Tyson Fury bingwa mpya wa uzito wa juu Duniani baada ya kumdunda Klitschko

Tyson Fury bingwa mpya wa uzito wa juu Duniani baada ya kumdunda Klitschko

Observer

JF HQ
Joined
Oct 18, 2006
Posts
189
Reaction score
299
Bondia Tyson Fury Kutoka Uingereza usiku huu wa leo 28/11/2015 amefanikiwa kutwaa mataji ya WBA, WBO na IBF katika uzito wa Heavyweight baada ya kumdunda kwa points bondia Wladmir Klitschko wa Ukraine ambaye ana makazi nchini Ujerumani.

Tyson amemaliza rekodi ya Klitschko ya kushinda mapambano 22 mfululizo, mara ya mwisho kwa Klitschko kupoteza pambano ilikuwa ni mwaka 2004.

Majaji walimpa Tyson Fury ushindi wa point 115 -112, 115 - 112, 116 - 111

tyson-fury-wladimir-klitschko_3382773.jpg

wladimir-klitschko-blood-bloodied-tyson-fury_3382777.jpg

fury_kl_3513030b.jpg
 
Lilikuwa pambano kali lenye umakini kwa kila upande!
 
Li Klitschko lina madharau mno, bora limedundwa.
 
Lilikuwa pambano kali lenye umakini kwa kila upande!

Sikutegemea kama Tyson angeshinda, nilikuwa ninaona ni wale wale mabondia wanaochonga sana nje ya uwanja.

Ila jamaa kashinda vita ya maneno na vita ya uwanjani
 
Muingereza amemshinda Vladmir Klitchko kwa points....breaking nine years reign. Kalamba 30 million pounds, kwa madafu zidisha kwa 3,300/
 
Muingereza amemshinda Vladmir Klitchko kwa points....breaking nine years reign. Kalamba 30 million pounds, kwa madafu zidisha kwa 3,300/

sipendi ushindi wa point,ndomana naamin hakuna bondia bora kama tyson,ngumi mvululu kama vyumba maktaba
 
sipendi ushindi wa point,ndomana naamin hakuna bondia bora kama tyson,ngumi mvululu kama vyumba maktaba

mkuu katika ngumi, KO inategemea power punch! Walio katika top ten wote wanahiyo power punch, kwahiyo kusavaiv kwenye ring ni lazima ujue pia kujilinda na hiyo power punch...sasa utascore vipi ushindi! Ni kuwa offensive, ku hit more target , kujilinda mpinzani wako asipate target kuscore points. Aliye hit more punches na ku hit target ndie winner by points. Ni kama ushindi aliopata maywether kwa pacquiao. Maywether hana power punch, pac ana power punch. Kwahiyo maywether aliscore more points kwa ku hit targets na kukimbia kuzuia power punches za pac! Kuna watu pia ni wagumu kuwapiga ko. Mfano holyfield enzi zake. So kuna kipindi ushindi wa points upo valid.
 
Vlad kabugi sana kupoteza kwa mUK, asubiri tambo zao!
 
asiyeshindwa ni Mungu pekee hakuna cha ajabu hapo.
 
klitschko jna alikukua anaonesha kuwa anaenda kupigwa hata body language akiwa dressng room showed alikua na hofu
 
Back
Top Bottom