Tusimlaumu Makamu, bali tuulaumu uongozi wa juu hata kama haturuhusiwi kuongea ukweli

Tusimlaumu Makamu, bali tuulaumu uongozi wa juu hata kama haturuhusiwi kuongea ukweli

Mr Dudumizi

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2020
Posts
7,799
Reaction score
14,215
Habari zenu wana JF wenzangu,

Ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika hapo juu.

Wana JF wenzangu, siku mbili tatu zilizopita tumeshuhudia lawama, kejeli na vijembe kutoka kwa watu mbali mbali wakimlaumu makamu mwenyekiti wa Chadema mh Lisu kwa kukimbia mapambano mapema na kukiacha chama kikiwa hakina muelekeo wa maana kisiasa. Watu wengi wameonekana kumlaumu makamu huyo bila kujua hasa chanzo halisi na cha kweli kilichomkimbiza m'beleji huyo alieingia nchini wiki tatu tu zilizopita baada ya kukaa Ubelgiji kwa zaidi ya miaka miwili kwa kile kinachofahamika na watu wengi wenye akili kwamba alikimbia aibu ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Ndugu Lisu alipotangaza kuja au alipoingia nchini chawa wengi walionekana kuwa na matumaini nae na kufikiri kwamba makamu huyo anakuja kukijenga tena chama ambacho kinaonekana kimeyumba haswa baada ya kuwa na shutuma kwamba mwenyekiti wa chama hicho taifa amelamba asali na kukiuwa chama kiaina, hali inayopelekea wananchi wengi wakose imani nacho.

Sasa inashangaza makamu huyo baada ya kuingia amefanya mikutano yake miwili mitatu bila kupata support ya aina yoyote kutoka kwa wale aliowatarajia. Lakini ukiachana na hayo ya kususwa katika mikutano hapo chini naorodhesha mambo makubwa yaliomfanya makamu huyo aingie mitini na kukitelekeza chama hicho.

1) Kitendo cha mwenyekiti wa chama kuvuta mpunga na kukikodisha chama hicho kwa Lowasa bado kipo katika akili ya makamu huyu japo kwa sasa hawezi ongea kwa sababu na yeye alimegewa fungu na kujikuta anameza matapishi yake mwenyewe.

2)Kitendo cha mwenyekiti kulamba asali na kuvuta ruzuku za wale covid 19 kimya kimya kupitia account ya uchochoroni pia kimemfanya makamu achukie kwani msimamo wa chama na wa mwenyekiti wa chama ni vitu viwili tofauti.

3) Katibu mkuu wa sasa hana muelekeo, ushawishi na uthubutu kama ule aliokuwa nao yule wanaemwita Dr Mihogo.

4) Chama kukosa muelekeo maana toka ruhusa ya mikutano ianze ni viongozi wachache tu wa chama hicho ndo wamejishirikisha na mikutano ila wengine wanaonekana kuwa busy na mambo yao ya kuwaingizia kipato chao kwa ajili yao na familia zao.

Hakuna mtu mwenye akili angekubali kuja kusimama juani kutwa nzima kusikiliza sera za kupigwa bunduki nk huku watoto nyumbani wakiwa hawajui watakula nini. Wakati huo huyo aliekusimamisha juani watoto wake wako Marekani wanakula bata na tayari wana uraia wa nchi hiyo.

Sababu zilizomkimbiza Lisu ni nyingi ila hizo ni baadhi tu. Siku akitoka chamani au kuachana na siasa atakuwa na mengi ya kuongea. Maana jamaa huwa ni mtu wa visasi kwahiyo naamini na haya yaliomchukiza na kumkimbiza kuna siku atayaongea tu. Let's wait time will tell.

J2 njema.
 
Hamna kitu hapo nguvu ya Maghufuli ndo imeua chama Kwa wananchi hasa baada ya kifo chake cha kimaghumashi, na matusi anayotukanwa sasa kuanzia serikalini mpak Chadema , ukiunganisha na huduma za hovyo serikalini + ugumu wa maisha Kwa kiasi kikubwa hayo ndo yamefutilia mbali morally ya wananchi na kuona kumbe jiwe alikuwa sahihi kwenda against nao....!!!

