Uamuzi wa Uingereza kuipiga marufuku kampuni ya Huawei ni hasara kwa Uingereza na maendeleo ya teknolojia ya huduma ya 5G

Uamuzi wa Uingereza kuipiga marufuku kampuni ya Huawei ni hasara kwa Uingereza na maendeleo ya teknolojia ya huduma ya 5G

Yoyo Zhou

Senior Member
Joined
Jun 16, 2020
Posts
126
Reaction score
215
Serikali ya Uingereza imetangaza kuwa kuanzia tarehe 31 Desemba mwaka huu, kununua vifaa vya teknolojia ya 5G kutapigwa marufuku, na vifaa vyote vya kampuni ya Huawei vya teknolojia ya 5G vitaondolewa nchini Uingereza kabla ya mwisho wa mwaka 2027. Hatua hii inaonyesha kuwa Uingereza imesujudu kwa shinikizo la Marekani, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitaka nchi hiyo iache kushirikiana na kampuni ya Huawei.

Marekani imekuwa ikiiandama kampuni ya Huawei hasa kutokana na kuwa kampuni hiyo imekuwa na nafasi nzuri ya ushindani kwenye soko la maendeleo ya teknolojia za kidigitali duniani, na kuwa na mbele ya Marekani. Hofu kubwa ya Marekani dhidi ya kampuni hiyo ni kwamba itachukua nafasi yake ya uongozi dunia kwenye mambo ya digitali.

Marekani imekuwa inatumia kisingizio kuwa China inaitumia kampuni ya Huawei kufanya shughuli za kijasusi, na kutumia kisingizio hicho kuzishawishi nchi mbalimbali duniani na hata kuzitishia kuzichukulia hatua nchi zitakazoshirikiana na China kwenye teknolojia ya 5G. Lakini mara kwa mara imethibitishwa na watalaamu wa maswala ya usalama wa kimtandao kuwa kampuni ya Huawei haijishughulishi na maswala ya ujasusi, ni kampuni ya mambo ya kidigitali kama ilivyo kwa makampuni mengine.

Tukiangalia kwa undani tunaweza kujua kuwa tukio hili si jipya, ni tukio linalojirudia duniani likiishirikisha Marekani kwa mara nyingine. Huko nyuma kampuni ya umeme ya Ufaransa Alstom iliyokuwa kampuni kubwa na ya muhimu kwa nchi hiyo, ililazimishwa kutoa fidia ya dola za kimarekani milioni 700, na kuuza asilimia 70 ya hisa zake zote kwa kampuni ya General Electric, iliyokuwa mshindani wake mkubwa nchini Marekani.

Kilichotajwa ni kuwa mkuu wa kampuni hiyo Bw Frederic Pierucci alifanya makosa nchini Indonesia yaliyokwenda kinyume na sheria ya Marekani ya ufisadi wa makampuni nje ya nchi iliyopitishwa mwaka 1977, ambayo kampuni yoyote yenye shughuli zake Marekani inaweza kuchukuliwa hatua kama ikifanya makosa nje ya Marekani. Sheria hiyo imeyakumba makampuni zaidi ya 29, lakini kati ya hayo 15 ni ya Ulaya, 6 ni ya Marekani na 8 ni kutoka sehemu nyingine tofauti tofauti.

Mazingira ya kufikilisiwa kwa kampuni ya Alstom ya Ufaransa, kimsingi yalikuwa yanalenga kuilinda kampuni ya General Electric ambayo licha ya kuwa mshindani wake aliondolewa sokoni, bali pia iliongezewa mtaji wa asilimia 70 ya hisa kutoka kwa kampuni ya Alstorm.

Tunachokiona kwenye mvutano kati ya kampuni ya Huawei na Marekani, hakina tofauti na mambo yaliyotokea huko nyuma. Kukamatwa nchini Canada kwa ofisa mkuu wa kampuni ya Huawei anayeshughulikia mambo ya fedha Bibi Meng Wenzhou, hakukutajwa kuwa ni sababu za kijasusi bali ni za “uhalifu wa kifedha”, lakini kulionyesha wazi kuwa Marekani inaisakama kampuni hiyo na kutaka kuiondoa kwenye ushindani kwenye sekta ya mambo ya digitali.

Kwa sasa wakati inaonekana kuwa Uingereza ambayo mwanzo ilifanya uamuzi wa kujitegemea bila kuingiliwa na Marekani, imeamua kufuata nia ya serikali ya Marekani na kupuuza maslahi ya watu wake na maendeleo ya 5G.
 
