#COVID19 Ubalozi wa Marekani, watoa tahadhari dhidi ya ongezeko kubwa la ugonjwa wa Covid-19

#COVID19 Ubalozi wa Marekani, watoa tahadhari dhidi ya ongezeko kubwa la ugonjwa wa Covid-19

Nadhani ubalozi wa marekani unawaandikia audience ya wamarekani wanaozuru Tanzania tu.
 
Wakuingilie mambo yako ya ndani una kipi wewe hata net za wajawazito wanakupa msaada. Embu ondoa kelele hapa? Ati mambo ya ndani ? Kataa basi na ARV wanazokupa.na zile chanjo za wajawazito na watoto tengenezeni za miti shamba
Hongera kwa kumjibu huyo chumia tumbo wa lumumba
 
Tahadhari tunachukua popote tulipo, kifo kinatisha, kinaweza kuwa chanzo cha umaskini kwa familia zetu lakini tuutafute ukweli wa madawa tunayopewa.

Usisahau mwanzo kabisa walishapendekeza kwamba majaribio yafanyike afrika kwa kigezo wanatupenda na kutuhurumia sana kwakuwa hatuna health facilities za kutosha.

Sasa na sisi tuwaambie tuu kwamba Afrika haijaathirika kama USA EU na Asia, waanze kuokoa idadi kubwa ya watu wao wanaokufa Upendo wa kweli huanzia nyumbani

Hakuna upendo wa kuwapa watoto wa jirani chakula wakati watoto wako wanakufa njaa
Mnachukua tahadhali ya ugonjwa gani huo?
 
Vichaa wanajulikana nchi hii wapo sehemu gani kama siyo lumumba
Wale wanaokaa sehemu chafu pale ufipa huku wakipokea mabilioni ya ruzuku kwa miaka29 ndio vichaa, wenye utimamu wanatambulika hata makazi yao miaka29 pale lumumba
Mfyuuuu
 
Eti Mashoga wanatuchimba Mkwara!? Ebu watuache kwanza waendelee na ndoa zao za njisia moja!!
Bakuli lenu wanawajazia hao hao mabeberu baada ya kwenda kuwapigia magoti
 
Naamini corona ni ya msimu hata mwaka jana miezi hii corona ilikuwa kali ikapelekea hadi shule kufungwa...kwahyo naamini kuja kufika mwezi wa nne hadi wa tano itakuwa imepungua sana....tuzidi kuchukua tahadhari
 
Tuombe Mungu kifo hakina mjuaji
Kwahio ukiomba Mungu ndio utaishi milele ?

Tuache masihara kifo ni cha kila mtu (ila vifo vingi ni uzembe fulani labda kifo cha uzee) sasa watu wengi wanapougua au wanashindwa kupumua wanaenda hospital wanakosa huduma sababu mashine za oxygen hapo kama sio uzembe ni nini ?

Moja (hakuna mashine za kutosha / facility); jambo ambalo ni understandable sababu wagonjwa wanakuwa wengi ila uzembe ni pale kutowapa watu tahadhari ili wote tusiugue kwa wakati mmoja thus taasisi za afya kuzidiwa..., Uzembe wa pili ni kubeza watu wanaokesha kutafuta chanjo ili kutokomeza ugonjwa wakati mbezaji has nothing to show, wala hayupo mbioni kutafuta chanjo....
 
Nani kasema corona hakuna[emoji28][emoji28] kwani Mungu alikupatia masikio ya nini? Si angekupea macho na vidole vya kutype tuu[emoji849][emoji849][emoji849]

Itawagegda nyinyi wote mnao idharau
 
Hatimaye Beberu limetema cheche! [emoji95][emoji95][emoji95][emoji56] Tunasubiri tamko la kukanusha na pia kumuita mara moja Balozi wa Marekani kujieleza.
 
Wale wanaokaa sehemu chafu pale ufipa huku wakipokea mabilioni ya ruzuku kwa miaka29 ndio vichaa, wenye utimamu wanatambulika hata makazi yao miaka29 pale lumumba
Mfyuuuu
Vichaa wamejazana lumumba kwa maana tayari walisha jitambulisha kuwa wao ni vichaa na wengine wakasema kuwa wana mafaili yao mirembe.
 
Sasa ni wazi kua covid Tanzania inaua watu vibaya sana. Magufuli yeye bora watu waendelee kufa kuliko kuwaambia wachukue tahadhari za kisayansi, yeye anahimiza njia za kienyeji na za kishirikina za kujifukiza, kunywa pilipili, sijui kachumbari.

Ni mambo ya ajabu.
mkuu we binafsi una unapendekeza njia gani itakuwa sahihi katika kupambana na Corona.
 
Wao wamechukua hatua zote kama Kutoa taharifa kwa wakati kuzuia mikusanyiko na hatua nyingine lakini Nini kinaendelea mahambukizi yanazidi. by the way akuna anaye weza kukwepa kifo Kama ni Corona itapita na wewe na Kama sio utaendelea tu kuishi
 
Nani alikuambia nataka kuvuka mto, halafu hata nikivuka lazima niingie kwenye maji? Umepitwa na wakati wewe

😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅😅

Vijimaneno vya kwenye kanga vya kuokoteza
 
Corona inaua sio utani, rafiki kafariki tumemzika mchana, kaanza kuumwa asubuhi shida kupumua mchana kafariki saa tisa tumetoka kumzika, nilivyoona ile misafara ya Coaster inayosindikiza marehemu wao mikoani sina hamu kabisa.

Kama mpaka sasa bado kuna mtu asieamini Tanzania kuna Corona Mungu amrehemu.
Wapo tena wengi niliingia kwenye daladala juzi peke yangu Nina barakoa yaani watu wananikata jicho niliuchuna sikuivua mpaka nikafika napoenda na wakati WA kurudi hivyohivyo. SASA hivi nikitoka nje ya Geti ni barakoa Tu. Ndugu wawili tumeshazika wiki 2 hizi.
 
Kuna Watanzani ni wajinga sana, mtu anakutahadhalisha kuhusu jambo la hatari unasema hana malengo mazuri na sisi. Serious?
Hivi nyie watanzania mnasema mnamuomba afu hamchukui tahadhari ni Mungu yupi mnemuomba, au mmerudia kuabudu miungu ya mababu zenu waliokua wanaiabudu kabla ya kuja hawa wazungu mnaowaita mabeberu kuwaambia jinsi ya kumuabudu Mungu wa kweli.
Huyo Mungu mnaesema mnamwabudu si ndo aliwatumia hawa wazungu kuja kuwambia muache kuabudu Miungu mingine Ila mumwabudu Mungu Mmoja tu ambaye ni Alfa na Omega.
Tuache utani wa hawa wanasiasa wenu, tuchukue tahadhari.
Achani kumjaribu Mungu, kwamba eti nitapita hapo kati kati ya mamba Mungu yupo atakupigania.
Hata wachungaji mnawaamini wanasiasa ambao wanaenda kuroga kupata vyeo, Leo ndo wawe wa kuwatabiria kwamba sisi watanzania hatutakiwi kuchukua tahadhari ya corona Mungu atatupigania.
Mungu hajaribiwi kama ambavyo Yeye hamjaribu Mtu
 
Back
Top Bottom