Lissu ameona no time to waste kila mmoja apambane na Hali yake
 
Ndugu mwana wanachukua chako mapema, a.k.a chawa wewe na Chadema wapi na wapi, 🤔 huo usemaji wa chama nani kakupaa ?au uchawa ndio shida yenyewe? Acha wenye chama wakisemee chama chao🤔
 
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika hapo juu.

Wana JF wenzangu, siku mbili tatu zilizopita tumeshuhudia lawama, kejeli na vijembe kutoka kwa watu mbali mbali wakimlaumu makamu mwenyekiti wa Chadema mh Lisu kwa kukimbia mapambano mapema na kukiacha chama kikiwa hakina muelekeo wa maana kisiasa. Watu wengi wameonekana kumlaumu makamu huyo bila kujua hasa chanzo halisi na cha kweli kilichomkimbiza m'beleji huyo alieingia nchini wiki tatu tu zilizopita baada ya kukaa Ubelgiji kwa zaidi ya miaka miwili kwa kile kinachofahamika na watu wengi wenye akili kwamba alikimbia aibu ya kushindwa vibaya katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Ndugu Lisu alipotangaza kuja au alipoingia nchini chawa wengi walionekana kuwa na matumaini nae na kufikiri kwamba makamu huyo anakuja kukijenga tena chama ambacho kinaonekana kimeyumba haswa baada ya kuwa na shutuma kwamba mwenyekiti wa chama hicho taifa amelamba asali na kukiuwa chama kiaina, hali inayopelekea wananchi wengi wakose imani nacho.
Sasa inashangaza makamu huyo baada ya kuingia amefanya mikutano yake miwili mitatu bila kupata support ya aina yoyote kutoka kwa wale aliowatarajia. Lakini ukiachana na hayo ya kususwa katika mikutano hapo chini naorodhesha mambo makubwa yaliomfanya makamu huyo aingie mitini na kukitelekeza chama hicho.

1) Kitendo cha mwenyekiti wa chama kuvuta mpunga na kukikodisha chama hicho kwa Lowasa bado kipo katika akili ya makamu huyu japo kwa sasa hawezi ongea kwa sababu na yeye alimegewa fungu na kujikuta anameza matapishi yake mwenyewe.
Kitendo cha mwenyekiti kulamba asali na kuvuta ruzuku za wale covid 19 kimya kimya kupitia account ya uchochoroni pia kimemfanya makamu achukie kwani msimamo wa chama na wa mwenyekiti wa chama ni vitu viwili tofauti.
3) Katibu mkuu wa sasa hana muelekeo, ushawishi na uthubutu kama ule aliokuwa nao yule wanaemwita Dr Mihogo.
4) Chama kukosa muelekeo maana toka ruhusa ya mikutano ianze ni viongozi wachache tu wa chama hicho ndo wamejishirikisha na mikutano ila wengine wanaonekana kuwa busy na mambo yao ya kuwaingizia kipato chao kwa ajili yao na familia zao.

Hakuna mtu mwenye akili angekubali kuja kusimama juani kutwa nzima kusikiliza sera za kupigwa bunduki nk huku watoto nyumbani wakiwa hawajui watakula nini. Wakati huo huyo aliekusimamisha juani watoto wake wako Marekani wanakula bata na tayari wana uraia wa nchi hiyo.
Sababu zilizomkimbiza Lisu ni nyingi ila hizo ni baadhi tu. Siku akitoka chamani au kuachana na siasa atakuwa na mengi ya kuongea. Maana jamaa huwa ni mtu wa visasi kwahiyo naamini na haya yaliomchukiza na kumkimbiza kuna siku atayaongea tu. Let's wait time will tell.

J2 njema.

We ndio umeingia zamu jioni hii? Utakuwepo zamu kwa muda gani leo?
 
Hamna kitu hapo nguvu ya Maghufuli ndo imeua chama Kwa wananchi hasa baada ya kifo chake cha kimaghumashi, na matusi anayotukanwa sasa kuanzia serikalini mpak Chadema , ukiunganisha na huduma za hovyo serikalini + ugumu wa maisha Kwa kiasi kikubwa hayo ndo yamefutilia mbali morally ya wananchi na kuona kumbe jiwe alikuwa sahihi kwenda against nao....!!!

