Uchaguzi 2020 Tusimuache Lissu atuahidi yasiyowezekana

Uchaguzi 2020 Tusimuache Lissu atuahidi yasiyowezekana

Hiyo millioni 50 imezaa zahanati na umeme wa REA kila kijiji..kumbuka kujiungia umeme ilikuwa 170,000 na sasa ni elf 27 tu..upewe nini?
Zahanati na umeme vinatoa mikopo kama ahadi ilivyesema juu ya milioni 50?au na wewe ndo walewale pelekwapelekwa
 
Ungeacha jazba ujenge hoja,urais si uongozi ndani ya Chadema kwamba kila lopolopo apewe.Tafakari
KAMA ULIMWAMINI CHIZI,LAGHAI NA MWIZI ( hata rambi rambi,tr.1.5) UTASHINDWAJE KUMWAMINI MSEMA KWELI?
 
Point. CCM hawajawahi kujenga ofisi. Zote zilijengwa na serikali chini ya chama kimoja. Hivi vitoto vya Instagram ilibidi viombwe hata birth certificates kabla ya kuungwa JF. Unaweza kukuta mwingine kamaliza clinic mwaka juzi leo anaparamia JF.Utaumia, huku kuna think tanks. Hawa wanastahili FB na Insta

Sent from my TECNO KB8 using JamiiForums mobile app
Ccm hawajajenga ofisi katika Tanzania hii labda kama ni ktk nchi nyingine.

Ndivyo Kanu kule Kenya walijidanganya kuwa zile ofisi zilikuwa ni zao lkn siku walipotolewa madarakani hawakuamini macho yao.

Hivyo nyie jidanganyeni tu hivyo kuwa mna ofisi. No situation lasts for ever.
 
Mkuu ila tuwaache CCM na Magufuli waendelee kutuahidi ajira million 8 wakichaguliwa tena ?. Badala ya kupinga ahadi za Lissu, ungeanza kwanz na Magufuli na CCM yake, ambao wameshindwa kuajiri asilimia kubwa ya wahitim within 5years, watawezaje kutengeneza ajira million 8 ndani ya miaka mitano ijayo? . Kama sector binafsi imenyauka mpaka kufikia kuajiri watu 100k badala ya 500k + 2015 kushuka nyuma, hizo ajira zinatoka wapi ?

Kama watu waliomba Ajira serikalini kupitia secretariat ya Ajira toka 2015_ 2018, walikuwa 600k +, na waliopata kazi wakawa 6567 hizi ajira million 8 zinatoka wapi ? .Kama mabenki hayakopeshi kutoka na capital cost kuwa kubwa, hivo watu kutolipa mikopo na mabeki kuogopa kokopesha, then wanaenda kununua hati fungani za serikali zinazotumia muda mrefu ku mature, hivyo kuipa sector ya fedha badi inflow and outflow, hizo ajira zitatoka wapi ?. kwa mwenye akili ulitakiwa ujiulize kwanza huu ulaghai !
Mungu amekupa akili na maarifa kama una elimu sio lazima uajiriwe kuna shughuli nyingi za kufanya mpaka vijijini kwa nini usiw mbunifu kazi ni nyingi tena zinavipato zaidi ya ajira .
 
Hoja inahusu utekelezaji wa ahadi za lisu ususa swala la bima usilete habari za magufuli au membe au hashimu rugwe au lipumba elewa hoja acha ubishi
Mkuu hivi bima ya afya kwa watanzania ambao si kwamba wanaishi hospital na elimu bure kwa mtazamo wako kipi chenye gharama nafuu?
 
Mungu amekupa akili na maarifa kama una elimu sio lazima uajiriwe kuna shughuli nyingi za kufanya mpaka vijijini kwa nini usiw mbunifu kazi ni nyingi tena zinavipato zaidi ya ajira .
Mkuu elimu ndo inatakiwa iwe maarifa si maarifa ya kupewa na Magu.Magu yupo kwenye ajira maisha yake yote amejitutumua tu kuanzisha Ranchi baada ya kuwa rais na still anatumia resources za serikali kuendesha biashara zake binafsi ,angekuwa na maarifa angetegemea kuajiriwa ili aendeshe maisha yake,?
 
