Ubunge sio the Comedy; Kwako Steve Nyerere

Ubunge sio the Comedy; Kwako Steve Nyerere

UBUNGE SIO THE COMEDY

Na, Robert Heriel

Ujumbe huu ni mchungu lakini naomba ufike kama nilivyokusudia, pengine maneno yake yakawa makali. Hivyo natoa angalizo; Kama unaroho nyepesi na mihemuko ya karibu tafadhali usisome.

Kuna kitabia cha kipuuzi Baadhi ya wasanii wanacho, yaani mtu akishahisi amekuwa maarufu anaona tayari ameshafuzu kupewa ubunge. Jambo ambalo sio sahihi.

Ubunge sio the Comedy, ubunge sio bongo movi sijui bongo fleva, Ubunge sio kukata mauno na kuimba imba matusi. Tunajua mambo hayo yamewasaidia kuwapa umaarufu, tunafahamu mambo hayo ndio yanaendesha maisha yenu na familia zenu. Lakini Watanzania hatutakubali usanii wenu ndio iwe ticketi ya kutuongoza sisi Watanzania kwa nafasi ya Ubunge.

Hatutaki bunge la vichekesho, bunge la vikatuni, bunge la watu wanaopenda kiki. Bunge hilo hatulitaki.
Mifano tunayo ya wabunge ambao ni vikatuni, yaani mbunge akichangia hoja anaongea vioja na vituko akitafuta umaarufu wa kipuuzi. Tena wabunge wengine ni watu wazima kabisa lakini ni vikatuni.

Hatutaki waheshimiwa Vikatuni, yaani ukiangalia bunge utadhani unatazama Tommy na Jerry hiyo hatutakubali.

Tupo Karne ya 21 hatutatumia kigezo cha kujua kusoma na kuandika katika kuchagua viongozi. Vigezo vifuatavyo tutazingatia:
1. Maadili na Uzalendo
2. Uchapakazi
3. Elimu kuanzia kidato cha sita kuendelea.
Wewe kama huna vigezo tajwa hapo mwaka huu utausikia kwenye bomba. Jamii makini haiwezi ongozwa na jitu ambalo halina maadili na uzalendo, jitu ambalo halijaenda shule, jitu sio lichapakazi.

Watanzania sasa wameamua kuleta mabadiliko, na mabadiliko hayaletwi na Vikatuni, the comedy, sijui waigizaji gani huko. Angalau kikatuni kiwe kimeenda shule, au comedian aliyeenda shule, au hata Mwanamuziki aliyeenda shule. Lakini kama shule hakuna huna nafasi katika bunge mwaka huu.

Jamii jinga ndio itachagua vikatuni, itaongozwa na watu wasioenda shule, wapiga domo tuu. Hivi mtu ambaye hajaenda shule atashauri nini kwenye ulimwengu wa sayansi na teknolojia, hatuwezi kurudishwa enzi za zama za mawe.
Steve, Shilole, harmonizer, na wengineo ambao shule ni ndogo muache kutuletea ukatuni.

Nitashangaa majimbo husika ikiwa yatakubali kuongozwa na watu wasio na elimu. Nitashangaa chama kitakachowapitisha watu wasio na elimu awamu hii.

Hatutaki wagonga meza bungeni, hatutaki waongea utumbo bungeni, hatuna muda wa kuwachagua.

Nafurahia majimbo yanayojielewa, majimbo yanayotaka mabadiliko chanya, ndio maana wanachagua watu wenye elimu ili kuhamasisha watoto waendelee kusoma. Na ndio maana kuna utofauti wa maendeleo baina ya jimbo na jimbo.
Huwezi ongozwa na Mtu asiye na elimu akaleta mabadiliko chanya ndani ya jamii. Ni upuuzi mtupu.

