Tuwatumie wafungwa kutekeleza mpango wa lishe mashuleni wenye matokeo makubwa

Tuwatumie wafungwa kutekeleza mpango wa lishe mashuleni wenye matokeo makubwa

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Joined
Apr 19, 2021
Posts
1,505
Reaction score
4,427
Rais wa JMT, Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan
Waziri wa kilimo, Mhe. Hussein Bashe
na wengine wanaohusika

Ninawapongeza sana viongozi wangu kwa kuwekea mkazo kilimo kiasi cha kilimo kuonekana ni ajira kwa vijana. Mipango na mikakati ya wizara ya kilimo inayobuniwa chini ya waziri Bashe inatoa matumaini kwa vijana kuona kilimo ni fursa. Mpango wa Building a Better Tommorow (BBT) utatengeneza fursa kwa vijana wengi.

Ninaamini kilimo sasa kinatoa kutoa fursa ya mpango wa lishe mashuleni kutekelezwa kwa matokeo makubwa. Kwa kuwa sasa kilimo kinafanyiwa maboresho na mapinduzi makubwa ni muda muafaka maboresho hayo yakasaidie mpango wa lishe na upatikanaji wa chakula mashuleni kupitia nguvu kazi ya wafungwa.

Wafungwa watumike katika kilimo kikubwa. Kwa kuwa ni nguvu kazi itakayotumika bila gharama kubwa itasaidia mpango huu kuwa na matokeo mazuri. Pia, wafungwa wakihusishwa na mpango huu itakuwa ni njia ya kuwajengea uwezo na ujuzi wa kufanya kilimo cha kisasa itakawafaa baada ya mafunzo yao.

Ni matumaini yangu mapendekezo haya yatafika kwa viongozi husika na kuangalia namna ya kuutekeleza kwa namna yoyote inayofaa.
 
Magereza yako wapi na mashamba yako wapi?
 
Ningetamani wewe kusema kua wafungwa pia wapewe posho kutokana na hiyo kazi watakayoifanya. Na hili ni kwa sababu zifuatazo.

1. JapoKua unawaita "nguvukazi isio na gharama", tambua kua wale sio punda, ni binadamu kama mimi na wewe ni vyema na haki wapate chochote kutoka kwenye jasho lao.

2. Unaposema watajifunza ujuzi wa kilimo cha kisasa, kama haumpi chochote kitu, hata akitoka jela, huo mtaji atatolea wapi?

3. Mfungwa hana pensheni, lakini unatoa ushauri atumike mpka achakae, anavokuja kutoka humo ndani je atatoa wapi nguvu ya kujitaftia chakula?

4. Wafungwa wengi wana familia na wategemezi huku uraiani, ambao wanateseka pia na hii hali ngumu ya maisha, ingekua vyema kama hao wategemezi japo wangepata chochote kitu kutoka kwenye nguvu ya ndugu zao walioko ndani.

Tofauti na haya yote, huu ushauri utakua unafki mkubwa usiojali haki za wenzetu walioko ndani. Maana wote hatuna guarantee. Siku yoyote unaweza kujikuta uko utengwani, utalia na kusaga meno io jua itavokupiga huku ukilima ili nguvu zako zitumike kuombea kura na kujinadi kwa watu wasiojua hata bei ya jembe.
 
Back
Top Bottom