Cha kushangaza hao viongozi wote wa CCM karibia wote wake zao ni machotora na watoto wa ni machotora.
Au wakikosa machotara viongozi wa CCM watachukua wake wenye kutumia mkorogo wa nguvu walau wake zao wafanane na machotara.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Cha kushangaza hao viongozi wote wa CCM karibia wote wake zao ni machotora na watoto wa ni machotora.
Sheikh Mohamed hii sasa ndio karata yao ya mwisho baada ya umma wa Kizanzibari kuamua kuikacha ccm kila siku zikienda. Lakini strategy hii ndio kama wanajichimbia kaburi lao...kufutika kabisa kabisa katika historia. Cha pili kilichobaki ni ulinzi haramu wanao pewa na Muungano.![]()
Vijana wa Chama cha Mapinduzi CCM wakipita mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akipokea matembezi ya Vijana hao waliotembea katika Mikoa Minee ya Kichama katika kuadhimisha miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyomalizia leo katika viwanja vya maisara Suleiman Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]
Picha hiyo hapo juu ni bango la Kikaburu katika mwaka wa 2016 bango linalotukuza ubaguzi wa rangi.
![]()
Sitaki kuamini kama Ali Mohamed Sheni na uongozi wa juu wa CCM Zanzibar wamewatuma vijana hawa kufanya haya.
Akili yangu inanikatalia kabisa.
Sitaki kuamini kuwa tumeanza kuwatengeza akina Hendrik Verwoerd na Eugene Terre Blanche weusi katika visiwa vya Zanzibar.
CCM Zanzibar inamuiga nani katika hili?
Hitler na Manazi walikuwa na vijana wao waliojulikana kama Stormtroopers ukipenda waite Brown Shirts?
Zanzibar tumeshawashuhudia Ton Ton Macout mfano wa wale wa Papa Doc wa Haiti visiwani wanajulikana kama Mazombie.
Sasa tumefungua ukurasa mwingine wa Adolf Eichman.
Hilo bango mbona litawagusa wengi katika safu ya uongozi wa siasa katika Zanzibar na wengine walipatapo hata kuiongoza nchi?
Machotara?
Nani huyu chotara?
Tumehama kwa Waarabu sasa tuko kwa Machotara!
Lakini huyo chotara si ana wajomba, babu, bibi na mama wakubwa na wadogo Waafrika?
CCM imefilisika kiasi hiki?
Nini hiki ni kiwewe cha CCM kushindwa uchaguzi au ni kitu gani?
Nini khasa tafsiri ya mambo haya?
Tusubiri In Sha Allah wakati utatupa jibu.
Kasema Mwalimu Nyerere karne ya ishirini na moja kuna watu wanapanda basi la ukabila...
Hawa wanapanda jahazi la ugozi.
Cha kushangaza hao viongozi wote wa CCM karibia wote wake zao ni machotora na watoto wa ni machotora.
Naona hiyo petrol itakuripukia mwenyewe. Ikiwa unasema raisi wa JMT hana uwezo na jukumu la kutatua mgogoro wa sehemu ya nchi yake lakini anaweza kutatua mgogoro wa Burundi. Siwezi kukusomaKila mtu anamtaka Rais Magufuli aingilie kati. Hana ubavu huo. Someni katiba ya Zanzibar. Hata kichama, mwenyekiti wa ccm ndiye mwenye mamlaka. tusihamishe magoli. Magufuli hahusiki kabisa ktk mgogoro huu huu wa kisiasa. Wajibu wake ni kuhakikisha amani na utulivu vinatamalaki.
Ni kweli Zanzibar imepasuka katikati na kwa misingi ya ubaguzi. Wote tumelipalilia na kulikuza. Kwa mfano, mantiki ya kuendelea kuwa na baraza la mapinduzi ni nini miaka 50 na ushee. Pia watu gani wanahodhi uchumi wa Zanzibar. Mwenye kutawala uchumi ndiye atakayetawala siasa. Katika hili huenda ccm wakaisoma namba. Nguvu ya kiuchumi ya cuf inakua kila kukicha na wamepanua matawi ya kiuchumi hadi bara. Tatizo siyo Shein au maalim Seif bali msukumo wa mwenye nguvu ya uchumi kutaka ahodhi siasa pia. Kwa Zanzibar kufanya hivyo kunasababisha mpasuko wenye kuleta sura ya kibaguzi.
Kama machotara wanatengwa basi ni wakati mzuri wa kuwaoa na kuwaleta bara. Hawatakuwa na nyodo tena, twendeni tukaoe hao machotara.
Ungazija wa babu ndio ulioponza mbele ya wabaguzi ccm.I am shocked... mwili umetawaliwa na hofu. In those old days watu tuliamini ASP hardliners ndo tatizo la msingi... hawa wamebaki kwa kiasi gani? Au wamepandikiza mbegu za chuki kwa watoto na wajukuu zao?!
Naiona CUF ikizidi kupata nguvu maradufu ya ile ya October 2015. Lililo wazi kwa sasa kule Zanzibar ni kwamba, hivi sasa CUF wanapata uungwaji mkono mkubwa sana katika harakati zao za kutaka Zanzibar yenye mamlaka kamili! Tofauti na zamani, hivi sasa wanapata uungwaji mkono hata kutoka kwa CCM Insiders... tofauti yao ni kwamba, CUF wanapigana hadharani na hawa CCM Insiders wanapigana chini kwa chini!
Trust me, hapo wala hawawalengi wana CUF bali zaidi ni "Machotara" wa CCM yenyewe! Watu kama akina SAS hawajawahi kukubalika na ASP/CCM Hardliners hadi kesho! Hata kama wameingiza suala la Hizbu hapo lakini hadi akina Karume hapo wanahusishwa! Yaani ASP/CCM Hardliners hata Mohammed Babu nae walikuwa wanamuita Mwarabu! Nilipokuja kuisoma historia ya Mohammed Babu, nikachoka kuona nae anakuwa referred kama Mwarabu wa Hizbu!
"Watu wanapofilisika hoja.....hukimbilia ukaburu, ukabila......" Hyt Nyerere. CCM wanazidi kuanikwa kila siku.......Mungu yupo.UNAFKI MKUBWA ndivyo navoweza kuanza. Tumeona wawakilishi na mawaziri wengi machotara ukiwa CCM ni mzalendo. Nje ya hapo utabaguliwa na kuitwa majina ya kibaguzi. CCM imebaki na akili hizo iwe Zanzibar na hata bara ukionekana tishio kwa uhai wa ccm utaanzishiwa lugha za kibaguzi (ukabila, ngozi na kidini) kwa ujumla ni manyani yasioweza kuona matatizo yao huku wakitaka kusuhisha wengine wakati ya hapa kwetu tu hawawezi kupata suluhu.
Mkuu akili ni kama nywele...Nadhani hapo ndio upeo wako wa kufikiri ulipoishia. Kazi kwelikweli.