TUPACified
JF-Expert Member
- Feb 27, 2015
- 1,367
- 604
- Thread starter
-
- #41
Yup yup, kuna game BuLi, Pep alianza na Boateng-Benatia-Dante (3 CBs), kati akawa na Rafinha na Bernat (kwenye flanks zaidi), Lahm-Shweini-Xabi katikati, mbele Muller na Lewy. Basically, timu nzima ilikuwa viungoKwa maelezo yaliyotolewa hapo juu. Basically siku hizi timu nzima ni midfielders.
Niliowataja ndio nimepata nafasi ya kuwaona sana bro, watu kama Baraja nilimuona Euro '04 na Spain, Makelele nilimuona msimu mmoja tu Madrid, Silva na Brazil ila nilikuwa siuelewi mpira kivile, so hata uwezo na majukumu yao siwezi kuyaelezea vizuri.
TUPACified ukitaja defensive midfielders bila kuwemo Claude Makelele, Gilberto Silva na Ruben Baraja hiyo listi sio legit!
Ule mpira wa cf anasubiri na kuagiza kama yupo hotelini imeisha siku hizi ndo maana uliona ibra alivyopata tabu na barca waqt etoo alikuwa ana fit penye mfumo
Binafsi nazifahamu hizi
Defensive Mids
Hawa siku hizi wanacheza kama mabeki au mabeki wanacheza kama viungo wakabaji kwa timu zinazomiliki mpira sana. Mabeki viungo wanajulikana kama ball playing defenders (David Luiz, Pique, Ramos etc). Then kuna viungo wakabaji ambao pia huwa wanatumika kama mabeki wa kati kulingana na mchezo unavyokwenda, ila ni viungo (Luiz Gustavo akiwa na Brazil, Busquets, Xabi).
Destroyers
Hawa ni viungo ambao primary role yao ni kuharibu tu, kama Coquelin wa Arsenal, Tiago wa Atleti n.k.
Deep Lying Midfielders
Hawa primary role yao ni kuchezesha team ila kutokea kwenye half yao zaidi, kina Toni Kroos Madrid, Pirlo Juve, Verratti PSG n.k.
Creative/Attacking Midfielders
Simply wazee wa assists, primary role yao ni kufungua ngome za wapinzani na kutoa pasi za mwisho. Iniesta, Gotze, Coutinho n.k.
Box to box Midfielders
Hawa wanafanya kila kitu, wanatakiwa kuwepo popote mpira ulipo. Isco na Modric chini ya Ancelotti, Yaya Toure mara nyingi Man City, Rakitic Barca, Matuidi PSG n.k.
Offensive Midfielders/strikers
Hawa ni washambuliaji ila pia ni wachezeshaji, kina Benzema, Messi at times, Welbeck, Rooney at times n.k.
Unazifahamu aina ngapi?
Huo ni mtazamo wangu tu, ruksa kunisahihisha nilipochemka pia.
Mifumo imebadilika sana maaana saiv namba 9 /CF kushuka chini kukaba jambo la kawaida.
Hakuna tena ma winger vibendera saiv ni Wing Midfielder ama Wing Back yan uwepo kwenye attack pia uwepo wakat wa kudefend..
Na GK wa saiv ndo anaaanzisha mashambuliz mfano Bayern Neur habuti mpira ovyo atakama ameanzisha akakosea attempt inayofatia atafanya tena ivyo ivyo...
Wakati nacheza mpira shule wakati huo nlikuwa nacheza namba 5 ila namba 6 alikuwa anachoka sana. Kwahyo nikawa kama nasaidiana nae. Aisee ukipata washambuliaji wajanja na wenye akili kadi zinakuhusu.
Kwangu mimu kwenye team mtu wa muhimu ni holding midfielder. Huyo akuzubaa au akiwa mzembe mtechezewa mpira mwingi sana