Kuna mgombea alisema anataka kuigeuza Tz iwe kama Ulaya,vip hapo.maana nadhani hiyo ndio ndoto kubwa isiyotekelezeka kuliko zote alizoota.
 
Lissu alikuaga mbunge lakini jimboni kwake sio ata pa kuongea kwa sauti ni mjini lakini hio aibu basi tu
Kwani Lissu anakusanya kodi?. Si hata kodi zilizokuwa zinakusanywa na halmashauri zimechukuliwa na serikali kuu, unatarajia afanye nini? Huyu mbunge aliyepo sasa hivi ameshafanya maajabu gani hadi sasa? Umeshatembelea majimbo mengine yaliyo chini ya ccm hapo mkoani Singida na kuona maendeleo yake?
 
TUSIMWACHE LISU ATUAHIDI YASIYOWEZEKANA.

Na Thadei Ole Mushi.

Kwenye kampeni za Lisu ana Mambo makubwa mawili anayowaomba watanzania wamchague nayo. Moja ni malalamiko yake ya kupigwa risasi hii Kwake Ni Kama Kete ya kuwaomba watanzania wamuonee huruma aingie Ikulu. Jambo la Pili ni Sera zake anazotakiwa awashawishi nazo watanzania ili wamchague kuwa Rais.

Nilishawahi kusema kuwa hakuna siku nitambeza Lisu kwa kupigwa Kwake Risasi na Wala sintoongea nikimuona analalamika kuwa mwili wake una machuma kila Mahali. Kama watanzania wataamua kumchagua kwa kuwa tu aliwahi kushambuliwa na watu wasiojulikana Hilo nimewaachia. Mimi nitajikita kwenye Sera zake ambazo kwangu ndio kipimo Cha kutoa kura yangu kumchagua Kiongozi katika ngazi zote iwe udiwani, Ubunge, au Urais nitazipima Sera kabla ya kuchagua.

Nimesikikiza Sera za mgombea urais Lisu anayo Mambo makuu matatu anayowaahidi watanzania kubwa kabisa ni kila mtanzania kumiki bima ya Afya, kupunguza Makato ya Wanufaika wa Bodi, kuleta maendeleo ya watu badala ya vitu. Haya ndio anayoyarudia kila Mara anaposhika kipaza sauti Leo tuongele moja kesho tutaongele lingine na leo tuanze na Bima ya Afya kwa kila mtanzania.

BIMA BURE

Nimejaribu ku survey nchi nyingi duniani, Ni nchi ipi yenye uwezo wa kuwapa wananchi wake wote Bima BURE sikuona.

Marekani ilijaribu kupitia Obama Care lakini baada ya Muda mfupi walishindwa na Obama care ikafa. Sababu kubwa Ni gharama za uendeshaji. Kutokana na U.S Census Bureau taifa la Marekeni lina watu milioni 28.1 tu ya wasiokuwa na Bima. Hivyo Obama care ilidhamiria kufanya Coverage ya watu milioni 28 tu kuwalipia huduma za Afya lakini wameshindwa kutokana na gharama zake. Hili ni taifa tajiri kuliko yote duniani limeshindwa kuwalipia watu milioni 28 tu je kwa Tanzania wenye Bima hawafikii milioni kumi je milioni Arobaini iliyobakia wanaofanya kazi wataweza kuwalipia gharama hizo?

Sababu nyingine ya wamarekani kukataa Obama care ni kuwa Kama itafanya kazi Kodi ingelipanda sana nchini marekani hivyo wakaamua kuitupilia mbali. Kuna nchi zinazotajwa kuwa na unafuu wa Bima Duniania lakini sio bure naomba kuzitaja:-

1.Ujerumani.

Ujerumani ndio taifa linaloonekana Kama Bima yake angalau Ina unafuu kwa wananchi wake. Lakini pia sio wajerumani wote ambao Wana Bima ya afya. Wafanyakazi wote nchini ujerumani wanalipia Bima zao kwa kushirikiana na waajiri. Wengine waliobakia wanalipia kiasi kidogo Bima zao.

