Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,904
Kwa miaka 4 sasa tangu Godbless Lema awe Mbunge wa Arusha, nimekuwa nikivutiwa na hotuba zake, nikimfuatilia na kumjifunza kwa karibu.
Baada ya kumfuatilia nimegundua sababu moja kubwa ya Arusha mjini chini ya Godbless Lema kuwa ngome ya Chadema isiyotikisika na ambayo hata ccm wanajua kuwa hawawezi kushinda mwaka 2015.
CCM wanaweza kufikiri kurudisha jimbo lo lote la Chadema lakini siyo Arusha mjini --- Wanajua Lema atashinda Arusha mjini kwa kishindo 2015.
Dalili za ukweli huo ni kuwa chaguzi zote za marudio za madiwani Arusha mjini Chadema ilishinda kwa kishindo pamoja na ccm kukamia kutaka kushinda. Swali la msingi ninalotaka tulijadili ni kwa nini imekuwa hivyo Arusha mjini?
kwa maoni yangu Sababu kubwa ni moja, Godbless Lema amejua tatizo la watanzania na linalochelewesha mabadiliko ni Woga. Agenda kubwa ya Lema Arusha Mjini tangu mwaka 2010 ambayo imefanikiwa sana ni agenda yake ya kudumu ya kuwapa wanaArusha ujasiri. Lema haamini kama mtu mwoga anaweza kuleta mabadiliko. Hilo jambo utaliona kwenye hoja zake Bungeni, kwenye vikao na kwenye hotuba zake kwa wananchi----- anasisitiza kuacha woga na kuwa na ujasiri.
Godbless Lema anaamini kuwa:
Kumwambia mtu mtanzania mwoga Chagua Chadema ni kazi ya hasara kwa kuwa atachagua Chadema na kura zitaibwa huku watu 20,000 watashindwa kulidna kura zao na kutawanywa na polisi 2 kwa sababu ya woga tu na ccm itashinda kwa wizi.
Lema ana amini kuwa unaweza kutumia mil 500 kuzunguka Tanzania nzima kuhubiri ubaya wa ccm halafu Waziri moja wa ccm ataita vyombo vya habari na kuwatisha watanzania kuwa ukichagua chadema nchi itaingia vitani na watu wote kwa uwoga wao wataichagua ccm hata kama dhamira zao hazitaki ccm.
kwa hiyo, kwa mtazamo wa Kamanda Godbless Lema mahubiri yo yote yasiyokuwa ya kuwabadilisha watanzania kuwa wajasiri na kuacha woga ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Na kwa bahati mbaya sana, ccm wameshajua kuwa watanzania wengi (ukiacha Arusha mjini) ni waoga sana na wanautumia uwoga huo wa watanzania kama mtaji wao, Na ndo maana;
mwaka 1995 waliwaonesha watanzania mauaji ya kimbali ya Burundi na watanzania wakatishika sana,
mwaka 2005, cuf ilipokuwa tatizo siku moja kabla ya siku uchaguzi IGP aliibuka na majambia ya CUF na kuwatisha watanzania - na wakatishika.
Mwaka 2010 walipoona Chadema ya Dr Slaa imekuwa tatizo kubwa zaidi wakaja na vitisho kigogo wa JWTZ na swahiba wa Kikwete,
Adulrahamani Shimbo akawatisha watanzania siku chache kabla ya siku ya Uchaguzi. Dr Slaa alipohoji kama Shimbo alitoa kauli kwa niaba JWTZ au ni kauli yake, hawakumjibu, lakini tayari wameshawatisha wapiga kura na kupunguza kura za wapinzani.
Mwaka 2015 kwa hali ilivyo tutake tusitake, lazima kutakwa na mradi wa kuwatisha watanzania.
Sijawahi kumsikiliza LEMA akitoa hotuba yo yote mahali po pote bila kutaja neno woga. Na amekuwa na kauli mbiu kadhaa zinazozungumzia ubaya wa woga kama vile, Hakuna dhambi kubwa kama dhambi ya woga....... Heri vita ya kutafuta haki kuliko amani inayopumbaza na kuhalilisha utu wa mwanadamu ........ Wakati wa mapambano ukiona wameniua,usilie, kanyaga maiti yangu, songa mbele pigania haki.
Hii ndo siri ya mafanikio ya Chadema Arusha -- wana Arusha hawana uwoga na vitisho vya aina yo yote wala kifo.
Je,ni wabunge na viongozi wangapi wa Chadema wanahubiri ubaya wa woga na kuwatia ujasiri wapiga kura wao??
