Tusker Challenge Cup Updates

Tusker Challenge Cup Updates

Invisible

JF Admin
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,286
Reaction score
8,380
Leo ilikuwa ni kati ya Mtibwa vs URA na matokeo ni kuwa Mtibwa wamelala kwa mabao 1 - 0.
 
Mtibwa yaanza vibaya kombe Tusker leo
MTIBWA Sugar ya Morogoro leo jioni imeanza vibayao michuano ya kombe la Tusker baada ya kuchapwa bao 1-0 na URA ya Uganda katika pambano lililofanyika uwanja wa zamani wa taifa.

Kazi nzuri iliyofanywa dakika ya 55 na Tonny Mawejje, iliweza kuipa ushindi mtamu timu hiyo iliyotawala pambano hilo.
Katika michuano hiyo, kesho Tusker ya Kenya itaumana na Prisons kwenye mechi ya Kundi B, kabla ya bingwa mtetezi, Yanga kushuka uwanjani keshokutwa dhidi ya URA.

habari toka NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.
 
Leo Prisons ya Mbeya,Tanzania imefungwa 2-0 na Tusker ya Kenya...Timu za Tanzania mhh mbona zinaanza vibaya jamani,jana Mtibwa leo Prisons...Noma kweli
 
TIMU ya soka ya Prisons ya Mbeya jioni hii imeanza vibaya michuano ya kombe la Tusker baada ya kufungwa mabao 2-0 na Tusker ya Kenya katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Mabao ya Tusker yalifungwa na Francis Oduor katika dakika ya 43 na la pili lilifungwa na Oscar Kadenge katika dakika ya 70.

Mchezaji Yona Ndabila wa Prisons alitolewa kwa kadi nyekundu katika dakika ya 51 baada ya kuonyeshwa kwa mara ya pili kadi ya njano.

Michuano hiyo itaendelea kesho kwa mchezo kati ya Yanga na timu ya Mamlaka ya Mapato Uganda (URA).

Habari na NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.


Tatizo la timu zetu liko wapi?
 
Matokeo ya Yanga ,nimesikia wanacheza leo
 
THANKS
Tupe Mfungaji if posible
 
Mpira umekwisha. Yanga 1 - URA 0.

Kesho ni Simba vs Prisons.
 
Yanga 1 URA 0.
Kesho Simba vs Prisons
 
Simba 1 Prisons 0, dk. 28.
Mfungaji Ramadhani 'Redondo'.
 
Dk. 37, Simba 2 Prisons 0....Mgosi katwanga la pili. 🙂
 
Back
Top Bottom