TV 15 zaibwa hospitalini Njombe. Mkuu wa mkoa azunguka mitaani kuzisaka

TV 15 zaibwa hospitalini Njombe. Mkuu wa mkoa azunguka mitaani kuzisaka

Hapo utakuta asilimia kubwa ya hao watumishi waliokubali kukatwa mshahara ili kufidia hawahusiki na wizi bali ni uonevu tu.
 
Si ajabu tukio la ukwapuaji huo halina RB
 
Wameambiwa wale kwa urefu wa kamba zao. Unategemea nini? Rais hafanyi ziara yoyote ya kushtukiza? Hakemei vikali wizi, rushwa, ufisadi. Angalau ingewapa watu hofu na kupunguza wizi.

Ndio kwanza yeye anawapa vyeo, promotion mafisadi, wezi na wala rushwa, wahuni ndio washauri wake wakuu.
Hii ni Hatari sana
 
Inasikitisha sana, mambo ya serikali ndivyo yalivyo...
 
Ukaguzi huu wakifanya kila idara ya serikali na halmashauri watakuta wizi Kama huu wa vifaa.laptops,tv,nk
 

=======
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka amemuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa huo kuwasimamisha kazi baadhi ya Watumishi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe akiwemo Katibu wa Afya, Watu wa Idara ya manunuzi pamoja na Idara ya TEHAMA ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za wizi wa TV 15 pamoja na kompyuta tatu katika Hospitali hiyo.

Mtaka ametoa maagizo hayo mara baada ya kushtukiza katika Hospitali hiyo baada ya kupata taarifa ya upotevu wa vifaa hivyo vilivyopotea miezi mitano iliyopita huku akimtaka Afisa manunuzi wa Hospitali hiyo Aloyce Kavumika kulipa takribani shilingi milioni.11 kwa ajili ya kununua TV 15 zilizoibwa.

Awali Afisa manunuzi akitoa taarifa ya wizi huo alisema alipata taarifa ya wizi wa TV July 08,2023 akiwa nje ya ofisi ambapo baada ya kurejea ofisini hapo alilazimika kukaa na Watumishi wenzake kwa nyakati tofauti huku wakikubaliana Watumishi wa Idara hiyo kuingia gharama zao kulipa TV hizo.

Amesema baada ya makubaliano hayo walikwenda kwenye moja ya duka la Mfanyabiashara mmoja mjini Njombe na kuagiza TV nyingine ambazo walipewa kwa makubaliano ya kuzilipa baada ya miezi miwili yaani mpaka mwezi huu wa November na waliweza kupewa bila maandishi yoyote kwakuwa wamekuwa wakishirikiana katika shughuli mbalimbali ambapo mpaka sasa fedha hiyo pia bado haijalipwa kwa mwenye duka.
Mkanganyiko mkubwa hapo.

Kwa nini wakubaliane kununua zingine?
 
Tatizo wizi
Kila mahali ni wizi mpaka wanaona cctv ni mfichua maovu kwa hiyo hata wakiziweka ( ambapo nina uhakika hakuna) wataziiba pia au kuzivunja aidha kupoteza ushahidi au hawataki kuumbuka

Nchi imejaa wizi hata unaemlisha anakuibia
Hakuna sehemu hakuna wizi hapa kwenye hii nchi. HAKUNA.

Nchi hii ina watu wa hovyo kupindukia.
 
U

=======
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka amemuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa huo kuwasimamisha kazi baadhi ya Watumishi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe akiwemo Katibu wa Afya, Watu wa Idara ya manunuzi pamoja na Idara ya TEHAMA ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za wizi wa TV 15 pamoja na kompyuta tatu katika Hospitali hiyo.

Mtaka ametoa maagizo hayo mara baada ya kushtukiza katika Hospitali hiyo baada ya kupata taarifa ya upotevu wa vifaa hivyo vilivyopotea miezi mitano iliyopita huku akimtaka Afisa manunuzi wa Hospitali hiyo Aloyce Kavumika kulipa takribani shilingi milioni.11 kwa ajili ya kununua TV 15 zilizoibwa.

Awali Afisa manunuzi akitoa taarifa ya wizi huo alisema alipata taarifa ya wizi wa TV July 08,2023 akiwa nje ya ofisi ambapo baada ya kurejea ofisini hapo alilazimika kukaa na Watumishi wenzake kwa nyakati tofauti huku wakikubaliana Watumishi wa Idara hiyo kuingia gharama zao kulipa TV hizo.

Amesema baada ya makubaliano hayo walikwenda kwenye moja ya duka la Mfanyabiashara mmoja mjini Njombe na kuagiza TV nyingine ambazo walipewa kwa makubaliano ya kuzilipa baada ya miezi miwili yaani mpaka mwezi huu wa November na waliweza kupewa bila maandishi yoyote kwakuwa wamekuwa wakishirikiana katika shughuli mbalimbali ambapo mpaka sasa fedha hiyo pia bado haijalipwa kwa mwenye duka.
Unaibiwa na kuuZIwa
 
Back
Top Bottom