Wasanii wote wasiosoma piga chini.
Sijui Steve Nyerere Piga chini
Sijui Shilole Piga chini
Sijui Harmonizer garagaza chini
Wote wa Darasa la saba B piga chini.
Sijui Msukuma piga chini.
Na wote wa namna hiyo piga chini.

Tanzania ya viwanda haitaletwa na wabunge ambao hawajaenda shule. Ni uongo wa mchana.

Hata kama Katiba inasema kila mtu anayohaki ya kugombea uongozi ilimradi ajue kusoma na kuandika lakini tuangalie ilisema lini na sasa hivi tupo wapi.

Hatutaki kuongozwa na wajinga sisi.

Nimemaliza.

Taikon wa Fasihi, niko njiani kuelekea Same kuchukua fomu ya ubunge.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
2299526_STEVE_NYERERE_KUMVAA_MSIGWA_IRINGA_MJINI.__Steven_Mengele_Steve_Nyerere_ametan__661_X_...jpg
 
Ukitaka kuoina seriousness ya nchi yoyote ni kwenye mambo kama haya. Wakati jirani zetu Kenya wakitaka mbunge au seneta awe na digrii ya kwanza na kuendelea sisi huku tuko busy kushikilia kigezo cha darasa la saba what a fuckin mistake. . . .
Na ndio maana hata kimaendeleo wametupiga bao sana kwa sababu bunge lao na senate yao imejaa vichwa vinavyofikiri na sio wagonga meza kama sisi tulionao huku. Naiunga mkono hoja yako kupinga bunge la vikatuni
safi kabisa ni ujinga kuwa na bunge la vilaza kichwana kwakwe unakuta hana article yoyote ambayo aliwa soma zaid ya mesej za kuchambana insta
 
Ukitaka kuoina seriousness ya nchi yoyote ni kwenye mambo kama haya. Wakati jirani zetu Kenya wakitaka mbunge au seneta awe na digrii ya kwanza na kuendelea sisi huku tuko busy kushikilia kigezo cha darasa la saba what a fuckin mistake. . . .
Na ndio maana hata kimaendeleo wametupiga bao sana kwa sababu bunge lao na senate yao imejaa vichwa vinavyofikiri na sio wagonga meza kama sisi tulionao huku. Naiunga mkono hoja yako kupinga bunge la vikatuni

Watu wanadharau sana, yaani kuruhusu watu kama hawa bungeni ni kudharau bunge na nchi kwa ujumla
 
Mwaka 2015 Kingwendu nae aligombea ubunge Kisarawe.

Tanzania watu wana masihara sana. Au sijui ni bunge wanalidharau ndio maana wanapata guts za kugombea ubunge? Nadahani Bunge lingekuwa imara, kali, serious na la kiweledi watu wangejipima kabla ya kugombea.

Pigia mstari hapo kuanzia aya ya pili.Ndipo penye jibu kwanini watu kama Steve wanapata uthubutu wa kufikiria kwamba wanamudu kazi ya ubunge Tanzania.

Ni kwamba bunge lenyewe limeshajishusha viwango.

Kwa sasa bungeni panaonekana kama sehemu ya kupiga soga na kupitisha muda tu huku ukisubiri miaka mitano iishe upate kiinua mgongo chako.

Naamini kwa aina ya bunge letu na mijadala inayofanyika mule ndani,sio Steve tu hata msela yeyote wa mtaani anamudu kabisa kazi ya ubunge.
 
Tupo Karne ya 21 hatutatumia kigezo cha kujua kusoma na kuandika katika kuchagua viongozi. Vigezo vifuatavyo tutazingatia:
1. Maadili na Uzalendo
2. Uchapakazi
3. Elimu kuanzia kidato cha sita kuendelea.
Wewe kama huna vigezo tajwa hapo mwaka huu utausikia kwenye bomba. Jamii makini haiwezi ongozwa na jitu ambalo halina maadili na uzalendo, jitu ambalo halijaenda shule, jitu sio lichapakazi.

