Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetoa tahadhari ya ongezeko la maambukizi ya ugonjwa wa corona.
Katika taarifa yake iliyotumwa kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, ubalozi huo, umesema kuwa kumekua na taarifa za ongezeko la maambukizi ya virusi vya corona tangu mwezi Januari.
‘’…hatua za kuondosha na kuzuia maambukizi ya Covid-19 bado zimeeendelea kuwa za kiwango cha chini, serikali ya Tanzania haijatoa takwimu zozote kuhusu visa vya maambukizi au vifo vilivyotokana na Covid-19 toka mwezi Aprili 2020’’ inasema sehemu ya taarifa hiyo.
Ubalozi huo pia unasema hospitali na vituo vya afya nchini Tanzania vinaweza kuzidiwa kwa haraka na idadi ya wagonjwa.
‘’Uwezo mdogo wa hospitali nchini kote Tanzania unaweza kusababisha wagonjwa walio katika hali ya dharura kuchelewa kupatiwa huduma, jambo linaloweza kuhatarisha maisha.’’
Taasisi mbalimbali zimeendelea kutoa tahadhari ya maambukizi ya virusi vya corona.
Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Tanzania (SUA) ilitoa taarifa hapo jana kwa wanafunzi na wafanyakazi wake kujilinda dhidi ya maambukizi ya corona.
Nacho Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kilitoa waraka wa kuchukua tahadhari ya kujilinda na maambukizi ya corona.
Hata hivyo waraka huo ulibatilishwa na wizara ya elimu kwa kukiuka utaratibu uliotolewa na wizara ya afya.
Mwezi uliopita Kanisa Katoliki nchini Tanzania lilitoa tahadhari juu ya wimbi jipya la maambukizi ya corona na kuwataka wananchi kuchukua hatua zote za kujikinga.
Tahadhari hiyo ilitolewa kupitia waraka ulioandikwa na Rais wa Baraza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania (TEC) Askofu Gervas Nyaisonga.
Hata hivyo Wizara ya afya nchini humo bado haijathibitisha taarifa za uwepo wa wagonjwa au vifo vinavyo sababishwa na wimbi jipya la virusi vya corona.
Mara ya mwisho kutolewa kwa taarifa za mwenendo wa maambukizi ya virusi vya corona ilikua mwezi Aprili mwaka jana.
Chanzo
BBC
Tovuti ya Ubalozi wa Marekani
Health Alert – U.S. Embassy Dar es Salaam (February 10, 2021) Location: Tanzania Event: Increase in COVID-19 Cases The U.S. Embassy is aware of a