Kila Taifa linafanya maamuzi kwa kuangalia maslahi yake kwanza,kama uamuzi waliochukua hautakuwa na tija kisha athari zake kuonekana haitakuwa mwisho wa dunia.Watarudi kukaa mezani na kulitatua kidiplomasia na kibiashara,kama yalivyo mengi (yaliyokwisha tatuliwa sasa na hapo nyuma)
 
USA ni majambazi wa biashara wao wanapohisi kuzidiwa badala waongeze juhudi na ubunifu wanaanza faulo kwa mpinzani wao.
Umetoa mfano wa Alstom ila pia walifanya kwa Airbus kuilinda Boeing ila pia wanafanya kwa Nord Stream 1 na 2 kulinda soko la gesi yao ulaya kwa kuiwekea vikwazo kampuni inayomiliki zile meli za kutandaza mambomba baharini. Sema hapa wameshindwa kwa kuwa Ulaya hasa Germany ambae ndo mteja mkubwa wa gesi ya Urusi hakuwaunga mkono ila pia shirika la gesi la Urusi wana meli yao inayoweza kumaliza task iliyobaki
 
USA ni majambazi wa biashara wao wanapohisi kuzidiwa badala waongeze juhudi na ubunifu wanaanza faulo kwa mpinzani wao.
Umetoa mfano wa Alstom ila pia walifanya kwa Airbus kuilinda Boeing ila pia wanafanya kwa Nord Stream 1 na 2 kulinda soko la gesi yao ulaya kwa kuiwekea vikwazo kampuni inayomiliki zile meli za kutandaza mambomba baharini. Sema hapa wameshindwa kwa kuwa Ulaya hasa Germany ambae ndo mteja mkubwa wa gesi ya Urusi hakuwaunga mkono ila pia shirika la gesi la Urusi wana meli yao inayoweza kumaliza task iliyobaki
China ana ubunifu gani zaidi ya wizi?
 
China ana ubunifu gani zaidi ya wizi?

BUSH BIN LADEN ametoa mifano ahi wa kuonyesha umafia wa ma YANKEE (Gringos) si kwa Uchina tu bali kwa Urusi, Ufaransa na Ujerumani - binadamu gani anawagehuka hata rafiki wake wa karibu, anawakumbuka tu anapotaka kuvamia/pigana vita na Banana Republics, mfano: Iraq,Afghanistani, Syria walitaka kuivamia Venezuela wakagwaya kutoka na uwepo wa Urusi na Uchina.

Mwaka jana nilimuona kwenye luninga a former Alstrom CEO, mfaransa huyo ingawa hivi sasa amezeeka sana lakini alikuwa anatahadhalisha Dunia hasa kampuni za Uchina kwamba Amerika ni Taifa ambalo halitaki kabisa ushindani wa biashara kwa maneno mengine hawataki Makampuni ya USA kuzidiwa kete na Mataifa mengine wapo radhi hata to kill rivals ili wakidhi matakwa yao - hiki ndicho kinaendelea baina ya kampuni ya Huawei na Serikali ya Trump, kampuni ya Gasprom (Urusi) na Serikali ya Trump, Amerika iliwahi kutaka kuingilia Kampuni ya Urusi inayo zalisha products za Aluminium kwa wingi Duniani, walitaka eti Managing Director wake abadirishwe - akili gani hizi?

Mwisho nimalizie kwa kusema kwamba wewe unahoji eti "China ina ubunifu gani zaidi ya wizi!!"" unarudia propaganda zile zile za media za magharibi - unacho sahau ni kwamba masuala ya teknolijia to put into practice principles za physics, hakuna physics za Kichina,Kimerikana wala Urusi,vyuo vikuu vyote Duniani ufundisha kanuni zile zile tofauti ni lugha tu, sasa nikiona watu na akili zao timamu wanawasema vibaya wachina as if hawana akili za kujiendeleza kiteknolojia nawashangaa sana, Amerika unikumbusha imani ya Wamasai kwamba Ngombe wote Duniani belogs to them au mwanangu aliye wahi kuniambia kwamba magari yote Duniani ni TOYOTA i.e hakuna kampuni yoyote yenye uwezo wa kuunda magari zasidi ya Toyota, baadhi ya members wa JF wana amini the World is Amerika uwambii kitu wakakusikiliza. Eti: Wachina wezi! Mbona Wachina wana teknolijia ya mawasiliano ya kisasa kabisa(5G) ambayo USA hawana kabisa au unataka kusema Wachina wanaiba teknolojia ambayo USA hawana - hivi hii inaingia akili kweli? Vile vile Wachina wana latest Hypersonic missiles kitu ambacho USA hawana, mbona hayo hamuyasemi - mnakazania Wachina wezi,wezi - kisa? Wamerika wamesema hivyo, yaani mnachukulia madai ya US dhidi ya Taifa la Uchina as if madai hayo ni Gospel truth.
 
China ana ubunifu gani zaidi ya wizi?

