Tuachane na utamaduni wa kubet kwenye kila kitu! Huyo kocha ana familia huko ulaya hivyo kaenda kutazama familia yake na wala si vinginevyo!
Suala la Mkude kuna kitu uongozi umeshakosea toka mwanzo na kumlea akaleleka kama alivyo! Mkude kacheza Simba sasa ni zaidi ya miaka 10, Hivyo ni jambo la ajabu leo akaonekana hana nidhamu wakati anaelekea kuzeekea Simba, isiwe kaanza kuwekewa mizengwe sababu Simba wamempa Thadeo Lwanga.
Kuhusu Morisoni sioni shida ya kuwepo kwake anaweza kucheza kama winga wa kushoto iwapo kocha atamtengenezea combination nzuri au atatengenezewa watu wanaoweza kucheza nae vizuri.
Medie Kagere bado ni bonge la straika hata mahasimu wetu wengi wanammezea, Simba wakirogwa wakamuacha mshambuliaji huyu kwa maneno ya mitandaoni itakuwa kama ilivyokuwa kwa Hamis Tambwe, maaa atadakwa na mahasimu wetu alafu huyohuyo ndio atakuwa silaha ya maangamizi kwa Simba.
Kagere atafutiwe tu formation nzuziri na ajengewe mahusiano mazuri na wenzake ili waendelee kumpa support na pasitokee wa kumuhujumu!