Uamuzi gani utafanyika mchezaji akikataa kufanyiwa sub?

Dabil

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2021
Posts
6,823
Reaction score
15,293
Wakuu mfano mechi inaendelea kocha akaamua kufanya sub halafu mchezaji akagoma kutoka, kama ni kipindi cha kwanza tunaweza kusema labda baada ya mapunziko atazuiwa kurudi.

Je kama ni kipindi cha pili akagoma kutoka uwanjani itakuwaje? Atachukuliwa kwa nguvu na polisi au itabidi amalize tu mechi.
 
Refa ataendelea na mchezo na hakuna mwenye mamlaka ya kumtoa mchwzaji kwa nguvu baada ya mechi kuisha timu itamalizana na mchezaji wao binafsi
 
Kepa alikuwa fala sana,anayeingia alikuwa kwa ajili ya matuta,walipoingia kwenye matuta Chelsea walifungwa kweli.

Hivi Keppa alikuja kupata adhabu?
Kepa hiyo mechi alishinda mkuu...fuatilia vizuri kaka.......Ila talking point haikuishia tu kepa kukataa kutoka au kushinda mechi Bali Ni jinsi maamuzi ya kumtoa yalivyokaa....Makipa wengi wakitolewa wakati wa upigaji penalty wanahisi kwamba makocha wanaudharau uwezo wao ktk kupangua mikwaju hiyo Tena wanawaonesha watu hadharani.....Makipa wengi hawapendi
 
Namkumbuka middle mchezaji wa misri amewahi mgomea kocha wao shekhhatta kipindi Cha mataifa huru ya Africa kwa SAS afcon
Mido hakugoma ila alileta ubishi ila alitoka kisha sub aliingia Amr zaki dakika ya 78 na akafunga baada ya kuingia tu, ilikua mechi ya Misri vs Sengal,Misri alishinda 2-1

Ilikua mwaka 2006 hiyo.
 
Ukigoma ndo hutoki tena akuna wa kukufanya kitu kwa muda huo.

salama yako ufunge goli mechi iishe 1-0 kwa goli ulilofunga wewe,hapo sasa uwenda ukapunguza hasira za kocha.
 

hakushinda walichwapwa kwenye penalties na Man city
 
Ukimgomea furguson su mourinho kesho yake tu anakuuza
 
Mtaani kwetu magomeni ilikua ukikataa kutoka nje wenzako wanakutangazia kua wewe ni "Nyama", kwamba popote utakapogusa mpira basi upigwe viatu. (Ukatwe).
 
Mtaani kwetu magomeni ilikua ukikataa kutoka nje wenzako wanakutangazia kua wewe ni "Nyama", kwamba popote utakapogusa mpira basi upigwe viatu. (Ukatwe).
Hii ninoma asee timu yako inakutangaza kwawapinzan huyu nyama yan utapigwa buti hadi zambavu nahata ndugu yako watimu moja ruksa kukuchezea rafu
 
Itawachukua miaka mingi sana Egypt kupata timu kama hii ya kina Zaki
Essam El Hadary ,Amri Zaki, Mohamed Aboutrika, Emad Moteab, Ahmed Hossam Mido, Mohamed Zidan, Mohamed Shawky, Mohamed Barakat, Ahmed Fathy....hiki kizazi kilikua balaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…