Naandika kwa tahadhari tu.
Toka mwaka 2016 kasi ya watu kujenga vibanda, mabanda na kujazana kandokando ya barabara kufanya biashara na shughuli mbalimbali imekua ikiongezeka kila kukicha na kwa kasi kubwa sana.Vijana wanaitana tu toka vijijini kuja mjini kuanzisha misheni town kwa kuuza bidhaa mahali popote wanapotaka ili kujipatia ridhiki.
Si jambo baya kuwa na vijana wanapambana lakini upambanaji wao sio tu umekuja kuua uwezo wao wa kufikiri kwa kutoainvest au kwa kuivest kiwango kidogo sana cha ujuzi na akili kwenye biashara zao na maisha yao bali pia umepunguza nguvu kazi kwenye uzalishaji,kwa kuwa vijana wanaotandaza nguo barabarani mitaa ya kariakoo, Mbezi, Tandika au miji mingine hawazalishi chochote zaidi ya kua na maisha ya hand to mouth au kuwatumikia watu wanaowapa bidhaa waziuze na serikali haipati chochote kutoka kwao zaidi na zaidi wamekua kikwazo kwenye movement ya magari na bidhaa kwa kuwa sasa magari hayapati nafasi tena ya kupita kwa uhuru na kwa haraka mfano ni barabara ya uhuru toka mnazi mmoja hadi karume,ilala boma pale.
Hoja yangu leo haikua kuangalia faida za watu waliojazana barabarani kwenye miji yetu bali kutoa tahadhari tu juu ya hatari inayoweza kutokea mbele ya safari. Mara kadhaa tumeshuhudia magari yakihama njia na kuparamia watu au makazi.Ni juzi tumeshuhudia Basi likaparamia nyumba kule shinyanga. Je, tutasubiri watu wangapi waparamiwe na lori ili tuanze kuwatoa watu barabarani?.Vipi siku gari likihama njia pale mbezi louis ama pale Ubungo Plaza hakutakuwa na dhahama kweli?
Tumekua wazuri sana wa kuanza mikakati baada ya janga kutokea lakini ni muhimu sana tukaanza kujifunza na kua na fikra za kuzuia tatizo badala ya kila siku kuunda kamati au kua na amsha amsha baada ya tukio.Huku kwetu Njombe na mashambani viongozi wa vijiji hawakazani tu kuhimiza njia za kuzuia moto bali wanaweka msisitizo kwe makatazo ya uchomaji moto ovyo angalau sasa misitu hususani pines zinasurvive.
Nihitimishe kwa kusema moto soko la kariakoo sio tu kuna watu hawatalipwa fidia kwa mali zao kutokuwemo kwenye list ya watu walipoteza kwa kua vibanda vyao na mali kulizunguaka soko havitakua kwenye list ya wapangaji lakini huenda vimeibwa na wahuni kwa kutohifadhiwa sehemu sahihi na kutokua kwenye maeneo sahihi.Hivyo sasa tujifunze namna bora ya kupangilia miji yetu na biashara zetu kwa kuangalia usalama wa watu na biashara zao.
Wakubwa tuambieni sasa
Sheria zetu za mipango miji,sheria za usalama barabarani na sheria ya Barabara na hifadhi ya barabara zilikuja kwa kazi gani?
Greatings from Southern Highland.
Toka mwaka 2016 kasi ya watu kujenga vibanda, mabanda na kujazana kandokando ya barabara kufanya biashara na shughuli mbalimbali imekua ikiongezeka kila kukicha na kwa kasi kubwa sana.Vijana wanaitana tu toka vijijini kuja mjini kuanzisha misheni town kwa kuuza bidhaa mahali popote wanapotaka ili kujipatia ridhiki.
Si jambo baya kuwa na vijana wanapambana lakini upambanaji wao sio tu umekuja kuua uwezo wao wa kufikiri kwa kutoainvest au kwa kuivest kiwango kidogo sana cha ujuzi na akili kwenye biashara zao na maisha yao bali pia umepunguza nguvu kazi kwenye uzalishaji,kwa kuwa vijana wanaotandaza nguo barabarani mitaa ya kariakoo, Mbezi, Tandika au miji mingine hawazalishi chochote zaidi ya kua na maisha ya hand to mouth au kuwatumikia watu wanaowapa bidhaa waziuze na serikali haipati chochote kutoka kwao zaidi na zaidi wamekua kikwazo kwenye movement ya magari na bidhaa kwa kuwa sasa magari hayapati nafasi tena ya kupita kwa uhuru na kwa haraka mfano ni barabara ya uhuru toka mnazi mmoja hadi karume,ilala boma pale.
Hoja yangu leo haikua kuangalia faida za watu waliojazana barabarani kwenye miji yetu bali kutoa tahadhari tu juu ya hatari inayoweza kutokea mbele ya safari. Mara kadhaa tumeshuhudia magari yakihama njia na kuparamia watu au makazi.Ni juzi tumeshuhudia Basi likaparamia nyumba kule shinyanga. Je, tutasubiri watu wangapi waparamiwe na lori ili tuanze kuwatoa watu barabarani?.Vipi siku gari likihama njia pale mbezi louis ama pale Ubungo Plaza hakutakuwa na dhahama kweli?
Tumekua wazuri sana wa kuanza mikakati baada ya janga kutokea lakini ni muhimu sana tukaanza kujifunza na kua na fikra za kuzuia tatizo badala ya kila siku kuunda kamati au kua na amsha amsha baada ya tukio.Huku kwetu Njombe na mashambani viongozi wa vijiji hawakazani tu kuhimiza njia za kuzuia moto bali wanaweka msisitizo kwe makatazo ya uchomaji moto ovyo angalau sasa misitu hususani pines zinasurvive.
Nihitimishe kwa kusema moto soko la kariakoo sio tu kuna watu hawatalipwa fidia kwa mali zao kutokuwemo kwenye list ya watu walipoteza kwa kua vibanda vyao na mali kulizunguaka soko havitakua kwenye list ya wapangaji lakini huenda vimeibwa na wahuni kwa kutohifadhiwa sehemu sahihi na kutokua kwenye maeneo sahihi.Hivyo sasa tujifunze namna bora ya kupangilia miji yetu na biashara zetu kwa kuangalia usalama wa watu na biashara zao.
Wakubwa tuambieni sasa
Sheria zetu za mipango miji,sheria za usalama barabarani na sheria ya Barabara na hifadhi ya barabara zilikuja kwa kazi gani?
Greatings from Southern Highland.