Watanzania sasa wameamua kuleta mabadiliko, na mabadiliko hayaletwi na Vikatuni, the comedy, sijui waigizaji gani huko. Angalau kikatuni kiwe kimeenda shule, au comedian aliyeenda shule, au hata Mwanamuziki aliyeenda shule. Lakini kama shule hakuna huna nafasi katika bunge mwaka huu.
Halafu ni kwa nini tusifikirie kuwa na wabunge walio kwenye standard kama za kina Zitto, Heche na hata kina Seleli na Filikunjombe wa siku za nyuma?
 
UBUNGE SIO THE COMEDY

Na, Robert Heriel

Ujumbe huu ni mchungu lakini naomba ufike kama nilivyokusudia, pengine maneno yake yakawa makali. Hivyo natoa angalizo; Kama unaroho nyepesi na mihemuko ya karibu tafadhali usisome.

Kuna kitabia cha kipuuzi Baadhi ya wasanii wanacho, yaani mtu akishahisi amekuwa maarufu anaona tayari ameshafuzu kupewa ubunge. Jambo ambalo sio sahihi.

Ubunge sio the Comedy, ubunge sio bongo movi sijui bongo fleva, Ubunge sio kukata mauno na kuimba imba matusi. Tunajua mambo hayo yamewasaidia kuwapa umaarufu, tunafahamu mambo hayo ndio yanaendesha maisha yenu na familia zenu. Lakini Watanzania hatutakubali usanii wenu ndio iwe ticketi ya kutuongoza sisi Watanzania kwa nafasi ya Ubunge.

Hatutaki bunge la vichekesho, bunge la vikatuni, bunge la watu wanaopenda kiki. Bunge hilo hatulitaki.
Mifano tunayo ya wabunge ambao ni vikatuni, yaani mbunge akichangia hoja anaongea vioja na vituko akitafuta umaarufu wa kipuuzi. Tena wabunge wengine ni watu wazima kabisa lakini ni vikatuni.

Hatutaki waheshimiwa Vikatuni, yaani ukiangalia bunge utadhani unatazama Tommy na Jerry hiyo hatutakubali.

Tupo Karne ya 21 hatutatumia kigezo cha kujua kusoma na kuandika katika kuchagua viongozi. Vigezo vifuatavyo tutazingatia:
1. Maadili na Uzalendo
2. Uchapakazi
3. Elimu kuanzia kidato cha sita kuendelea.
Wewe kama huna vigezo tajwa hapo mwaka huu utausikia kwenye bomba. Jamii makini haiwezi ongozwa na jitu ambalo halina maadili na uzalendo, jitu ambalo halijaenda shule, jitu sio lichapakazi.

Watanzania sasa wameamua kuleta mabadiliko, na mabadiliko hayaletwi na Vikatuni, the comedy, sijui waigizaji gani huko. Angalau kikatuni kiwe kimeenda shule, au comedian aliyeenda shule, au hata Mwanamuziki aliyeenda shule. Lakini kama shule hakuna huna nafasi katika bunge mwaka huu.

Jamii jinga ndio itachagua vikatuni, itaongozwa na watu wasioenda shule, wapiga domo tuu. Hivi mtu ambaye hajaenda shule atashauri nini kwenye ulimwengu wa sayansi na teknolojia, hatuwezi kurudishwa enzi za zama za mawe.
Steve, Shilole, harmonizer, na wengineo ambao shule ni ndogo muache kutuletea ukatuni.

Nitashangaa majimbo husika ikiwa yatakubali kuongozwa na watu wasio na elimu. Nitashangaa chama kitakachowapitisha watu wasio na elimu awamu hii.

Hatutaki wagonga meza bungeni, hatutaki waongea utumbo bungeni, hatuna muda wa kuwachagua.