Kuna watu hapa wanaitetea sana China ila wajue mchina ni mwizi mkubwa sana. Sijakataa Huawei ni the best ila kaiba technology halafu kampuni hii inaiba siri za Marekani na nchi nyingine na kuipa serikali ya china. Hata kama ni mm siwezi kukuvumilia lazima nikuweekee zengwe
 
Kuna watu hapa wanaitetea sana China ila wajue mchina ni mwizi mkubwa sana. Sijakataa Huawei ni the best ila kaiba technology halafu kampuni hii inaiba siri za Marekani na nchi nyingine na kuipa serikali ya china. Hata kama ni mm siwezi kukuvumilia lazima nikuweekee zengwe
5G kaina wapi nakwanani ?!
wakat hata hao US hawana ?!


Kuhusiana na kuiba siri za US mbna hata US anaiba na Alishaiba.....
 
Kuna watu hapa wanaitetea sana China ila wajue mchina ni mwizi mkubwa sana. Sijakataa Huawei ni the best ila kaiba technology halafu kampuni hii inaiba siri za Marekani na nchi nyingine na kuipa serikali ya china. Hata kama ni mm siwezi kukuvumilia lazima nikuweekee zengwe
Kuhusu Huawei kuwapa serikali siri za wateja, unajua kwanini Edward Snowden yuko uhamishoni?
 
Serikali ya China inabidi ibadili tabia kama inataka kufanya biashara West.

Kwanza imekuwa ikisapoti wizi wa intellectual properties unaofanywa kupitia hacking, swala ambalo wamelalamikiwa sana bila ya kuchukua hatua.

Halafu kuna katiba yao ambayo inalazimisha kila mwananchi na kampuni zote za kichina kusaidia serikali kwenye maswala ya National security itakapoitajika kufanya ivyo.

Hayo maswala mawili yamechangia.

Dili ya Huawei ilikuwa very complicated iliyopelekea kampuni kutoa mpaka access kwa ya serikali UK kuangalia kama kuna loopholes za system (whatever that means in electronic engineering) ambazo zinaweza tumiwa kupata info za watumiaji. Iko ndio kilikuwa kigezo cha kuwapa kibali cha kufanya biashara UK.

Kilichovunja dili kabisa ni janga la COVID 19 serikali ya China ilivyo behave; usiri kwenye kitu sensitive kilichopelekea kuaribu uchumi wa West.

Now these ppl operate on trust and predictable behaviour of their partners. Wachina awajajifunza hilo, leo serikali yao inasema aitawalazimisha Hauwei kushirikiana nao kitu ambacho kimesaidia kampuni kupata biashara ingawa katiba yao inasema vingine, however through COVID waingereza wamepata somo you can’t trust the behaviour of the Chinese government kwa sababu ata kupitia WHO kwenye afya watu wanatakiwa kushirikiana they dint do that to protect their interest and the whole thing became so costly to the rest of the world.

Kwa ivyo kuwafukuza Huawei sio swala walilokurupuka January tu Boris Johnson alikuwa upande wa Huawei na pressure ilikuwa ndogo, six month later pressure ya kuvunja mkataba imekuwa kubwa kutoka kwa wabunge wa conservative na wameazimia serikali isipovunja mkataba wao awata support bill ikienda bungeni kwa ivyo PM amebanwa.

Yes kuna US influence pia ambazo zimechangia but for the most it’s the Chinese government behaviour which UK feared the most na kupitia COVID wamepewa somo don’t trust the chinese.
 
Kuna watu hapa wanaitetea sana China ila wajue mchina ni mwizi mkubwa sana. Sijakataa Huawei ni the best ila kaiba technology halafu kampuni hii inaiba siri za Marekani na nchi nyingine na kuipa serikali ya china. Hata kama ni mm siwezi kukuvumilia lazima nikuweekee zengwe

Someni historia ya uvumbuzi wa kisayansi Duniani kabla hamjawazulia Wachina.

FYI, Wachina ndio binadamu wa kwanza Duniani kuzalisha karatasi, wa kwanza kuzalisha wino,manual dublicating machine, mathematic calculator (Abacus) wengine wanasema ndio computa ya kwanza duniani ambayo haitumii umeme, gunpowder, roketi na viberiti, kalamu, nguo za silki, sahani za udongo,chai, compass, magnet, NAVY ya kwanza ilikuja mpaka Afrika inasemekana walikwenda mpaka kwenye kontinenti la Amerika kabla ya Columbus, elimu ya Nyota nk - je, nchi za magharibi zili copy mangapi kutoka Uchina - mengi tu, mbona wachina hawaja wahi kudai malipo ya intellectual property kutoka wazungu wezi wa uvumbuzi wa tekinolojia ya Kichina hata kama ilikuwa ya enzi za stone age bado pioneers ni Wachina sio wazungu, kumbukeni hilo kwanza kabla hamujatuletea Mickey Mouse stories - wachina wezi, wachina wezi - hivi Dunia inaweza kushindana na Oriental race yenye binadamu wenye IQ kubwa kuliko races zote Duniani - wanao wabeza Wachina hawajui ukweli huu, tunap juwa ukweli huo atushangai China kuikosesha usingizi America, Wachina si watu wa kuchukuliwa kimzaa mzaa hata kidogo.
 
