Ubaguzi ninaoupata Zanzibar, wakija Dar nitawapa haki yao

Ubaguzi ninaoupata Zanzibar, wakija Dar nitawapa haki yao

Kazini nanyanyasika sana. Pamoja na kuwa nina jina ambalo si la kikafir ila ubara wangu umekuwa kama kikwazo kwao.

Hapa mimi nmekuja kufanya kazi na ninajituma kiasi kuna wakati Boss anasema bila kuficha kuwa mimi ni mchapa kazi mzuri. Sina ukaribu naye yeye ni Raia wa kigeni. Anaona kazi zangu.

Nimetoka Dar tena nlikuwa naishi kwa sister, imagine. Nije kupiga kazi. Huku nanyanyasika sana. Wanasema nataka ufanyakazi bora. Wanasema najipendekeza kwa wakubwa nionekane.

Basi imekuwa ni maneno tu kwa hawa jamaa. Likitokea jambo tu utasikia "atakuwa huyo Mbara" kila jambo baya linahusishwa na mimi. Kuna siku mtu ka misplace simu yake akawa haioni. Anatafuta wanaongea kwa sauti kuwa wao huwa hawana hizo tabia atakuwa ni mtu mgeni ndo kaiba simu.

Bahati nzuri yule bwana alikuja ikuta simu yake kwenye gari lake chini ya seat kwa maelezo yake. Ila ilishaonekana kuwa mimi mbara ndo nitakuwa nimeiba. Binafsi sina tabia za wizi.

Jamaa wananinyanyasa, wananibagua waziwazi. Lakini nawaza jinsi ambavyo wapemba wanaishi nasi huku Bara. Wanaishi bila bugudha yoyote. Hawanyanyaswi wala kubughudhiwa.

Najua wanataka mwishowe niachie ngazi. Nami nawaambia naendelea kupiga kazi. Ila.... Watakuja home pia. Wanaamini katika haki nami ni muumini mzuri wa haki. Tutakutana tu.
Aisee...
 
Huu muungano inabidi upate majasiri wa kuongoza jahazi uvunjike
tumeshazoa ndugu wa damu mna hisi hii nchi ya tzn mna haki peke ynu lkn mtazoewea tu acheni kasumba za kifala huu muungano muolewa wa nchi mbili chuki na kasumba daima hazijwngi
 
Huo sasa ubaguzi, una agenda zako na wewe...uliposema hapo bora ukodishe panya kwa kuwa hio nyumba ina nini kikubwa?
Hao watanganyika wanaokuja zanzibar, wazanzibari nao wangesema hawawakodishi bora wakodishe panya si wangelala barabarani. Maana watanganyika wengine wanakuja zanzibar hawana hata issue, wanafuata mkumbo tu wa kuja kutafuta maisha Na huwa hawajui hata wataanzia wapi. Ndio wengine wakikuta nyumba hazijamaliza kujengwa wanavamia tu na kukaa hata kama hamna choo.
Kipindi naishi home mbweni, jirani kulikuwa kuna nyumba ndio kwanza imepauliwa tu...wakaja kuhamia wanyamwezi, walikuwa wanajisaidia kwenye mifuko na kutupa ovyo. Nyumba haina hata choo wala maji jiulize walikuwa wanakaa vp. Upande tuliokuwa tumepakana ukuta na hio nyumba kulikuwa kunanuka harufu ya uvundo. Sema tu walitukuta majirani hatuna midomo ya kugombana. Hapo bado usalama, ukisahau kitu nje asubuhi hukikuti washabeba
Umeandika kitabu sina mda wa kusoma. Nimeshasema nyumba sipangishi mzanzibari. Nyumba bado mpya nipangishe mzanzibari waifuje ichakae watu wenyewe wachafu bora waishi panya na mende.
 
ubaguzi ni ktk udhaifu wa kudumu wa binadamu. utegemee popote pale. kikubwa mfanyie wema aliyekufanyia wema, mzingue anayekuzingua. nishaacha kuwatazama watu kwa tofauti za nasaba zao.
 
Na sasa hivi tuna andaa proposal kwamba kuingia Zanzibar mpaka uwe na passport ila kwenda bara ni utawala wa manyani maana machogo mmezidi kuwa wengi sana huku Zanzibar.
Kabla ya kuweka passport. Mtoeni kwanza rais anayetoka ccm.
 
