Ubora wa Lugha ya Kiswahili " Kwishnei"

Hata hizo alama za uandishi ("....." ) *funga,fungua semi*, unazoziita mabano nao ni upotoshaji upotoshaji na uharibifu wa lugha yetu.....!!

Usahihi wake ni upi, mkuu?
 

Kuhusu Dr. Magufuli hapo umekwenda kombo. Yeye ni mtaalamu wa kuchanganya lugha ya kiingereza na kiswahili katika hotuba zake.
 
Maneno mengine yanayo udhi kuyasikia ni kama haya:- Mdada, Mbaba, Mmama, Mkaka n.k. Mpaka hapo BAKITA, na Wahariri wa Magazeti bado wapo kimya tu.

Maneno mengine haya hapa: Noma, Kusepa, Kula nyoro, Ulabu, Kupiga chabo, Ndivyo sivyo n.k. Wahusika wenye dhamana wanaendelea 'kuchapa' usingizi.
 
Maneno mengine haya hapa: Noma, Kusepa, Kula nyoro, Ulabu, Kupiga chabo, Ndivyo sivyo n.k. Wahusika wenye dhamana wanaendelea 'kuchapa' usingizi.

Lakini nadhani Neno ULABU na NDIVYO SIVYO, Ni kiswahili fasaha. Sijui kuhusu KUPIGA CHABO. Nadhani hata Neno KUPIGA CHABO, ni msemo sahihi wa Kiswahili.
 
wewe mwanamke ni mbulula kweli, khaa
 
Tena ilitakiwa hawa wasanii wa muziki na filamu wakitoa kazi mpya tu lazima kwanza zipitiwe na wataalam wa lugha ili kuboreshs lugha yetu tukufu
 
Mimi naenda Tabola ntakaa kama li wiki li moja na ninategemea kuludi kupitia Alusha ntapumzika kama li saa limoja tu kisha ntaendedelaga na safari yangu mpaka kologwe ( Hiki ndio Kiswahili cha sasa ni upuuzi mtupu ukimsikia mtu anaongea namna hii ndio unajua sasa Kiswahili imekua lugha isiyokuwa na wakuiendeleza na BAKITA wamelala)
 

Nikweli ndugu yangu. Na watu hawa sasa hivi wengi wao wamo kwenye uandishi wa habari. Na wenyewe wanadhani wapo sahihi.
 
Nakushukuru mleta mada. Ni dhahiri kuwa unaguswa vilivyo na tabia hii mbovu ya kuharibu lugha yetu iliyo tamu kinywani kama titi la mama mzazi.
Nami binafsi ninaumia katika hilo. Jambo hili kwa mawazo yangu lina mizizi kwa wadau wawili:
1. Hatuna au kuna uhaba wa walimu bora wa kufundisha watoto kusoma na
kuandika lugha hii ( hasa matamshi )
2. Tasnia ya habari hasa waandishi wengi hawana ujuzi wa lugha hii hivyo
wanakuwa wabanangaji tu.
Makundi haya mawili kama yangelikuwa na umakini katika maeneo yao nina hakika lugha yetu isingelifikia hapa ilipo. Ni aibu kuwa na watangazaji au waandishi wa habari na walimu wasio na ujuzi wa lugha yao, tena kibaya zaidi hii lugha kwa sasa ni lugha ya kwanza kwa wengi wetu!
Ushauri:
Kama kweli tunaipenda lugha hii, tutafute,tununue na tuvisome kwa wingi vitabu vya waandishi mahiri wa lugha ya Kiswahili akina Almarhum Shaaban Ufuko Robert, Profesa Abdallah Safari, Mohamed S. Abdullah na wengineo ili tujifunze msamiati halisi wa lugha hii na kuutumia mahala na wakati sahihi na si kubananga au kuchanganya lugha ovyo ovyo kama vile wewe ni mgeni na ndio umeanza kujifunza lugha hii.
Binafsi sijawahi kumuona au kumsikia raia wa bara la Ulaya tena mzungu akichanganya labda kiingereza na kifaransa wakati akiongea. Ugonjwa huu tunaumwa sisi.
Kwa walimu muwe tayari kujifunza kila wakati hasa matamshi sahihi ili watoto wetu wajifunze kutamka maneno kwa usahihi kutoka kwenu kwani wao ndio waandishi na walimu wa baadaye.
Asante mleta mada!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…