Tuweke uwanja sawa wa kampeni. Mambo ambayo Dkt. Magufuli na wapambe wake wamefanya yanayokiuka maadili ya Uchaguzi na NEC wako kimya..

Tuweke uwanja sawa wa kampeni. Mambo ambayo Dkt. Magufuli na wapambe wake wamefanya yanayokiuka maadili ya Uchaguzi na NEC wako kimya..

This is...

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
5,050
Reaction score
5,204
Tumemsikia Mkurugenzi wa NEC akitoa tuhuma dhidi ya mgombea urais wa chadema kwamba anakiuka maadili ya uchaguzi, lakini hatujamsikia akiongelea upande wa pili wa Dkt. Magufuli. Sisi kama wananchi tumeshuhudia matendo yanayokiuka maadili ya uchaguzi yanayofanywa na Dkt. Magufuli kwa uchache nitaorodhesha machache:

1. Dkt. Magufuli kutumia hazina ya taifa kutoa fedha za miradi wakati akijua ana hadhi sawa na wagombea wengine,kurubuni wananchi. Hii Ni rushwa ya wazi. NEC mko wapi??

2. Dkt. Magufuli kuwatisha wananchi kuwa hatowaletea miradi ya maendeleo wasipochagua wagombea wa chama chake. Hapa Kuna mambo mawili Dkt. Magufuli amejuaje kwamba atachaguliwa tena, pili hivi ni vitisho na kuligawa taifa. NEC hamuoni?

3. Kassim Majaliwa kufanya kampeni nchi nzima na kutumia rasilimali za serikali wakati yeye si mgombea urais wala si mgombea mwenza. Yeye ni mgombea ubunge wa Ruangwa. NEC mmeziba masikio.

4. Polepole kumuita Lissu katuni, kuiagiza TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI kumuita Lissu katika Kamati ya Maadili. NEC hawaongei hili wala kukemea lakini Mkurugenzi anajinasibu wako huru na hawafanyi kazi kwa shinikizo.

5. Mkurugenzi wa Tume akiwa kama refa anaipigia CCM kampeni waziwazi lakini Tume haichukui hatua zozote.

ONGEZEA MENGINE ILI KUWEKA KUMBUKUMBU SAWA.
 
Je hamjui taratibu za kuwasilisha malalamiko kwa mujibu wa kanuni na taratibu za maadili ya uchaguzi. Pelekeni malalamiko yenu kwenye kamati ya maadili badala ya maneno ya mitandaoni iwapo mna ushahidi (nothing more nothing less)?Haikubaliki kutuhumu tu bila kufuata taratibu pia ni uchochezi na uvunjivu wa maadili. Fullstop.
 
Pamoja kuwa na kikao na wakuu wa vikosi vya jeshi wote, ukawambia amani ya nchi hii wao ndio wanapaswa kuilinda,nao wamesema watakacho amua wananchi ndicho watakacholinda
Jeshi limegawanyika
-12tqsl.jpg
 
Hapa kinachotakiwa ni kupiga kelele kupitia hili jukwaa huru la JF, vinginevyo hao NEC au yeyote hawawezi kuifanya chochote ccm wala kiongozi yeyote aliye upande huo anayevunja kanuni na maadali ya uchaguzi.

Safari bado inasonga japo the day hasn't come but we'll reach.
 
Je hamjui taratibu za kuwasilisha malalamiko kwa mujibu wa kanuni na taratibu za maadili ya uchaguzi. Pelekeni malalamiko yenu kwenye kamati ya maadili badala ya maneno ya mitandaoni iwapo mna ushahidi (nothing more nothing less)?Haikubaliki kutuhumu tu bila kufuata taratibu pia ni uchochezi na uvunjivu wa maadili. Fullstop.
Ccm wamepeka malalamiko au tume ndo mbadala wa CCM?
 
Je hamjui taratibu za kuwasilisha malalamiko kwa mujibu wa kanuni na taratibu za maadili ya uchaguzi. Pelekeni malalamiko yenu kwenye kamati ya maadili badala ya maneno ya mitandaoni iwapo mna ushahidi (nothing more nothing less)?Haikubaliki kutuhumu tu bila kufuata taratibu pia ni uchochezi na uvunjivu wa maadili. Fullstop.
Umekurupuka,moja ya watu wanaoweza kulalamikia mgombea kwa mwenendo wake wa kampeni kwa mujibu wa maadili ya uchaguzi ni Tume yenyewe na ndio maana wameweza kumwita Lissu.
Pili,umetoka usingizini ukaja kupost humu,Je,JPM hajaagiza fedha zitolewe,Polepole hajamtukana Lissu,Majaliwa hapigi kampeni nchi nzima,Mkurugenzi hajaipigia CCM kampeni.?? Kama huna hoja kaa kimya acha ushabiki maandazi.
Tatu, NEC watende haki kwa wote.Pakichacha hapa sote tutaathirika,machafuko hayatachagua chama.
Nne,unapohubiri Amani ,hubiri na haki pia.Hakuna amani pasipo haki.
Tano,sijui unaishi mbuga ipi Tz ambayo hujui kinachoendelea.
Sita,nenda kasome maadili ya uchaguzi ndio ulete porojo za kijinga hapa.
 
Hawezi kukujibu mkuu,hajui wajibu wa tume ni upi kulingana na maadili ya uchaguzi huu.Kwa mujibu wa maadili hayo NEC wenyewe ni walalamikaji pale wanapoona Kuna mwenendo usiofaa
Ccm wamepeka malalamiko au tume ndo mbadala wa CCM?
 
Je hamjui taratibu za kuwasilisha malalamiko kwa mujibu wa kanuni na taratibu za maadili ya uchaguzi. Pelekeni malalamiko yenu kwenye kamati ya maadili badala ya maneno ya mitandaoni iwapo mna ushahidi (nothing more nothing less)?Haikubaliki kutuhumu tu bila kufuata taratibu pia ni uchochezi na uvunjivu wa maadili. Fullstop.
Swali ni kuwa hiki kinachofanywa na ccm na tume (kwa mijibu wa orodha ya matukia ya ukiukaji wa sheria kama ilivyowekwa na mtoa post) ni sahihi kwa mujibu wa sheria na kanuni za uchaguzi? Kama ni sawa kwa nini kiwe makosa kwa upande wa pili?
 
😶😶😶😶😶😶😶😶😶😶🤨🤨🤨🤨🤨
 
Nachojua mimi Ni baba mpumbavu pekee kama stone anayeweza kusifiwa kwa kumnunulia mkewe Iphone X lakini aliacha mwanae akafa kwa kukosa laki moja ya matibabu. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 8[1](a) inasema "Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa (wananchi) WATU sio ustawi wa VITU. Asomaye na afahamu.!
 
Back
Top Bottom