2. Singapore

Singapore wao Wana mfumo wa Bima unaoitwa Medshield ambao serikali kwa asilimia kubwa ndio inabeba gharama za matibabu lakini kila mtu nchini Singapore anatakiwa alipie asilimia 10 ya kipato chako kwenye mfuko huo. Kama ni Mkulima wanakupigia mahesabu asilimia 10 ya unachokipata ulipie kwenye mfuko wa bima, Kama ni mfanyakazi vivyohivyo pamoja na kuwa unaonekaba kuwa mfumo Bora kuliko yote duniani lakini bado unalipiwa na wenye kipato kikubwa bado wanaumia sana kukatwa asilimia 10 kwa ajili ya Bima.

3. Japani

Japani wao Wana mfumo wa Bima unaoitwa SHIS mfumo huu nao watu wanatakiwa kujiandikisha na kulipia.

4. Uingereza.

Wao ndio kwa asilimia kubwa wamefanikiwa kwa kuwa hospital asilimia kubwa zinamilikiwa na serikali na wafanyakazi wote hulipwa na Serikali. Mfumo wao wa Bima wa NHS gharama zake zote hutolewa na Serikali. Ila bado una changamoto na mtu akitaka kutibiwa private ambako Kuna huduma nzuri na za haraka unatakiwa kulipia mwenyewe.

Hizo Zina unafuu Duniania Soma unafuu wake halafu tulinganishe na Tanzania.

Tanzania.

Tuna Bima ya NHIF ambayo huangaika na watumishi wa Umma na wategemezi wao. Huu tunauchangia asilimia Kama mataifa mengine yanavyouchangia. Tena asilimia tatu tu tofauti na mataifa Mengi sana Duniania.

Tuna mfuko mwingine iCHF (Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii ulio Boreshwa), huduma hii ya Bima ni kwa gharama nafuu kabisa kwa Watanzania wote katika Sekta ya Afya kwa Familia ya watu sita yaani Baba, Mama na watoto wanne kwa Tsh. 30,000/- tu kwa mwaka mzima. Una pata huduma zoote za matibabu kuanzia kituo kidogo cha Afya mpaka Hospital ya Mkoa.

Serikali Ina mpango pia wa kuleta Sheria Bungeni ya kuwataka watanzania wote kuingizwa kwenye mfuko wa Bima ya Afya.

Mimi nataka kufahamu Lisu anataka kuifanyaje hiyo Bima yake. Sio kwamba nambeza la hasha nataka kufahamu Bima yake anayoihubiri Ina nini ndani na itakuwa inafanana na ya nchi gani.

Tusimwache Lisu atudanganye Kuna haja ya kuchambua haya yanayoongelewa na wanasiasa. Kesho tutachanbua Sera ya Lisu nyingine.

Hoja yangu CHADEMA naomba muwaeleweshe watanzania hiyo Bima yenu ina package gani?

Ole Mushi
0712702602
Nafikiri amepotosha Makusudi kwa sababu ni mwanaFisiemu...

Katika suala la afya na bima, Lissu anazungumzia upatikanaji wa huduma za afya pamoja na unafuu wa gharama za matibabu....i.e. Accessibility and Affordability

Lissu hajasema kutakuwa na bima ya bure, isipokuwa anasema huduma z afya nchini zinaweza kuboreshwa kwa kila Mwananchi kuwa na bima ya afya iliyo nafuu....kwamba uchangiaji Utakuwa nafuu, atakayeweza kulipia huo unafuu ndo atafaidika...hoja kubwa hapa ni dhamira, bima ya afya isiwe exclusive kwa kundi flan tu...Kama Magustinho naye anataka aoneshe dhamira, yeye atafanya nini? Serikali yake itaendelea tu kukwanyua hela za NHIF na mifuko ya hifadhi ya Jamii kujenga madaraja?

La pili Lissu anakemea mfumo wa kibaguzi katika utaratibu wa sasa wa huduma za matibabu kwa bima ya NHIF...Lissu analalamika kuwa Serikali imekopa mabilioni ya fedha kutoka NHIF kiasi kwamba taasisi hiyo inaamua kuwadhulumu Wanachama wake kwa kuwanyima kupata huduma za matibabu kwa Kisingizio cha kiwango cha mchango wa mwanachama; kama mchango wako ni chini ya 600,000/- kwa mwaka hutibiwi, utaishia kuandikiwa panadol tu

Kingine Serikali haiwasilishi kwa NHIF makato ya Mishahara ya Wafanyakazi wake kwa ajili ya bima ya afya...wanakata hela halaf zinaliwa juu-kwa-juu

Kwa hiyo Lissu anakemea mambo Haya ni Lazima aungwe mkono!
 