Serikali ya Uingereza imetangaza kuwa kuanzia tarehe 31 Desemba mwaka huu, kununua vifaa vya teknolojia ya 5G kutapigwa marufuku, na vifaa vyote vya kampuni ya Huawei vya teknolojia ya 5G vitaondolewa nchini Uingereza kabla ya mwisho wa mwaka 2027. Hatua hii inaonyesha kuwa Uingereza imesujudu kwa shinikizo la Marekani, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitaka nchi hiyo iache kushirikiana na kampuni ya Huawei.

Marekani imekuwa ikiiandama kampuni ya Huawei hasa kutokana na kuwa kampuni hiyo imekuwa na nafasi nzuri ya ushindani kwenye soko la maendeleo ya teknolojia za kidigitali duniani, na kuwa na mbele ya Marekani. Hofu kubwa ya Marekani dhidi ya kampuni hiyo ni kwamba itachukua nafasi yake ya uongozi dunia kwenye mambo ya digitali.

Marekani imekuwa inatumia kisingizio kuwa China inaitumia kampuni ya Huawei kufanya shughuli za kijasusi, na kutumia kisingizio hicho kuzishawishi nchi mbalimbali duniani na hata kuzitishia kuzichukulia hatua nchi zitakazoshirikiana na China kwenye teknolojia ya 5G. Lakini mara kwa mara imethibitishwa na watalaamu wa maswala ya usalama wa kimtandao kuwa kampuni ya Huawei haijishughulishi na maswala ya ujasusi, ni kampuni ya mambo ya kidigitali kama ilivyo kwa makampuni mengine.

Tukiangalia kwa undani tunaweza kujua kuwa tukio hili si jipya, ni tukio linalojirudia duniani likiishirikisha Marekani kwa mara nyingine. Huko nyuma kampuni ya umeme ya Ufaransa Alstom iliyokuwa kampuni kubwa na ya muhimu kwa nchi hiyo, ililazimishwa kutoa fidia ya dola za kimarekani milioni 700, na kuuza asilimia 70 ya hisa zake zote kwa kampuni ya General Electric, iliyokuwa mshindani wake mkubwa nchini Marekani.

Kilichotajwa ni kuwa mkuu wa kampuni hiyo Bw Frederic Pierucci alifanya makosa nchini Indonesia yaliyokwenda kinyume na sheria ya Marekani ya ufisadi wa makampuni nje ya nchi iliyopitishwa mwaka 1977, ambayo kampuni yoyote yenye shughuli zake Marekani inaweza kuchukuliwa hatua kama ikifanya makosa nje ya Marekani. Sheria hiyo imeyakumba makampuni zaidi ya 29, lakini kati ya hayo 15 ni ya Ulaya, 6 ni ya Marekani na 8 ni kutoka sehemu nyingine tofauti tofauti.

Mazingira ya kufikilisiwa kwa kampuni ya Alstom ya Ufaransa, kimsingi yalikuwa yanalenga kuilinda kampuni ya General Electric ambayo licha ya kuwa mshindani wake aliondolewa sokoni, bali pia iliongezewa mtaji wa asilimia 70 ya hisa kutoka kwa kampuni ya Alstorm.

Tunachokiona kwenye mvutano kati ya kampuni ya Huawei na Marekani, hakina tofauti na mambo yaliyotokea huko nyuma. Kukamatwa nchini Canada kwa ofisa mkuu wa kampuni ya Huawei anayeshughulikia mambo ya fedha Bibi Meng Wenzhou, hakukutajwa kuwa ni sababu za kijasusi bali ni za “uhalifu wa kifedha”, lakini kulionyesha wazi kuwa Marekani inaisakama kampuni hiyo na kutaka kuiondoa kwenye ushindani kwenye sekta ya mambo ya digitali.

Kwa sasa wakati inaonekana kuwa Uingereza ambayo mwanzo ilifanya uamuzi wa kujitegemea bila kuingiliwa na Marekani, imeamua kufuata nia ya serikali ya Marekani na kupuuza maslahi ya watu wake na maendeleo ya 5G.
Kwani lazima wanunue mitambo ya 5G toka Huawei?
 
Back
Top Bottom