Lanlady
JF-Expert Member
- Feb 27, 2019
- 1,836
- 6,303
Nawasalimu nyote. Natumai mu wazima. Karibuni kwenye kikao cha familia tuimarishe mahusiano yetu.
Kwanza nianze kwa kusema, kwenye maisha yangu mimi binafsi, nimekuwa nikijifunza katika kila jambo ninaloliona au kusikia. Ninaamini kwamba, kila jambo huwa na sababu. Iwe nzuri au mbaya. Lazima tu kuna sababu ya jambo hilo kutokea.
Sasa nimeona katika familia nyingi, wazazi wengi hawajui au hawatambui kwamba vinywa vyao vimebeba baraka au laana kwa watoto wao. Baadhi ya wazazi hudhani kile kiumbe walichokileta duniani kitajiimarisha chenyewe na kujifunza chenyewe au kupokea baraka za moja kwa moja kutoka huko juu. La hasha!
Baraka za watoto ziko katika vinywa vya wazazi wao. Kila neno analotamka mzazi linaumba. Ni mara chache sana kukuta mzazi anamtakia mwanae mema au mabaya halafu yasimkute. Ni nadra sana.
Wengi kadri wanavyotamkiwa na wazazi wao ndivyo inavyokuwa.
Hivyo basi, ndugu mzazi uliye na watoto au mzazi tarajali, jitahidi kadri uwezavyo kuwatamkia watoto wako yaliyo mema. Ondoa kabisa chuki, hasira zinazotokana na msongo wa mawazo kwenye matamshi yako kwa watoto wako.
Nanyi walezi, mnayo fursa ya kusaidia kutoa mawaidha mema kwa watoto wengine mnaowalea. Hasa kwa wale wanaoishi na watoto wasio wa kuwazaa na wazazi wao hawako tena duniani.
Kuna watu wengi sana leo hii wanataabika kwenye safari ya mafanikio; si kwasababu ya matendo au mienendo yao, bali ni kwa sababu ya matamko ya laana kutoka kwa wazazi wao. Wamekosa kabisa muelekeo.
Wazazi wao ndio hasa kikwazo kwao.
Huenda ni kwasababu ya kutofautiana kiimani, mtazamo au mwenendo.
Mwenyezi Mungu atusaidie sana. Ili tuwatamkie watoto wetu baraka. Tuwasaidie kuishi pasipo majuto "kwanini hawa wamekuwa wazazi wangu?, kwanini nimezaliwa katika hii familia? "
Kumbuka haiwezekani mtoto kuchagua aina ya mzazi anayemtaka; bali ni rahisi kwa mzazi kutengeneza aina ya mtoto anayemtaka.
Hakuna mtoto anayechagua jina lake mwenyewe, bali wengi kama sio wote hupewa majina na wazazi/walezi wetu. Hakuna anayechagua kabila, wote tunarithi toka kwa wazazi.
Ndugu mzazi, chagua jina zuri la kumpa mtoto wako!
Asanteni kwa kunisoma!
Kwanza nianze kwa kusema, kwenye maisha yangu mimi binafsi, nimekuwa nikijifunza katika kila jambo ninaloliona au kusikia. Ninaamini kwamba, kila jambo huwa na sababu. Iwe nzuri au mbaya. Lazima tu kuna sababu ya jambo hilo kutokea.
Sasa nimeona katika familia nyingi, wazazi wengi hawajui au hawatambui kwamba vinywa vyao vimebeba baraka au laana kwa watoto wao. Baadhi ya wazazi hudhani kile kiumbe walichokileta duniani kitajiimarisha chenyewe na kujifunza chenyewe au kupokea baraka za moja kwa moja kutoka huko juu. La hasha!
Baraka za watoto ziko katika vinywa vya wazazi wao. Kila neno analotamka mzazi linaumba. Ni mara chache sana kukuta mzazi anamtakia mwanae mema au mabaya halafu yasimkute. Ni nadra sana.
Wengi kadri wanavyotamkiwa na wazazi wao ndivyo inavyokuwa.
Hivyo basi, ndugu mzazi uliye na watoto au mzazi tarajali, jitahidi kadri uwezavyo kuwatamkia watoto wako yaliyo mema. Ondoa kabisa chuki, hasira zinazotokana na msongo wa mawazo kwenye matamshi yako kwa watoto wako.
Nanyi walezi, mnayo fursa ya kusaidia kutoa mawaidha mema kwa watoto wengine mnaowalea. Hasa kwa wale wanaoishi na watoto wasio wa kuwazaa na wazazi wao hawako tena duniani.
Kuna watu wengi sana leo hii wanataabika kwenye safari ya mafanikio; si kwasababu ya matendo au mienendo yao, bali ni kwa sababu ya matamko ya laana kutoka kwa wazazi wao. Wamekosa kabisa muelekeo.
Wazazi wao ndio hasa kikwazo kwao.
Huenda ni kwasababu ya kutofautiana kiimani, mtazamo au mwenendo.
Mwenyezi Mungu atusaidie sana. Ili tuwatamkie watoto wetu baraka. Tuwasaidie kuishi pasipo majuto "kwanini hawa wamekuwa wazazi wangu?, kwanini nimezaliwa katika hii familia? "
Kumbuka haiwezekani mtoto kuchagua aina ya mzazi anayemtaka; bali ni rahisi kwa mzazi kutengeneza aina ya mtoto anayemtaka.
Hakuna mtoto anayechagua jina lake mwenyewe, bali wengi kama sio wote hupewa majina na wazazi/walezi wetu. Hakuna anayechagua kabila, wote tunarithi toka kwa wazazi.
Ndugu mzazi, chagua jina zuri la kumpa mtoto wako!
Asanteni kwa kunisoma!