Denmark wanatia bima kwa kila raia na hata wageni. Ukishapata working au permanent residence na raia wao wote unpewa kitambulisho Cha ukazi/uraia na yenyewe ni bima. Unaenda hospital yeyote kumuona Dr. Ni hurry, vipimo vyote ni bure, upasuaji wa Aina yeyote Ile bure. Unalipia dawa tu. Na dawa hiyo Ina subsidy (ruzuku) ukinunua dawa za DKK1000 utalipa 100% kuanzia 1001-2000 unalipia 75% , zaidi ya 2001-3000 unakupa 50% ukinunua dawa 3001-4000 unalipia 25% above 4001 ni free.

Pamoja na yote hizo bima zao hazifanyi coverage kwa meno na miwani.

Pia watoto wote below 12 Yrs bure kila kitu na wazee wote above 65yrs bure kila kitu.

Fanya research yako Tena Bob mushi
 
Ahadi za TL ni sawa na ahadi za mlevi wa Konyagi, kama wameshindwa kujenga hata ofisi ya chama chao wataweza ya kuwajengea Watanzania mahitaji yao? Ruzuku ya 320+ millioni kila mwezi pamoja na michango ya wabunge wao wameshindwa kuwa na ofisi miaka zaidi ya 20 tangu hiki chama kianzishwe na baba mkwe wa mlevi wa konyagi.
KWANI VYAMA VINGINE VILIWAHI KUJIJENGA OFISI?
 
TUSIMWACHE LISU ATUAHIDI YASIYOWEZEKANA.

Na Thadei Ole Mushi.

Kwenye kampeni za Lisu ana Mambo makubwa mawili anayowaomba watanzania wamchague nayo. Moja ni malalamiko yake ya kupigwa risasi hii Kwake Ni Kama Kete ya kuwaomba watanzania wamuonee huruma aingie Ikulu. Jambo la Pili ni Sera zake anazotakiwa awashawishi nazo watanzania ili wamchague kuwa Rais.

Nilishawahi kusema kuwa hakuna siku nitambeza Lisu kwa kupigwa Kwake Risasi na Wala sintoongea nikimuona analalamika kuwa mwili wake una machuma kila Mahali. Kama watanzania wataamua kumchagua kwa kuwa tu aliwahi kushambuliwa na watu wasiojulikana Hilo nimewaachia. Mimi nitajikita kwenye Sera zake ambazo kwangu ndio kipimo Cha kutoa kura yangu kumchagua Kiongozi katika ngazi zote iwe udiwani, Ubunge, au Urais nitazipima Sera kabla ya kuchagua.

Nimesikikiza Sera za mgombea urais Lisu anayo Mambo makuu matatu anayowaahidi watanzania kubwa kabisa ni kila mtanzania kumiki bima ya Afya, kupunguza Makato ya Wanufaika wa Bodi, kuleta maendeleo ya watu badala ya vitu. Haya ndio anayoyarudia kila Mara anaposhika kipaza sauti Leo tuongele moja kesho tutaongele lingine na leo tuanze na Bima ya Afya kwa kila mtanzania.

BIMA BURE

Nimejaribu ku survey nchi nyingi duniani, Ni nchi ipi yenye uwezo wa kuwapa wananchi wake wote Bima BURE sikuona.

Marekani ilijaribu kupitia Obama Care lakini baada ya Muda mfupi walishindwa na Obama care ikafa. Sababu kubwa Ni gharama za uendeshaji. Kutokana na U.S Census Bureau taifa la Marekeni lina watu milioni 28.1 tu ya wasiokuwa na Bima. Hivyo Obama care ilidhamiria kufanya Coverage ya watu milioni 28 tu kuwalipia huduma za Afya lakini wameshindwa kutokana na gharama zake. Hili ni taifa tajiri kuliko yote duniani limeshindwa kuwalipia watu milioni 28 tu je kwa Tanzania wenye Bima hawafikii milioni kumi je milioni Arobaini iliyobakia wanaofanya kazi wataweza kuwalipia gharama hizo?

