Nimekua nikiangalia mashabiki wa mziki wa kwetu kwa muda mrefu, kuna wanaosema nchi yetu ina mwanamziki bora Afrika nzima!
Nasikitika lakini sina namna nabaki kushangaa tu.
Afrika Magharibi wanatuzidi ktk sehemu zote iwe ni burudani, elimu,Biashara, utamaduni,uigizaji,michezo,comedy nk!
Youssor N'Dor, salif Keita,Sekouba Bambino,Toumane Diabate, Amadou Balake,Coumba Gawlo,Habib Faye,Jimi Mbaye, Gnonas Pedro,Oumoh Sangare,Thione Sekh,Bonkana Maiga,Mbalou Kante na wengine wengi tu ukiwasikiliza unajua wanajua barabara zao, mziki wao unazungumza sehemu ipi barani Afrika wanatokea.
Mziki umechanganywa na Siasa,tamaduni zao,imani zao,asili zao,uelewa wao,ukomavu wao na uzoefu wao!
West Africa wanafahamika sehemu nyingi zaidi ya dunia, wana tuzo zisizo na idadi, wana vipato vikubwa sana kulinganisha na wa kwetu.
Tanzania tumebarikiwa ujuaji mwingi,kujikweza kwingi,kujiona tunastahili kuheshimiwa kuliko wengine,tunahitaji tuonekane tuna pesa nyingi kuliko tulivyo!
Mfano rahisi ni Youssor N'Dor ana utajiri wa usd 145 milioni, lakini sisi hatuelewi hayo tunataka tutambulike tuko juu ya wote.
View attachment 2027940