Kwa vile mchakato wa kuwapata wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, umetangazwa, nashauri ili taifa lipate wawakilishi wazuri na makini, tufanye mambo mawili yafuatayo
- Kwa waliokuwa wawakilishi wetu kwenye Bunge hilo ambao wanataka kuwania kuendelea kwa awamu yaa ya pili, waulizwe katika uwakilishi wao, ndani ya Bunge hilo kwa miaka 5 iliyopita, wamechangia nini na wamelisaidia nini taifa?. Taarifa zao ziandamane na uthibitisho wa hansard ya Bunge hilo, ili wale waliotuwakilisha vizuri, ndio wapewe fursa ya kugombea kipindi cha pili, tuwarudishe, na wale mabubu, tuwashukuru kwa uwakilishi wao kwa kuwaambia asante, tuwapumzishe!. Baada ya kuiingiza DRC ndani ya EAC na ujio wa AfCFTA, hizi sio zama za Tanzania kuwakilishwa na mtu ili mradi ni mtu, we real need competent people kutuwakilisha.
Karibuni.
Paskali.