Sababu nyingine ya wamarekani kukataa Obama care ni kuwa Kama itafanya kazi Kodi ingelipanda sana nchini marekani hivyo wakaamua kuitupilia mbali. Kuna nchi zinazotajwa kuwa na unafuu wa Bima Duniania lakini sio bure naomba kuzitaja:-

1.Ujerumani.

Ujerumani ndio taifa linaloonekana Kama Bima yake angalau Ina unafuu kwa wananchi wake. Lakini pia sio wajerumani wote ambao Wana Bima ya afya. Wafanyakazi wote nchini ujerumani wanalipia Bima zao kwa kushirikiana na waajiri. Wengine waliobakia wanalipia kiasi kidogo Bima zao.

2. Singapore

Singapore wao Wana mfumo wa Bima unaoitwa Medshield ambao serikali kwa asilimia kubwa ndio inabeba gharama za matibabu lakini kila mtu nchini Singapore anatakiwa alipie asilimia 10 ya kipato chako kwenye mfuko huo. Kama ni Mkulima wanakupigia mahesabu asilimia 10 ya unachokipata ulipie kwenye mfuko wa bima, Kama ni mfanyakazi vivyohivyo pamoja na kuwa unaonekaba kuwa mfumo Bora kuliko yote duniani lakini bado unalipiwa na wenye kipato kikubwa bado wanaumia sana kukatwa asilimia 10 kwa ajili ya Bima.

3. Japani

Japani wao Wana mfumo wa Bima unaoitwa SHIS mfumo huu nao watu wanatakiwa kujiandikisha na kulipia.

4. Uingereza.

Wao ndio kwa asilimia kubwa wamefanikiwa kwa kuwa hospital asilimia kubwa zinamilikiwa na serikali na wafanyakazi wote hulipwa na Serikali. Mfumo wao wa Bima wa NHS gharama zake zote hutolewa na Serikali. Ila bado una changamoto na mtu akitaka kutibiwa private ambako Kuna huduma nzuri na za haraka unatakiwa kulipia mwenyewe.

Hizo Zina unafuu Duniania Soma unafuu wake halafu tulinganishe na Tanzania.

Tanzania.

Tuna Bima ya NHIF ambayo huangaika na watumishi wa Umma na wategemezi wao. Huu tunauchangia asilimia Kama mataifa mengine yanavyouchangia. Tena asilimia tatu tu tofauti na mataifa Mengi sana Duniania.

Tuna mfuko mwingine iCHF (Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii ulio Boreshwa), huduma hii ya Bima ni kwa gharama nafuu kabisa kwa Watanzania wote katika Sekta ya Afya kwa Familia ya watu sita yaani Baba, Mama na watoto wanne kwa Tsh. 30,000/- tu kwa mwaka mzima. Una pata huduma zoote za matibabu kuanzia kituo kidogo cha Afya mpaka Hospital ya Mkoa.

Serikali Ina mpango pia wa kuleta Sheria Bungeni ya kuwataka watanzania wote kuingizwa kwenye mfuko wa Bima ya Afya.

Mimi nataka kufahamu Lisu anataka kuifanyaje hiyo Bima yake. Sio kwamba nambeza la hasha nataka kufahamu Bima yake anayoihubiri Ina nini ndani na itakuwa inafanana na ya nchi gani.

Tusimwache Lisu atudanganye Kuna haja ya kuchambua haya yanayoongelewa na wanasiasa. Kesho tutachanbua Sera ya Lisu nyingine.

Hoja yangu CHADEMA naomba muwaeleweshe watanzania hiyo Bima yenu ina package gani?

Ole Mushi
0712702602
Tuanze na yule aliyetuahidi Mill. 50 kila kijiji.
 
TUSIMWACHE LISU ATUAHIDI YASIYOWEZEKANA.

