Tusipowakemea hawa wabunge wanaobeza elimu yetu na wasomi wetu, tutazalisha Taifa la hovyo kabisa

Mimi napinga kabisa kwamba usomi ndo unaleta maendeleo, kusoma kote huko sisi watanzania na bado nchi inazidi kuwa maskini tu, mimi najua tupate watu wa kuwajibika na kuleta maarifa, tupate watu wa kujua na kupambana, na mazingira kwenye jamii na kuondoa changamoto zinazowakabili, wananchi. Kwa mfano marekan ilianza kujengwa na watu wakaida kabisa wasio na elimu, na ndo waliiweka kwenye msingi ndo leo!
 
Kweli Dr. Biteko, dk mwigulu
Hizi PhD zonamsaada Gani?

Profesa kabudi katiba mpya haitaki teana
 
Hao wabunge wapo sahihi kwa sababu hao wasomi wengi wao wamedidimiza maendeleo ya hii.Hii inathibitisha usomi hauleti maendeleo bali uzalendo wa mhusika kwenye majukumu yake
 
Form six ana Nini Cha ziada kumzidi darasa la saba mwenye pesa
 
Nani amekuambia Nyererea liendesha nchi kwa mafanikio makubwa? Haujui kama kipindi chake ndio nchi ilitopea kwenye lindi la umasikini
 
Viwanda vilikufa wakati wa Nyerere, nadhani hukuwepo. Yaani ujamaa na azimio la Arusha alishindwa.

Kwa mfano. Sera yake moja ilisema kiongozi asiwe na nyumba za kupangisha. Rafiki zake wengi walikuwa na majumba kariakoo.
 
Kuanzia zama za magufuli wasomi wamedhalaulika sana, ukosefu wa ajira na mambo waliyokua wanayafanya wanasiasa wasomi mfano Pro. Kabudi imesababisha wasomi wote waonekana hamnazo.
Usisahau pia miaka hiyo ya 2005 kurudi nyuma jinsi watu wasiosoma walivyokuwa wakidharaulika kuwa walikimbia umande walioonekana Kama watu wasio na faida kwa taifa hili
 
Tufunge shule zote mtoto akifikia miaka 7 aende kupambana mtaani
 
Usisahau pia miaka hiyo ya 2005 kurudi nyuma jinsi watu wasiosoma walivyokuwa wakidharaulika kuwa walikimbia umande walioonekana Kama watu wasio na faida kwa taifa hili
Yap nyakati zinabadilika mkuu. Hata zamani vipotabo ilikua ndio habari ya mjini walikua wanaita english figure sasa hivi chura ndio mpango mzima.
 
Mafanikio gani?
Uwongo mtupu! Tupo tulioishi nyakati hizo Msingi Mbovu kabisa wa Taifa ukijengwa.
 
Acha uongo unataka kusema benjamin franklin alikua hajasoma
Nchi hii inawajinga wengi ikiwemo wewe
 
Mkuu jaribu kuangalia picha kubwa. Ili msomi aweze kua-apply elimu yake inahitajika awe kwenye taasisi kubwa au ya kati au apate support kubwa sana ya capital, leo hii mchukue msomi aliehitimu uinjia ua udaktari umpe laki moja mwambie a-apply elimu yake we unafikiri atafanya nini? Atafungua phamarcy, ataanzisha hospitali, atafungua ofisi ya architect ya majengo? Haitoshi iyo hela kwaiyo ataishia uko uko tu kwenye mishe za uchuuzi zinazofanywa na hao standard 7, ndipo hapo unakuta msomi akikosa ajira hana ujanja kwa sababu alichosomea kinahitaji capital kubwa ambayo hana. Utawasema madokta wameshindwa kutengeneza hata panado tu lakini unajua gharama za kutengeneza dawa kuanzia utafiti, vifaa, majaribio, vibali mpaka inaruhusiwa kutumika? Jiulize graduates au madokta wetu wataweza kuzimudu?
 
Acha ukweli usemwe. Inakuwaje mtu Anakuwa professor Hana Tija Kwa Taifa

Hata kingereza Hajui.

Mfano Ndalichako waziri...Alifanya nini Kwenye Taifa hili kama waziri wa Elimu

Wako wengi tu. Hawana impact Kwa jamii
Sasa si ndo uelewe kuna some thing behind
 
Acha ukweli usemwe. Inakuwaje mtu Anakuwa professor Hana Tija Kwa Taifa

Hata kingereza Hajui.

Mfano Ndalichako waziri...Alifanya nini Kwenye Taifa hili kama waziri wa Elimu

Wako wengi tu. Hawana impact Kwa jamii
Daah hao wabunge wana tu ponda sana hawajui nini kinatukumba aisee
 
Acha uoga wataje kwa majina unaogopa Nini.

Wale wabunge wanacho taka Elimu yetu iendane na mazingira..

Haiwezekani MTU wa PHD awe mkuu wa wilaya ama mkoa ama mbunge akitoka kwenye wadhifa ama kustaafu wadhifa awe omba omba..ama kiongozi msomi wa Elimu za juu anahamasisha watu wajiajir ikiwa yeye anajiingezea muda wa kustaafu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…