Tutajuta kwa suala linaloendelea Ngorongoro, tutake tusitake

Tutajuta kwa suala linaloendelea Ngorongoro, tutake tusitake

Acha upuuzi wako,wanyama wangekuwa wanaangamizwa kwa Kasi kama unavyosema si wangeshaisha kitambo?

In fact wameongezeka Sana ndio maana ya kuanzishwa bucha za wanyamapori na migogoro ya wanyama kuvamia Mazao ya wananchi.
Fact!
Alikuwa na point ila hapo Kwa wanyama kuisha hadi kubakia tembo 30😂 kaharibu mantiki imepotea!
 
Maasai........ni binadamu na ndugu zetu.....watu pori.....nna hakika wanaingiliana na wa kule kenya.....na anaweza fanya uhalifu tz akakimbilia kenya.....bado najiuliza wakiwafurusha kwa lazima...si watateemkia KE......wakatulie kwanza then ...moto ukipoa warudi...busara, busara, busara...utalii tunautaka....na maasai wawe salama...
 
Tatizo la ujinga wa watanzania kila kitu wanafanya siasa, hasa kwenye mambo ya msingi. Leo CCM wanawaza mambo ya kura za wamasai..na sio urithi wa vitukuu vyetu
 
Mwaka 1960 Ngorongoro Ilikuwa na Tembo zaidi ya 2000! Ila leo hii Tembo waliobaki Ngorongoro ni 30! Moja ya utajiri wa kipekee duniani ni kuwa na wanyama Mwitu kama hawa ambao sisi wabongo tunawachukulia poa sana!

Ila wana thamani kubwa katika ulimwengu huu! Dunia nzima kwa sasa inateigemea zaidi Tanzania kuhusu wanyama pori. Tanzania ndio wenye wanyama wengi tuliobakia duniani. Ila mbali na hilo wanyama wamekuwa wakiangamizwa kwa speed ya kutisha na sisi wenyewe Watanzania na sasa kuna wanyama ambao wapo kwenye Hatari ya kuangamia kabisa katika uso wa dunia.

Wamasai wakihamishwa ngorongoro tutakuwa tumeokoa maisha ya wanyama adimu ulimwenguni. Mwaka 1959 wakati England wanasaini makubaliano na Wamasai Ngorongoro ilikuwa na watu 8000!

Ila hadi sasa ndani ya ngorongoro kuna binadamu wapatao 120000! Tukiendelea na akili za ajabu. baada ya miaka 50 kutoka sasa Ngorongoro itakuwa na Binadamu 1000,000 na tukubali tukatae wajukuu zetu watakuja kuwa wanawaona Twiga na Tembo kwenye Picha na I pad!

Maana kwa akili zetu waTanzania Tembo Wa Ngorongoro hana tumaini tena la kuwa na kizazi chake miaka 30 ijayo!

Ana hekima yoyote ambae anasimama na kuwatetea fisi na chui walio kwenye hatari ya kuangamizwa ulimwenguni kutokana na uharibifu wa binadamu!

By the way Kitenge awe katumwa au hajatumwa, aliloongea lina Faida kwetu na kizazi kijacho! ila kwa sababu Sisi weusi huwa tunaangalia leo hatuangalii kabisa kesho itakuaje, basi mimi najiandaa kurushiwa maneno makali na Kitenge akae chonjo maana binadamu waharibifu wasiofikiria kesho watamuwinda kama digidigi.

**************

Shida Sio uwepo wa Masai Ngorongoro! shida ni Uharibifu unaofanywa na Binadamu Ngorongoro kutokana na Ungezeko la kuzaliana kwao (Masai ni Binadamu).

Kama nilivyosema 1959 kulikuwa na Binadamu 8000, na kulikuwa na Tembo zaidi ya 2000. Leo kuna Binadamu 120000, na tembo wamebaki 30! haya ngoja binadamu wazaliane wafike 1000,000 halafu mje mnipe idadi ya tembo watakaokuwa wamebaki.

LEO HII TUNATOKA NJE KUSAKA MAJANGIRI WANAOUA SIMBA WAKATI MAJANGIRI WAPO NDANI YA NYUMBA HIYO HIYO TUNAYOKAA!

## AKILI ZETU WATANZANIA MMMH!!!
Inauma sana

Ushauri wangu ni binadamu wawaache Wanyama Hapo mbugani. Maana Binadamu si wanyama, hawawezi kuishi na wanyama pamoja mwituni. Watafutiwe maeneo yatakayowafaa wao na mifugo yao, Tanzania ni kubwa sana na maeneo mazuri kwa ufugaji ni mengi sana.
wewe hao tembo wamekusaidia nini

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Wamasai wanakula tembo au? Tembo wanaisha kwa sababu za uwindaji haramu...
Nilikuwa naandika kwenye thread mbalimbali zilizohusu hii scandal kuwa kama wao walihamia pale baada ya kutoka Serengeti how come ngorongoro?, but now kweli wanaondoka.
 
Back
Top Bottom