Naweza sema with full confidence kuwa wewe unajua mpira. Hongera.Ndugu mzabzab hawa tulio nao hata tungewajali vipi hata kama tukisema Kila mtu asafiri na jet yake na kiwango Cha kulipwa ajitajie mwenyewe haitasaidia Kwa sababu uwezo wao umeishia hapo walipofikia ndio maana tumeishia kuwa dalaja la kupandia wenzetu.
Ni uzwazwa uliopindukia kukazana kuingia gharama kubwa kuajiri makocha wenye CV kubwa na wanaolipwa hela nyingi waje wafundishe hapa.
Ni sawa na kununua mitambo mikubwa sana ya kisasa wakati una umeme hafifu alafu mitambo ikianza kusumbua uanze kulaumu mafundimitambo, nakuhakikishia utafukuza na kufukuza as long as hutatatua tatizo la udhaifu wa umeme wako hutatatua tatizo.
Naomba nieleweke siwalaumu wachezaji wetu naamini wanajituma na huenda wanatoa %100 ya uwezo wao but hivyo ndivyo tulivyowaandaa.
Kama tuna nia ya kuleta mabadiliko ya kweli ni lazima tubadilishe namna ya kuwaandaa watu wetu. Na hili linaihitaji wizara pamoja na TFF kukaa pamoja na kupeana majukumu ya namna ya kutengeneza kizazi kipya cha ushindani na weledi.
Ishu ni sisi kushindwa kuanda wachezaji wetu.
Mkakati unataikwa kuwa endelevu sio ujinga wa taifa stars maboresho 🤣🤣🤣 wat a load of nonsense.
Shule zinatakiwa kuwa na qualified coaches ambao watafundisha mpira with the appropriate age category drills. So unafindisha mtoto wa miaka 14 kama unafundi jitu la miaka 26.
Kozi kila leo tunaona zinaendeshwa so makocha wapo so high time hao makocha ndio waende kufundisha huko mashuleni ili sasa tupate wachezaji wenye ubora. Haya na haya mambo ya kuchanguana kwa ajili ni mtoto wa mjomba tuache. Mara sijui mtoto atoe laki tatu ndio achaguliwe hapana