Binafsi na naamini kuwa mabomu ya Arusha ni mradi wa watawala kuwatisha wana Arusha waachane na Lema na Chadema yake --- wameshidwa vibaya. Wamekufa watu wengi na baada ya vifo hivyo chadema ikashinda kwa kishindo kwenye chaguzi zilizofuata. Wengi hawajui kuwa mabomu yale yangekuwa mahali pengine (siyo Arusha ya Godbless Lema) Chadema ingeshidwa vibaya sana kwa sababu hofu na woga.
Na ifahamike, kila baada ya matukio mashushu wanajazwa mitaani na kuhusisha kila aina ya vurugu hizo na Godbless au Chadema kwa ujumla wake.
Kwa bahati nzuri sana Godbless Lema ameshawajaza ujasiri wana Arusha kiasi kwamba hawaogopi tena kifo kutokana kauli mbiu tajwa hapo juu na nyingine nyingi.
Ni kwa sababu hiyo basi,
Binafsi nimeongoka nimeongoka na nimeamini kuwa tatizo kubwa la watanzania ambalo lazima litatuliwe kwanza kabla ya mengine ni tatizo la Uwoga, mgombea nafasi yo yote wa upinzania asipolitatua tatizo hili kwanza katika eneo lake, anajiandaa kushindwa.
Pili, uchaguzi wa Serikali za mtaa ukianza nachukua likizo nitakwenda kuwajaza ujasiri wana Mbulu hadi wawe kama Arusha mjini.
Huu ndo mwarobaini wa kuiondoa ccm mwaka 2015 kwa sababu hakuna mtanzania asiyejua ubaya wa ccm, tatizo lao ni woga.
Tatu, narudia tena, tusipowajaza watanzania ujasiri mithili ya Godbless Lema hata katiba ya Chenge na Sita italetwa mtaani na watanzania watatishwa na itapita. Wakiweza kuwatisha wabunge, watashindwaje kuwatisha wanachi wa kawaida? Au kama wana ujasiri wa kuiba kura za wabunge kwa kutumia wapambe wa Bunge, watashidwaje kuiba kura za wananchi mtaani kwa kutumia polisi na JWTZ.
Tuondoe kwanza uwoga wa watanzania KWANZA ndipo tufikirie katiba mpya na mradi wa kuiondoa ccm 2015, vinginevyo.............
Nawasilisha.
MICHALE AWEDA.
Baada ya kumfuatilia nimegundua sababu moja kubwa ya Arusha mjini chini ya Godbless Lema kuwa ngome ya Chadema isiyotikisika na ambayo hata ccm wanajua kuwa hawawezi kushinda mwaka 2015.
CCM wanaweza kufikiri kurudisha jimbo lo lote la Chadema lakini siyo Arusha mjini --- Wanajua Lema atashinda Arusha mjini kwa kishindo 2015.
Dalili za ukweli huo ni kuwa chaguzi zote za marudio za madiwani Arusha mjini Chadema ilishinda kwa kishindo pamoja na ccm kukamia kutaka kushinda. Swali la msingi ninalotaka tulijadili ni kwa nini imekuwa hivyo Arusha mjini?
kwa maoni yangu Sababu kubwa ni moja, Godbless Lema amejua tatizo la watanzania na linalochelewesha mabadiliko ni Woga. Agenda kubwa ya Lema Arusha Mjini tangu mwaka 2010 ambayo imefanikiwa sana ni agenda yake ya kudumu ya kuwapa wanaArusha ujasiri. Lema haamini kama mtu mwoga anaweza kuleta mabadiliko. Hilo jambo utaliona kwenye hoja zake Bungeni, kwenye vikao na kwenye hotuba zake kwa wananchi----- anasisitiza kuacha woga na kuwa na ujasiri.
Godbless Lema anaamini kuwa:
Kumwambia mtu mtanzania mwoga Chagua Chadema ni kazi ya hasara kwa kuwa atachagua Chadema na kura zitaibwa huku watu 20,000 watashindwa kulidna kura zao na kutawanywa na polisi 2 kwa sababu ya woga tu na ccm itashinda kwa wizi.
