Kamgomoli
JF-Expert Member
- May 3, 2018
- 1,896
- 4,058
Baada ya mechi 2 za Yanga na Al hilal nikaona nisubiri mechi ya leo ili nifanye hitimisho km kweli Nabi ana uwezo wa kuiwezesha Yanga kufanya vzr kimataifa au laa. Nisema tu Yanga wasitarajie maajabu yoyote kutoka kwa huyu Profesa aliye-specialize kwenye kushinda mechi za ndani. Hebu tuache rekodi ziongee kwa kutazama mechi za kimataifa ambazo Nabi kaiongoza Yanga.
1.Yanga VS Rivers United 0:1 lose
2.Rivers United VS Yanga 1:0 lose
3.Yanga VS Al hilal 1:1 draw
4.Al hilal VS Yanga 1:0 lose
5.Yanga VS Club Africain 0:0 draw
Next.....??? Mimi Natabiri kipigo.
Mechi za kirafiki kimataifa Yanga Day.
6.Yanga VS Zanaco 1:2 lose
7.Yanga VS Vipers. 0:2 lose
Kati ya mechi saba Nabi kashinda mechi moja tu tena kwa mbinde. Hii ni rekodi mbaya kabisa kwa timu kubwa km Yanga.Mpaka hapo kwanini nisihitimishe kuwa huyu ni profesa wa mechi za ndani pekee?
Jana niliandika uzi kuonya km Yanga watacheza vile walivyocheza dhidi ya Al hilal kwa staili ya polepole( slow),hawatoweza kamwe kumfunga Club Africain. Cha ajabu leo wamecheza vile vile hali iliyofanya kutotengeneza shambulizi lolote la maana kwa dk zote 90.
Yanga wanacheza kwa kueleweka kuanzia kwa Diara hadi katikati ya uwanja. Baada ya hapo kila mtu anaanza kucheza anavyojua. Huoni timu ikicheza kwa mpangilio maalamu. Wakuamua kupiga chenga atapiga, wakuamua kukimbia na mpira atakimbia nao.Wa kupiga juu atapiga. Hapo ndipo nilipohitimisha kwa kusema Nabi hana uwezo wa mechi za kimataifa.
Sisemi afukuzwe ila Yanga waangalie malengo yao. Je malengo ni kuendelea kushinda ligi kuu pekee au wanataka kumfuata mtani wao kule aliko? Kazi ni kwao wenyewe wataamua.
Ni hayo tu kwa sasa.
1.Yanga VS Rivers United 0:1 lose
2.Rivers United VS Yanga 1:0 lose
3.Yanga VS Al hilal 1:1 draw
4.Al hilal VS Yanga 1:0 lose
5.Yanga VS Club Africain 0:0 draw
Next.....??? Mimi Natabiri kipigo.
Mechi za kirafiki kimataifa Yanga Day.
6.Yanga VS Zanaco 1:2 lose
7.Yanga VS Vipers. 0:2 lose
Kati ya mechi saba Nabi kashinda mechi moja tu tena kwa mbinde. Hii ni rekodi mbaya kabisa kwa timu kubwa km Yanga.Mpaka hapo kwanini nisihitimishe kuwa huyu ni profesa wa mechi za ndani pekee?
Jana niliandika uzi kuonya km Yanga watacheza vile walivyocheza dhidi ya Al hilal kwa staili ya polepole( slow),hawatoweza kamwe kumfunga Club Africain. Cha ajabu leo wamecheza vile vile hali iliyofanya kutotengeneza shambulizi lolote la maana kwa dk zote 90.
Yanga wanacheza kwa kueleweka kuanzia kwa Diara hadi katikati ya uwanja. Baada ya hapo kila mtu anaanza kucheza anavyojua. Huoni timu ikicheza kwa mpangilio maalamu. Wakuamua kupiga chenga atapiga, wakuamua kukimbia na mpira atakimbia nao.Wa kupiga juu atapiga. Hapo ndipo nilipohitimisha kwa kusema Nabi hana uwezo wa mechi za kimataifa.
Sisemi afukuzwe ila Yanga waangalie malengo yao. Je malengo ni kuendelea kushinda ligi kuu pekee au wanataka kumfuata mtani wao kule aliko? Kazi ni kwao wenyewe wataamua.
Ni hayo tu kwa sasa.