Tusiendekeze nyadhifa(titles) za kifamilia katika siasa na uongozi wa umma

Tusiendekeze nyadhifa(titles) za kifamilia katika siasa na uongozi wa umma

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kuitana "mama yangu", "baba yangu", "mdogo wangu", "kaka yangu", "dada yangu", "shangazi yangu", "shemeji yangu" na vyeo vingine kama hivyo katika shughuli za siasa na umma ni utamaduni mpya uliovuka mipaka, kushika kasi na sasa unaanza kukomaa.

Zamani vyeo vya kifamilia ambavyo nilikuwa nimevizoea ni "mzee" ikasogea mbele kidogo ikawa "kaka" kwa wingi, sijui wanasiasa wamegundua nini sasa hivi idadi kubwa kama sio karibia wote wanaitana kwa vyeo vya kifamilia katika shughuli zote za umma.

Rudini kwenye mtindo wenu wa zamani tu wa kuitana ndugu, komredi na kamanda. Utamaduni mpya sasa unapelekea viongozi wadogo kuanza kujimilikisha viongozi wa umma wakubwa kama mama au baba zao jambo ambalo sio sahihi.

Japo inaweza kuonekana ni kama uungwana fulani bado sio sahihi kabisa viongozi kuanza kuitana na kuchukuliana kwa mfumo huo wa kifamilia kwa sababu itapeleka kuwa vigumu kuwajibishana, itazidisha tabia ya kuchukulia uongozi kwa mazoea na pia itapelekea kupeana nafasi na fadhili(favours) isivyostahili.
 
Huu upuuzi unalelewa na kuendekezwa na makada muflisi wa CCM. [emoji31][emoji31]
 
Kuitana "mama yangu", "baba yangu", "mdogo wangu", "kaka yangu", "dada yangu", "shangazi yangu", "shemeji yangu" na vyeo vingine kama hivyo katika shughuli za siasa na umma ni utamaduni mpya uliovuka mipaka, kushika kasi na sasa unaanza kukomaa.

Zamani vyeo vya kifamilia ambavyo nilikuwa nimevizoea ni "mzee" ikasogea mbele kidogo ikawa "kaka" kwa wingi, sijui wanasiasa wamegundua nini sasa hivi idadi kubwa kama sio karibia wote wanaitana kwa vyeo vya kifamilia katika shughuli zote za umma.

Rudini kwenye mtindo wenu wa zamani tu wa kuitana ndugu, komredi na kamanda. Utamaduni mpya sasa unapelekea viongozi wadogo kuanza kujimilikisha viongozi wa umma wakubwa kama mama au baba zao jambo ambalo sio sahihi.

Japo inaweza kuonekana ni kama uungwana fulani bado sio sahihi kabisa viongozi kuanza kuitana na kuchukuliana kwa mfumo huo wa kifamilia kwa sababu itapeleka kuwa vigumu kuwajibishana, itazidisha tabia ya kuchukulia uongozi kwa mazoea na pia itapelekea kupeana nafasi na fadhili(favours) isivyostahili.
Hi wa ccm wanaipita kama hawajaiona,hivi ukiwa na chama cha ccm huwa wanalogwq nini hata mabaya wao ndiooo
 
Ajabu ni kuwa anaye itwa "mama yangu mpendwa" akiitwa anachekelea bila aibu!
Nakumbuka Nyerere alikataza kumuita "mtukufu Rais" bali aitwe "ndugu Rais".
Haya yametokea wapi?

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Cha kwanza ni kuitoa nafasi ya Rais kwa mama!
Kila kitu, kila mtu kila hali ni mama mama mama!
Kesho na kesho kutwa ikitokea mwanaume tunaweza kuendeleza hii title na kuanza kuita baba.
 
Nilichokiona Makonda kaumia sana kuondolewa Kuwa mwenezi, na anawasiwasi wa kupigwa chini kabisa,anachofanya saiv nikutumia gharama yeyote aonewe huruma na Raisi
 
Hakuna binadamu mwenye dhambi kubwa kama kumtukuza binadamu mwenzie, hawa wanaweza hata kumsujudia kiongozi na yeye akacheka cheka tu huku akijua fika ni dhambi kubwa sana
Najua ukiwa mwanasiasa na kiongozi basi unakuwa huwa dini
Ndio maana unaona hata viongozi wa Dini wakianza kusifia wanavuka mipaka na kujisahau kabisa na kumsahau Mungu kabisa

Mungu awahurumie tu ila kumtukuza kiumbe ni laana kubwa sana
Na wakitimuliwa ndio wa kwanza kutukana na kuanza kumkumbuka Mola wao , utasikia Riziki anatoa Mungu bwana
 
Nilichokiona Makonda kaumia sana kuondolewa Kuwa mwenezi, na anawasiwasi wa kupigwa chini kabisa,anachofanya saiv nikutumia gharama yeyote aonewe huruma na Raisi
Hizo ni siasa wanakua vizuri hao ndio maana wanateuana wao Kwa wao kila siku na bado maovu wanasingiziana wao,,,sifa wanapeana wao,,kula nchi wanakula wao lakini hujawahi sikia wala kuona wanachukuliana hatua stahiki NI makelele tuu yakuwaona hao wanaowaita wanyonge wajisikie faraja ili Kodi zinazotokana na nguvu za hao wanyonge waendelee kuzitafuna
 
Back
Top Bottom