Nimesikikiza Sera za mgombea urais Lisu anayo Mambo makuu matatu anayowaahidi watanzania kubwa kabisa ni kila mtanzania kumiki bima ya Afya,

BIMA BURE

Nimejaribu ku survey nchi nyingi duniani, Ni nchi ipi yenye uwezo wa kuwapa wananchi wake wote Bima BURE sikuona.

Ole Mushi
0712702602
Contradiction; Unaandika kuwa Lisu anasema kila mtanzania kumiliki bima ya Afya; wewe mwenyewe unajiongezea eti BIMA BURE
 
Lissu anatoa ahadi zinazotekelezeka sio zile za milion 50 kila kijiji au laptop kila mwalimu.

Mlet mada ni mpumbavu. Hiyo Marekani aliyotaja hajui kuwa kati ya makampuni tajiri ni yale yanayotoa bima za afya! Hajui fedha za bima huwekezwa kwenye mabenki na kuzaa. Hakui kuwa waougua na kuhitaji matibabu ni sehemu ndogo sana ya watoa michango na ni pesa ndogo sana kutoka pesa ya jumla. Mleta mada hajui kuwa watoa michango nyuma ya pazia ni watu wanaofanya kila bidii ili wasiugue - hivo kufanya michango yao kuhudumia wachache tu!!

Ahadi anazotoa Lissu zinatekelezeka! Kama atashinda au kushindwa, hili ni jambo lingine.
 
Kwani Lissu anakusanya kodi?. Si hata kodi zilizokuwa zinakusanywa na halmashauri zimechukuliwa na serikali kuu, unatarajia afanye nini? Huyu mbunge aliyepo sasa hivi ameshafanya maajabu gani hadi sasa? Umeshatembelea majimbo mengine yaliyo chini ya ccm hapo mkoani Singida na kuona maendeleo yake?


Kazi ya mbunge ni kuwasemea wananchi bungeni matatizo waliyo nayo: toka lissu ameingia kua mbunge sjawahi ona akishuhulikia miradi yoyote na wananchi wake, yeye kazi yake ni kuropoka always
 
TUSIMWACHE LISU ATUAHIDI YASIYOWEZEKANA.

Na Thadei Ole Mushi.

Kwenye kampeni za Lisu ana Mambo makubwa mawili anayowaomba watanzania wamchague nayo. Moja ni malalamiko yake ya kupigwa risasi hii Kwake Ni Kama Kete ya kuwaomba watanzania wamuonee huruma aingie Ikulu. Jambo la Pili ni Sera zake anazotakiwa awashawishi nazo watanzania ili wamchague kuwa Rais.

Nilishawahi kusema kuwa hakuna siku nitambeza Lisu kwa kupigwa Kwake Risasi na Wala sintoongea nikimuona analalamika kuwa mwili wake una machuma kila Mahali. Kama watanzania wataamua kumchagua kwa kuwa tu aliwahi kushambuliwa na watu wasiojulikana Hilo nimewaachia. Mimi nitajikita kwenye Sera zake ambazo kwangu ndio kipimo Cha kutoa kura yangu kumchagua Kiongozi katika ngazi zote iwe udiwani, Ubunge, au Urais nitazipima Sera kabla ya kuchagua.

Nimesikikiza Sera za mgombea urais Lisu anayo Mambo makuu matatu anayowaahidi watanzania kubwa kabisa ni kila mtanzania kumiki bima ya Afya, kupunguza Makato ya Wanufaika wa Bodi, kuleta maendeleo ya watu badala ya vitu. Haya ndio anayoyarudia kila Mara anaposhika kipaza sauti Leo tuongele moja kesho tutaongele lingine na leo tuanze na Bima ya Afya kwa kila mtanzania.

BIMA BURE

Nimejaribu ku survey nchi nyingi duniani, Ni nchi ipi yenye uwezo wa kuwapa wananchi wake wote Bima BURE sikuona.

Marekani ilijaribu kupitia Obama Care lakini baada ya Muda mfupi walishindwa na Obama care ikafa. Sababu kubwa Ni gharama za uendeshaji. Kutokana na U.S Census Bureau taifa la Marekeni lina watu milioni 28.1 tu ya wasiokuwa na Bima. Hivyo Obama care ilidhamiria kufanya Coverage ya watu milioni 28 tu kuwalipia huduma za Afya lakini wameshindwa kutokana na gharama zake. Hili ni taifa tajiri kuliko yote duniani limeshindwa kuwalipia watu milioni 28 tu je kwa Tanzania wenye Bima hawafikii milioni kumi je milioni Arobaini iliyobakia wanaofanya kazi wataweza kuwalipia gharama hizo?

