Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
1. Mwomba huduma sie anaepanda kwa chombo cha kusafiria, bali anamwombea rafiki/nduguu usafiri na kulipia
2. Madereva waliojiunga na Uber ili kutoa huduma kwa wateja kukosa uaminifu/uadilifu etc
3. Mazingira ya biashara kila uchao taratibu zabadilika za uendeshaji biashara kwa tz
4. Gharama na mifumo ya barabara kwa tz
Kama la kondeboiNitamnunulia gari
Kama alivyorudi dubai akaja na ushauri wa SGR kutumia mabasi ya umeme?Taratibu mmoja mmoja atafunga virago. Lazima tufike uchumi wa kati.
Mama akirudi toka vacation Marekani atakuja na mbadala wa Uber.
Ni kuanzia tarehe 14..ikifika saa 6 usiku leo ndio mwishoMbna inafungukaView attachment 2186727
Tumefanya uamuzi mgumu wa kusitisha huduma zetu nchini Tanzania kuanzia Alhamisi ya Tarehe 14 Aprili 2022.Request..
Tena wanaomba special namba ili wavunje sheria bila kusimamishwa na trafic watumiapo barabara.Wao si wanasafiri na chopa ndiyo maana hawajali maumivu ya waTz.
Ni vigumu sana kwa nchi yetu kuendelea kwa mfumo hovyo wa ccm uliopo madarakani, yubsdilishe.Wakuu,
Usiku huu Uber wametuma ujumbe unaosomeka hivi:
👇🏾
Huduma ambayo ilianza kama wazo tu — la kutumia simu yako kupata usafiri ndani ya dakika chache— Mfumo wa Uber umeenea duniani kote na zaidi ya safari milioni 15 hufanyika kila siku kupitia kwenye mfumo huu. Imekuwa ni heshima kubwa kupata nafasi ya kusaidia watu kupata usafiri duniani wanapofanya shughuli zao na kutangamana na watu wengine.
Lakini, maandalizi ni sehemu muhimu katika kufikia malengo ya siku za usoni.
Siku zote, lengo letu ni kuwa mshirika muhimu katika miji mbalimbali kwa kutoa usafiri wenye ufanisi, kutengeneza fursa za kiuchumi zinazowapa madereva uhuru wa kujiingizia kipato kwa muda wanaotaka wao na kuchangia katika mapato ya serikali. Na tumelisimamia lengo hili tangu tulipofungua milango yetu katika jiji la Dar es Salaam mwaka 2016.
Sera za usimamizi zinapaswa kuwa chachu wala sio kikwazo cha ubunifu
Tumefanya uamuzi mgumu wa kusitisha huduma zetu nchini Tanzania kuanzia Alhamisi ya Tarehe 14 Aprili 2022. Nauli elekezi iliyowekwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imesababisha changamoto kubwa kwa mifumo kama Uber kuendelea kutoa huduma kwa wateja wetu. Inakua ngumu kwetu kuendelea kutoa huduma. Hatuta weza kutoa huduma mpaka pale mazingira yatakapo kua rafiki kwa sisi kuendelea kutoa huduma.
Kipaumbele Chetu: kuwasaidia Madereva Watanzania
Uamuzi huu umekuja baada ya mamlaka kuweka kanuni ambazo ni changamoto kubwa kwa mifumo kama Uber kuendesha biashara yake. Tutafanya kazi kwa karibu na madereva kwenye mpito huu.
Tuweke Wazi: Tungependa sana kuendelea kutoa huduma zetu nchini Tanzania
Nchi ya Tanzania kupitia Dira ya Maendeleo ya 2025 imedhamiria kujenga uchumi imara, anuwai, himilivu na shindani ambao unaendana na mabadiliko ya masoko na kiteknolojia kikanda na kimataifa. Tulitegemea kwamba hii ingejumuisha kujenga mazingira wezeshi ili biashara ya ndani na kimataifa inawiri katika njia nzuri na yenye usawa, lakini kwa bahati mbaya, hali ni kinyume na matarajio.
Tutarudi kuzindua huduma zetu mara tu kutakapokuwa na kanuni mpya.
Ingawa tumefunga huduma za UberX, UberXL na UberX Saver nchini Tanzania, tuko tayari kushirikiana na mamlaka husika katika kuunda kanuni ambazo zitawezesha teknolojia kunawiri, ili tuanze tena kutoa huduma zetu zinazopendwa na watu wengu.
Asante, Tanzania!
Enzi zile tungekuwa tayari tumeshaanza mchakato wa kutengeneza Uber ya sirikali, tenda lingepewa Jeshi[emoji205]
Ni vigumu sana kwa nchi yetu kuendelea kwa mfumo hovyo wa ccm uliopo madarakani, yubsdilishe.
Naomba kuuliza, hivi nikirequest uber akaitumia mtu mwingine shida inakua ni nini hapo? mie ilikua ndio zangu hizo.Sasa mama atawaweza wabongo.
Wabongo wanataka Magu.
Ili la mtu kumuitia uber mtu mwingine muitaji si mpandaji, madereva sio aliyesajiliwa na chombo yaani kampa deiwaka.
Madereva Wana namna yao ya kucheza unapewa bei tofauti na uliyoomba ukosefu wa uaminifu.
Hapo ni SAwa na kumuagizia kinywaji ndugu yakoNaomba kuuliza, hivi nikirequest uber akaitumia mtu mwingine shida inakua ni nini hapo? mie ilikua ndio zangu hizo.
Tuvumilie tu, maana anaupiga mwingi mno, wengi walishangilia nchi imefunguliwaKumeumana hali ngumu na screw zinaongezeka.