Nafurahia majimbo yanayojielewa, majimbo yanayotaka mabadiliko chanya, ndio maana wanachagua watu wenye elimu ili kuhamasisha watoto waendelee kusoma. Na ndio maana kuna utofauti wa maendeleo baina ya jimbo na jimbo.
Huwezi ongozwa na Mtu asiye na elimu akaleta mabadiliko chanya ndani ya jamii. Ni upuuzi mtupu.

Wasanii wote wasiosoma piga chini.
Sijui Steve Nyerere Piga chini
Sijui Shilole Piga chini
Sijui Harmonizer garagaza chini
Wote wa Darasa la saba B piga chini.
Sijui Msukuma piga chini.
Na wote wa namna hiyo piga chini.

Tanzania ya viwanda haitaletwa na wabunge ambao hawajaenda shule. Ni uongo wa mchana.

Hata kama Katiba inasema kila mtu anayohaki ya kugombea uongozi ilimradi ajue kusoma na kuandika lakini tuangalie ilisema lini na sasa hivi tupo wapi.

Hatutaki kuongozwa na wajinga sisi.

Nimemaliza.

Taikon wa Fasihi, niko njiani kuelekea Same kuchukua fomu ya ubunge.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kunywa Maji Mwanangu sio kwa povu hilo umetoa mpaka nguo zimetakata! Ata pia umetoa ya Moyoni yanayokusumbua
 
Acha mambo ya kibwege, kila mtu ana haki ya kugombea ubunge awe tu ametimiza masharti!
 
Watu wanadharau sana, yaani kuruhusu watu kama hawa bungeni ni kudharau bunge na nchi kwa ujumla
Hakika ila tukisema wengine wanakuja juu. Fikiria, tumekuwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni (KUB) aliyepata div-0 form six na baadaye kuwa DJ kwenye kumbi za disco (bilcanas). Matokeo yake hahudhurii vikao vya kamati ya uongozi, kamati ya bajeti, n.k na kusababisha bunge na nchi kukosa uwakilishi mzuri na safu ya upinzani kudorora.

Ni wakati sasa wa kuchagua wabunge wenye upeo. Kujua kusoma na kuandika ni minimum standard ili kukidhi demokrasia za kinafiki duniani basi. Ila ukweli unajulikana bunge linahitaji wasomi na sio cereblities.
 
Ujinga ndo mtaji wa chama cha mapinduzi kuendelea kutawala...

Fikiria Bunge likiongozwa na Spika linaacha kujadili bajeti ya serikali wanaanza kujadili ulevi wa mtu...Ni sahihi hao kina Steve na Shilole waone ubunge ni kazi rahisi kwa maana kujadili watu ndo kazi zao.
 
CCM ipeleke bungeni wabunge mahiri, wenye maarifa na uwezo wa kuisaidia serikali ya chama chao kuongoza vizuri nchi.
Bungeni kusijae watu ambao hakuna linaloenda vila fitna, majungu na mambo yanayoendana na hayo. Tusidanganyane, tunahitaji wabunge ambao hata wakipewa uwaziri, watajituma kutimiza wajibu wao
 
Kazi ya kua mbunge kwa nchi hii ni kama zawadi kutoka kwa viongozi wa vyama vya siasa. Sio upinzani sio chama tawala... Wale wabunge wa viti maalum hata sijui ni wa kazi gani? Nchi hii bado kuna sehemu hatupo serious. Bunge ni chombo muhimu cha kuinyoosha serikali inapopinda, sio kushangilia na kutukana tu au kufanya fujo. Bado naiona nchi yangu ina safari ndefu sana ya kwenda kwenye uchumi wa kati
 
Huyu si ndiye wanayemtaja kuwa ni KUWADI WA MADADA wa Bongo na baadhi ya watu maarufu bongo.

Au siye?
 
Shida sio kutokusoma kwao, wanagombea ubunge kupitia chama gani?, kama ni kupitia vyama pinzani imekula kwao.
 
Back
Top Bottom