Sababu nyingine ya wamarekani kukataa Obama care ni kuwa Kama itafanya kazi Kodi ingelipanda sana nchini marekani hivyo wakaamua kuitupilia mbali. Kuna nchi zinazotajwa kuwa na unafuu wa Bima Duniania lakini sio bure naomba kuzitaja:-

1.Ujerumani.

Ujerumani ndio taifa linaloonekana Kama Bima yake angalau Ina unafuu kwa wananchi wake. Lakini pia sio wajerumani wote ambao Wana Bima ya afya. Wafanyakazi wote nchini ujerumani wanalipia Bima zao kwa kushirikiana na waajiri. Wengine waliobakia wanalipia kiasi kidogo Bima zao.

2. Singapore

Singapore wao Wana mfumo wa Bima unaoitwa Medshield ambao serikali kwa asilimia kubwa ndio inabeba gharama za matibabu lakini kila mtu nchini Singapore anatakiwa alipie asilimia 10 ya kipato chako kwenye mfuko huo. Kama ni Mkulima wanakupigia mahesabu asilimia 10 ya unachokipata ulipie kwenye mfuko wa bima, Kama ni mfanyakazi vivyohivyo pamoja na kuwa unaonekaba kuwa mfumo Bora kuliko yote duniani lakini bado unalipiwa na wenye kipato kikubwa bado wanaumia sana kukatwa asilimia 10 kwa ajili ya Bima.

3. Japani

Japani wao Wana mfumo wa Bima unaoitwa SHIS mfumo huu nao watu wanatakiwa kujiandikisha na kulipia.

4. Uingereza.

Wao ndio kwa asilimia kubwa wamefanikiwa kwa kuwa hospital asilimia kubwa zinamilikiwa na serikali na wafanyakazi wote hulipwa na Serikali. Mfumo wao wa Bima wa NHS gharama zake zote hutolewa na Serikali. Ila bado una changamoto na mtu akitaka kutibiwa private ambako Kuna huduma nzuri na za haraka unatakiwa kulipia mwenyewe.

Hizo Zina unafuu Duniania Soma unafuu wake halafu tulinganishe na Tanzania.

Tanzania.

Tuna Bima ya NHIF ambayo huangaika na watumishi wa Umma na wategemezi wao. Huu tunauchangia asilimia Kama mataifa mengine yanavyouchangia. Tena asilimia tatu tu tofauti na mataifa Mengi sana Duniania.

Tuna mfuko mwingine iCHF (Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii ulio Boreshwa), huduma hii ya Bima ni kwa gharama nafuu kabisa kwa Watanzania wote katika Sekta ya Afya kwa Familia ya watu sita yaani Baba, Mama na watoto wanne kwa Tsh. 30,000/- tu kwa mwaka mzima. Una pata huduma zoote za matibabu kuanzia kituo kidogo cha Afya mpaka Hospital ya Mkoa.

Serikali Ina mpango pia wa kuleta Sheria Bungeni ya kuwataka watanzania wote kuingizwa kwenye mfuko wa Bima ya Afya.

Mimi nataka kufahamu Lisu anataka kuifanyaje hiyo Bima yake. Sio kwamba nambeza la hasha nataka kufahamu Bima yake anayoihubiri Ina nini ndani na itakuwa inafanana na ya nchi gani.

Tusimwache Lisu atudanganye Kuna haja ya kuchambua haya yanayoongelewa na wanasiasa. Kesho tutachanbua Sera ya Lisu nyingine.

Hoja yangu CHADEMA naomba muwaeleweshe watanzania hiyo Bima yenu ina package gani?

Ole Mushi
0712702602
Hakuna mahali Lissu amesema atatoa Bima ya Afya bure. Amesema atatoa Bima ya Afya kwa kila Mtanzania lakini hajasema atatoa bure

Sent from my vivo 1904 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom