dhidi yake kwa namna yoyote inayowezekana ni halali.
 
Watanzania wanaelewa na kufahamu ni nani mwenye uwezo wa kuwaongoza na chama kipo chenye kubeba Matumaini yao.watanzania kwa akili zao Timamu na ufahamu wa kutosha wanatambua wazi ya kuwa ni CCM pekee na wagombea wa CCM wenye uwezo wa kuwaongoza na kuwaletea maendeleo.watanzania wanatambua ya kuwa ni CCM pekee yenye uchungu na Maisha yao.ndio maana wana imani na CCM na ndio maana wameipigia kura za kutosha na kwa wingi mkubwa sana.

Watanzania hawataki ubabaishaji wa vyama vya upinzani kama CHADEMA ambavyo viongozi wake ni wababaishaji,wasaka Tonge na wachumia tumbo tu waliojaa ulaghai mtupu.

Embu angalia mtu kama lissu atalalamika vipi kuwa chama chake kimeshindwa uchaguzi au kilipaswa kushinda wakati hata yeye mwenyewe hakupiga kura? Nani atakipa ushindi CHADEMA wakati hata viongozi wake wenyewe kama Lissu hawajapiga kura na wala hawakujiandikisha?
 
Tumeshuhudia uchaguzi uliojaa uchafu wa kila aina, kuanzia kanuni za hovyo kabisa za kusimamia uchaguzi, uandikishaji wa wapiga kura bandia, uenguaji wa wagombea, mpaka utengenezaji wa kura bandia, kamatakamata ya wanaozuia kura za wizi, mpaka mauaji ya wanaoonekana ni kikwazo dhidi ya uovu wa kupokonya maamuzi ya wananchi.

Lengo la haya yote, ni kuwanyima haki wananchi ya kuwachagua viongozi wanaowataka. Watawala wameamua wawape wananchi watu wa kuwatawala.

Hawa viongozi walioletwa na watawala ili wawatawale wananchi, utiifu wao ni kwa aliyewapa hizo nafasi, kamwe hawawezi kuwa na wananchi, kamwe hawawezi kuwatetea wananchi. Wananchi watambue kuwa wameletewa vibaraka wa watawala ambao jukumu lao kubwa ni kutekeleza matakwa ya waliowateua.

Huu ni ukoloni mpya wa watu weusi dhidi ya weusi wenzao. Akina Chabruma, Mkwawa, Isike, Mirambo, japo hawakuwa na elimu, lakini walipambana kwa mioyo yao yote kuukataa ukoloni. Leo pamoja na elimu zetu za kwenye makaratasi, tumeshindwa kupambana na ukoloni mbaya zaidi kuliko hata ule wa mzungu.

Hata katika unyonge mbaya kabisa, tunastahili kuupinga ukoloni huu mpya.

Yeyote anayezuia wananchi kuwachagua viongozi wanaowataka, ni adui yetu, ni adui wa Taifa, kupambana dhidi yake kwa namna yoyote inayowezekana ni halali.
Ndiyo maana leo hii tuna kusanyiko la wahuni wanaojiita bunge, kila ujinga utakaoletwa pale na serikali wanapitisha kwa vile wameingizwa pale kwa mabavu ya vyombo vya dola hivyo utii wao ni kwa dola na siyo wananchi kwenye majimboni watokako.
 
Back
Top Bottom