Lema ana amini kuwa unaweza kutumia mil 500 kuzunguka Tanzania nzima kuhubiri ubaya wa ccm halafu Waziri moja wa ccm ataita vyombo vya habari na kuwatisha watanzania kuwa ukichagua chadema nchi itaingia vitani na watu wote kwa uwoga wao wataichagua ccm hata kama dhamira zao hazitaki ccm.
kwa hiyo, kwa mtazamo wa Kamanda Godbless Lema mahubiri yo yote yasiyokuwa ya kuwabadilisha watanzania kuwa wajasiri na kuacha woga ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Na kwa bahati mbaya sana, ccm wameshajua kuwa watanzania wengi (ukiacha Arusha mjini) ni waoga sana na wanautumia uwoga huo wa watanzania kama mtaji wao, Na ndo maana;
mwaka 1995 waliwaonesha watanzania mauaji ya kimbali ya Burundi na watanzania wakatishika sana,
mwaka 2005, cuf ilipokuwa tatizo siku moja kabla ya siku uchaguzi IGP aliibuka na majambia ya CUF na kuwatisha watanzania - na wakatishika.
Mwaka 2010 walipoona Chadema ya Dr Slaa imekuwa tatizo kubwa zaidi wakaja na vitisho kigogo wa JWTZ na swahiba wa Kikwete,
Adulrahamani Shimbo akawatisha watanzania siku chache kabla ya siku ya Uchaguzi. Dr Slaa alipohoji kama Shimbo alitoa kauli kwa niaba JWTZ au ni kauli yake, hawakumjibu, lakini tayari wameshawatisha wapiga kura na kupunguza kura za wapinzani.
Mwaka 2015 kwa hali ilivyo tutake tusitake, lazima kutakwa na mradi wa kuwatisha watanzania.
Sijawahi kumsikiliza LEMA akitoa hotuba yo yote mahali po pote bila kutaja neno woga. Na amekuwa na kauli mbiu kadhaa zinazozungumzia ubaya wa woga kama vile, Hakuna dhambi kubwa kama dhambi ya woga....... Heri vita ya kutafuta haki kuliko amani inayopumbaza na kuhalilisha utu wa mwanadamu ........ Wakati wa mapambano ukiona wameniua,usilie, kanyaga maiti yangu, songa mbele pigania haki.
Hii ndo siri ya mafanikio ya Chadema Arusha -- wana Arusha hawana uwoga na vitisho vya aina yo yote wala kifo.
Je,ni wabunge na viongozi wangapi wa Chadema wanahubiri ubaya wa woga na kuwatia ujasiri wapiga kura wao??
Binafsi na naamini kuwa mabomu ya Arusha ni mradi wa watawala kuwatisha wana Arusha waachane na Lema na Chadema yake --- wameshidwa vibaya. Wamekufa watu wengi na baada ya vifo hivyo chadema ikashinda kwa kishindo kwenye chaguzi zilizofuata. Wengi hawajui kuwa mabomu yale yangekuwa mahali pengine (siyo Arusha ya Godbless Lema) Chadema ingeshidwa vibaya sana kwa sababu hofu na woga.
Na ifahamike, kila baada ya matukio mashushu wanajazwa mitaani na kuhusisha kila aina ya vurugu hizo na Godbless au Chadema kwa ujumla wake.
Kwa bahati nzuri sana Godbless Lema ameshawajaza ujasiri wana Arusha kiasi kwamba hawaogopi tena kifo kutokana kauli mbiu tajwa hapo juu na nyingine nyingi.
Ni kwa sababu hiyo basi,
Binafsi nimeongoka nimeongoka na nimeamini kuwa tatizo kubwa la watanzania ambalo lazima litatuliwe kwanza kabla ya mengine ni tatizo la Uwoga, mgombea nafasi yo yote wa upinzania asipolitatua tatizo hili kwanza katika eneo lake, anajiandaa kushindwa.
Pili, uchaguzi wa Serikali za mtaa ukianza nachukua likizo nitakwenda kuwajaza ujasiri wana Mbulu hadi wawe kama Arusha mjini.
Huu ndo mwarobaini wa kuiondoa ccm mwaka 2015 kwa sababu hakuna mtanzania asiyejua ubaya wa ccm, tatizo lao ni woga.
Tatu, narudia tena, tusipowajaza watanzania ujasiri mithili ya Godbless Lema hata katiba ya Chenge na Sita italetwa mtaani na watanzania watatishwa na itapita. Wakiweza kuwatisha wabunge, watashindwaje kuwatisha wanachi wa kawaida? Au kama wana ujasiri wa kuiba kura za wabunge kwa kutumia wapambe wa Bunge, watashidwaje kuiba kura za wananchi mtaani kwa kutumia polisi na JWTZ.
Tuondoe kwanza uwoga wa watanzania KWANZA ndipo tufikirie katiba mpya na mradi wa kuiondoa ccm 2015, vinginevyo.............
Nawasilisha.
MICHALE AWEDA.