Majungu kazini kawaida Kuambiwa Unapiga Kazi Kujipendekeza kwa Wakubwa Au Kupandishwa Cheo Kawaida Mkuu.Puuza Fanya Lililokupeleka Kama Unataka Walipizia Kisasi Wakija bara Hakikisha Upo Kwenye Kampuni yako waajiri Watese Au Uwe Na Pesa Vinginevo Utabaaki Kulaani Baadala Ya kufanya Kazi
 
Piga kazi na usiwaonyeshe kwamba unaumia,wakijua kwamba unaumia kwaajili yao aisee watakutemea na mate,be happy🙂be humble.wasalimie vizuri tu cheka nao hata wakisema unajipendekeza sawa tu, jipe Raha mwenyewe.watakuelewa tu na watajirudi kwako.
 
Umeandika kitabu sina mda wa kusoma. Nimeshasema nyumba sipangishi mzanzibari. Nyumba bado mpya nipangishe mzanzibari waifuje ichakae watu wenyewe wachafu bora waishi panya na mende.
Kwa hio panya na mends ndio wasafi!!!?
 
Kikwete Mzanzibari? Ubaguzi upo tu kila sehemu.

Mbona alimbagua Dr. Salim Ahmed Salim kwa kisingizio cha Uhizbu tena hiyo ni baada ya Dr. Salim kushika nyadhifa nyeti kadhaa kitaifa na Kimataifa?!!
Dr Salim alikataliwa na Wazanzibar wenzake tangu enzi za Nyerere.
 
Kazini nanyanyasika sana. Pamoja na kuwa nina jina ambalo si la kikafir ila ubara wangu umekuwa kama kikwazo kwao.

Hapa mimi nmekuja kufanya kazi na ninajituma kiasi kuna wakati Boss anasema bila kuficha kuwa mimi ni mchapa kazi mzuri. Sina ukaribu naye yeye ni Raia wa kigeni. Anaona kazi zangu.

Nimetoka Dar tena nlikuwa naishi kwa sister, imagine. Nije kupiga kazi. Huku nanyanyasika sana. Wanasema nataka ufanyakazi bora. Wanasema najipendekeza kwa wakubwa nionekane.

Basi imekuwa ni maneno tu kwa hawa jamaa. Likitokea jambo tu utasikia "atakuwa huyo Mbara" kila jambo baya linahusishwa na mimi. Kuna siku mtu ka misplace simu yake akawa haioni. Anatafuta wanaongea kwa sauti kuwa wao huwa hawana hizo tabia atakuwa ni mtu mgeni ndo kaiba simu.

Bahati nzuri yule bwana alikuja ikuta simu yake kwenye gari lake chini ya seat kwa maelezo yake. Ila ilishaonekana kuwa mimi mbara ndo nitakuwa nimeiba. Binafsi sina tabia za wizi.

Jamaa wananinyanyasa, wananibagua waziwazi. Lakini nawaza jinsi ambavyo wapemba wanaishi nasi huku Bara. Wanaishi bila bugudha yoyote. Hawanyanyaswi wala kubughudhiwa.

Najua wanataka mwishowe niachie ngazi. Nami nawaambia naendelea kupiga kazi. Ila.... Watakuja home pia. Wanaamini katika haki nami ni muumini mzuri wa haki. Tutakutana tu.
Dogo fanya kazi acha ujinga.

Wanakunyanyasa?
Je wanakunyima.chakula? Wanakulaza Nje? Wanakubaka/kukulawiti?

Wafrika sisi ni wapumbavu.

Fanya kazi usiwe kama wale wajinga wanaoenda nje wanarudi mikono mitupu ukiwauliza wanasema walikuwa wanabaguliwa.

Huwa nawauliza tu ulinyimwa chakula? Ulilazwa nje? Ulifanyishwa kazi nje ya muda wa watu wengine? Ulinyimwa mshahara?

Sasa kama sio hayo unasemaje unabaguliwa?
Tatizo tunataka kwenda makazini kutafuta urafiki na kila mtu.

Chapa kazi kwa uaminifu sepa.

Unasingiziwa kuiba simu? Au unatabia hizo
 
Wacha kuwafuatilia,utaumia.
Hao wakiona huelewi wanakaa kikao,wanachanga pesa kisha safari ya kuelekea Pemba au Tanga inaanza.
Wakisharudi utajua tuu walienda kufanya nini maana huwa hawakai kimya na hapo sasa ndio utajutaa
 
Eti ni kweli mkuu Kalaga baho akijamba mwajuma mnasingiziwa nyie wa bara
Mm Sijakumbana nao huo hapo naskia sikia. Ila ofkooz Wana tendency ya kuhus ubara ni tatizo hasahasa katika mlengo wa maadili na tabia. Huku hata ujinga ni ulemavu.. unaweza kutengwa kimazungumzo kisa mitaa huijui au kinachozungumzwa hukijui..

Mm naona inategemea pia na tafsiri binafsi ya matukio unatofanyiwa na namna unavyoyabeba. Mm sioni tatizo hata wakiniuliza jina nawaambiaga Makame tu
 
Back
Top Bottom