Lissu ameona no time to waste kila mmoja apambane na Hali yake
Sera za Magufuli zipo ndan ya ilani ya CCM + na sera za Samia zipo ndan ya ilani hiyo hiyo ya CCM.

Mziki ni kwa wale waliwatukana wazalendo wa kweli wa nchi hii, i mean baba wa taifa mw. Nyerere na hayati Magufuli lazima wakumbane na adhabu yao kwanza hapa hapa duniani ili iwe funzo kwa wengine.
 
Ndugu mwana wanachukua chako mapema,a.k.a chawa wewe na Chadema wapi na wapi, 🤔 huo usemaji wa chama nani kakupaa ?au uchawa ndio shida yenyewe?Acha wenye chama wakisemee chama chao🤔
Hao unaosema wenye chama, huwa hawaruhusiwi kutoka hadharani na kuongea ukweli kama huu.

Nani wa kwanza unaejua aliwahi kuongea ukweli kuhusu chama chao. Mtaje hapa tumuone.
 
Mbona hukushauri msimpige risasi wakati ule?
Tumuulize mwenyekiti wa chama, kwanini kila anapotokea mtu ambae anahisi kwamba anaweza kumnyang'anya tonge mdomoni basi mtu huyo hufa kama Chacha Wangwe, hufukuzwa chama kama Zito au akinusurika kuuwawa hukimbia kama Lisu.

Tena haya hutokea pale unapokaribia uchaguzi mkuu wa chama.

Narudia tena, siku Lisu akiondoka Chadema au kuachana na siasa atakuwa na mengi ya kusema.
 
Tumuulize mwenyekiti wa chama, kwanini kila anapotokea mtu ambae anahisi kwamba anaweza kumnyang'anya tonge mdomoni basi mtu huyo hufa kama Chacha Wangwe, hufukuzwa chama kama Zito au akinusurika kuuwawa hukimbia kama Lisu.

Tena haya hutokea pale unapokaribia uchaguzi mkuu wa chama.

Narudia tena, siku Lisu akiondoka Chadema au kuachana na siasa atakuwa na mengi ya kusema.

Kesi ya Chacha Wangwe iliiendeshwa kwenye mahakama hizi hizi za CCM, kama hukuridhika na hukumu, unaweza kurudi mahakamani ukaweka ushahidi wazi ili muhalifu akamatwe.

Kuhusu Zito katiba ya CDM iko wazi kuwa mwanachama haruhusiwi kukipeleka chama mahakani. Zito alikiuka hili kwa kwenda mahakamani. Hata hivyo hakufukuzwa bali aliondoka mwenyewe ili akaanzishe chama na kupata nafasi aitakayo.

Lisu hana lolote la kupoteza na sio muoga wa kuongea ukweli. Kama alimwambia dhalimu ukweli wake wakati alikuwa anamiliki kundi la watu wasiojulikana, CDM wana nini cha kumtisha? Tafuta propaganda nyingine, hizi ni za kizee mno.
 
Mambo mawili:
1. Unapoanzisha uzi make sure heading inakuwa wazi kwetu wasomaji. Umeandika "Tusimlaumu makamu", mimi nikafungua uzi chapu chapu nikidhani ni Makamu wa Rais, kumbe ni lisu. Acha ulaghai bwashee.
1) Kitendo cha mwenyekiti wa chama kuvuta mpunga na kukikodisha chama hicho kwa Lowasa bado kipo katika akili ya makamu huyu japo kwa sasa hawezi ongea kwa sababu na yeye alimegewa fungu na kujikuta anameza matapishi yake mwenyewe.
2. Hiyo 👆 wala usingeiweka kama reason ya kumtetea, maana yeye pia alivuta mpunga. Tena mbaya zaidi, mwanzo alikuwa upande wa kundi letu, kundi la Dr Slaa na akina Mnyika, alipokatiwa mshiko akatusaliti na kuhamia kundi la kina mbowe. Kwa taarifa yako unatukumbusha maumivu, ambayo pia yamechangia kuiua chadema tuliyoijenga kwa jasho na damu!
 
Back
Top Bottom